Tuesday, November 24, 2009

Lishe duni inadumaza ukuaji wa watoto

NA MWANDISHI WETU


24th November 2009















Watoto wakisubiri mgao wa chakula.

Utapiamlo kwa watoto bado ni tatizo kwa nchi zinazoendelea duniani ingawa wataalam wanasema nchi nyingi zimeweza kupiga hatua .

Moja ya tatu ya vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kwenye nchi hizo zinahusishwa na ulaji duni , ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto (Unicef) inasema.

UNICEF wanasema pia kuwa katika watoto wapatao milioni 195 mmoja kati ya watatu amedumaa kutokana na kukosa lishe bora , ingawa kiwango chao kimekuwa kikipungua kuanzia mwaka 1990.

Ripoti hiyo inaeleza pia kuwa idadi ya watoto ambao wana uzito mdogo ukilinganisha na umri wao imebakia kubwa huku nchi nyingi zikifanya jitihada ili kuweza kufikia malengo yanayotakiwa walao kupunguza idadi hiyo ifikie nusu yake.

Kiwango cha watoto wanaodumaa kukua kinaweza kuwa kikubwa kwa sababu wakati watoto wengine wana uzito wa kawaida wako pia watoto ambao wana uzito mkubwa zaidi- hii ni kutokana na kuwa chakula wanachokula ni duni na hivyo kuathiri ukuaji wao.

Wataalam wanaonya kuwa mara nyingi hali kama hiyo ikitokea ni kitu kisichoweza kurekebishwa na mara nyingi inamfanya mtu kama huyo abakie na afya mbaya maisha yake yote.

Kiongozi wa Unicef, Ann Veneman anasema kuwa : " Lishe duni inawanyima watoto nguvu kiasi kwamba baadhi ya magonjwa ambayo mwili ungeweza kupambana nayo unaweza ukashindwa na hiyo ni hatari kwao”.

"Kama hatua za lazima hazitachukuliwa ili kuhakikisha kuwa mama na mtoto wanapata chakula bora tujue kuwa gharama yake itakuwa kubwa siku za baadaye.."

Tunawezaje kumaliza tatizo hilo

Moja ya maeneo ambayo yamefanyiwa kazi ni huko Peru, Amerika ya Kusini ambako tatizo la lishe duni lilikuwa kubwa.

Mwaka 1999, serikali ya nchi hiyo kwa kushirikiana na Unicef walianzisha kwa pamoja na shirika la Maendeleola Marekani mradi wa kuwahudumia watoto katika umri mdogo.

Mradi huo uliweza kuwatumia wafanyakazi wa afya kutoa huduma kwa akina mama baada ya kujifungua kwa kuwahimiza kunyonyesha watoto na kutoa chakula cha kulikiza katika majimbo matano ya vijiini.

Ilipofika mwaka 2004, zaidi ya watoto 75,000 waliokuwa chini ya miaka mitatu ambao walikuwa wananufaika na mpango huo kiwango cha watoto wengi kudumaa kilipungua kutoka asilimia 54 hadi kufikia 37.

Mpango huo kwa sasa unaendeshwa kwa nchi nzima ambapo wataalam wanaeleza kuwa siku za kwanza 1,000 za mtoto ambazo ni sawa na miaka mitatu ya mwanzo ni muhimu ili kuweza kutatua tatizo hilo.

Wataalam hao wanasema kuwa suala la kuhimiza unyonyeshaji katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo ni muhimu.

Hata hivyo Unicef wanasema kuwapatia watoto pia vyakula vya ziada ni suala litakalosaidia tatizo la lishe duni

Mipango mingi inayohusiana na lishe imekuwa ikiongeza madini ya joto kwenye chumvi ili kuwasaidia watoto kupata madini hayo yanayochangia katika ukuaji wa ubongo pia kuwapatia vitamini Ambayo inasaidia katika ukuaji wa mifupa na kuuwezesha mwili kupambana na maambukizo.Hatua kama hiyo repoti hiyo ya Unicef inasema itasaidia kupunguza moja ya tano ya vifo vya watoto.

Unicef inasema kuwa kwa kushirikiana na wadau wengine zikiwemo na serikali husika na mashirika ya misaada imekuwa ikipiga hatua katika kuboresha lishe kwa watoto kwenye nchi 150 zinazoendelea.

Kuanzia mwaka 1990 uwiano wa watoto ambao wanakuwa na uzito mdogo imepungua kwa kiwango cha moja ya sita ,kulingana na mipango na takwimu ambazo Unicef na mashrika menginge wanayofuatilia suala hilo kama Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia.

Hata hivyo pamoja na hatua hizo zote kuchukuliwa kwenye baadhi ya nchi hali ni mbaya kwani takwimu zinaonyesha kuwa kati ya nchi 117 ambazo zina tatizo hilo ni nchi 63 tu ndizo zitaweza kufikia Malengo ya Milenia katika kipengere hicho ambapo lengo ni kupunguza nusu ya idadi ya watoto wanaokuwa na uzito mdogo ifikapo 2015.

Kwa upande wa Afrika hali ya mafanikio bado siyo makubwa wakati nchi za Asia zina afadhali kidogo na wakati Amerika ya Kusini imekuwa ikipiga hatua zaidi.

Kitty Arie, mtaalam wa masuala ya sera kwenye shirika la Save the Children, anasema kuwa lishe duni ina madhara ya muda mrefu ikiwemo mtoto kushindwa kufanya vizuri shuleni.

"Hili ni suala muhimu sana na linawezakana na ni lazima litafutiwe dawa.."

No comments:

Post a Comment