Wednesday, November 25, 2009

Huu si wakati wa Kukata tamaa



Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe

Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha yanaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu familia zetu, jamii zetu, au nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?".

Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kujihisi kuvunjwa moyo (discouraged) na hivyo kuona kuwa hakuna lolote na chochote kinachoweza kufanyika Tanzania ambacho kinaweza kuturudisha kwenye matumaini?

Je huu ndio wakati wa kukata tamaa na kuwaachia mafisadi wafanye wapendavyo? Je huu ndio wakati wa kukubali viongozi wabovu na wasio na uwezo alimradi tuendelee katika hali ya utulivu, amani na mshikamano? Je huu ni wakati wa kusalimu amri na kukubali kile ambacho kimetuangukia na kuwa yote ni "mapenzi ya Mungu"?

Je unajihisi kukata tamaa ukiangalia mambo yanayoendelea katika nchi yetu?

Niandikie:

No comments:

Post a Comment