tag:blogger.com,1999:blog-37694459520681433582024-03-13T02:03:34.078+03:00Kyela Community InitiativesKyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.comBlogger49125truetag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-47547510599674566682010-01-01T09:41:00.000+03:002010-01-01T09:41:01.582+03:00SALAMU ZA MWAKA MPYA WA 2010Tovuti ya Kyela Community Initiatives inawatakia heri ya mwaka mpya wasomaji na wapenzi wa tovuti hii. Mungu awape nguvu na furaha katika maisha yenu na familia zenu. Mwaka huu wa 2010 uwe ni wenye mafanikio kwako na familia yako. Tovuti hii inaomba radhi kwa kutoweza kutoa maada kwa mwezi wa Decemba, 2009 kwa sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wake. <br />
<br />
Lakini tunapenda kuwaahidi kuwa muda si mrefu mtaendelea kupata maada nzuri na zitakazosaidia maedeleo ya jamii zetu na Taifa letu la Tanzania kwa ujumla.<br />
<br />
Mungu wabariki Watu wako hapa Duniani ili wakujue kuwa wewe ndiye muweza.<br />
<strong>Kyela Community Iniatives</strong>.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-41573916371092071322009-11-30T15:35:00.000+03:002009-11-30T15:35:12.935+03:00USALAMA WA TAIFA NI LAZIMA UBADILIKE, KAMA TUNATAKA TUSALIMIKE! – Sehemu ya 1Na. M. M. Mwanakijiji<br />
<br />
<br />
Usalama wa taifa wa nchi yoyote ile duniani ndiyo kinga ya mwisho dhidi ya tishio lolote la uhuru wa taifa hilo. Nitarudia tena kauli hii. Usalama wa taifa wa nchi yoyote ile duniani ndiyo kinga ya mwisho dhidi ya tishio lolote la uhuru wa taifa hilo. Usalama ya usalama wa Tanzania ndiyo kinga ya mwisho ya uhuru wetu na wakati wowote ule idara hiyo inapokuwa katika shaka, shuku, kutokuaminika, wasiwasi, kudhaniwa, tuhuma, au madai hasi basi uhuru wetu uko matatani. <br />
<br />
Wengine wanafikiria uhuru wetu unalindwa na Jeshi la Wananchi au na Polisi, hawa ni watekelezaji wa kile ambacho usalama wa taifa umefanya. Pasipo usalama wa taifa kufanya kazi yake vizuri basi vyombo vya ulinzi vinajikuta vinafanya kazi ngumu zaidi ya kutulinda kwani kinga ya mwisho ya usalama wetu iko matatizoni. Bila ya idara yenye nguvu ya usalama wa taifa kazi ya ulinzi wa taifa inakuwa ngumu zaidi kuliko inavyopasa. <br />
<br />
Uhuru wa nchi yoyote duniani unaenda sambamba kabisa na uwezo wake katika mambo ya kijasusi. <br />
<br />
Ninapozungumzia Usalama wa Taifa ninazungumzia kundi la watu ambao kutokana na nafasi zao wamepewa jukumu la kukusanya, kuchambua, na kuamua juu ya hatua mbalimbali za kuchukuliwa juu ya taarifa za kijasusi ambazo zinatishia maslahi ya taifa letu. Ninazungumzia wale wenye jukumu la kuhakikisha kuwa mipango yoyote, njama yoyote, na mikakati yoyote ya watu wasiotutakia mema inagundulika mapema kabla haijatekelezwa na hatua za kujibu mashambulizi au kuadhibu zinachukuliwa mara moja. Ni watu ambao jukumu lao kubwa ni kutambua taarifa za kijasusi na kuchukua hatua mara moja za kuzuia kitu chochote, mtu yeyote au jambo lolote kuingilia uwepo wa Taifa letu huru, usalama wa watu wake, na usalama wa maslahi yake mahali popote duniani. <br />
<br />
Kati ya mambo ambayo yamo moyoni mwangu kwa muda mrefu sasa ni suala hili la usalama wa taifa. Ninapoangalia mambo kadha wa kadha yanayotokea nchini na ambayo yamekwisha tokea nimejifunza mambo fulani ambayo naamini ni muhimu kuwashirikisha ili tuweze kuelewa vita hii dhidi ya ufisadi kwa muda mrefu ujao haitakuwa na mafanikio bila ya kuboresha vyombo kadhaa na cha kwanza miongoni mwao ni Usalama wa Taifa (UwT). <br />
<br />
Nimeshaandika mara kadhaa huko nyuma nikiwa mtu wa kwanza kuvunja mwiko wa kuzungumzia usalama wa taifa hadharani na kwa kina, mwiko ambao ninaendelea nao katika sehemu hii ya kwanza ya mabadiliko ya lazima ya “Idara” kama Watanzania tunataka tusalimike. Ningekuwa na uwezo ningewaweka chini wana usalama wote na kuwapatia somo hili la bure ambalo ningedai ni la lazima kabla ya mtu yeyote kula kiapo cha utumishi! <br />
<br />
Kwanini mabadiliko ni lazima?<br />
<br />
Umuhimu wa kutaka kusababisha mabadiliko ndani ya idara hii nyeti ni mlolongo wa matukio ya kushangaza ambayo kimsingi kabisa yanatishia uhuru wetu kuliko utawala wa kikaburu au mvutano wa mataifa ya Magharibi na Mashariki wakati wa Vita Baridi. Matukio ambayo tunayaita ni “ufisadi” msingi wake na kutokea kwake kumekuja sababu ya kulegalega na kuyumbayumba kwa idara hii nyeti. <br />
<br />
Kinachonitisha zaidi ni kuwa hakuna mtu ambaye yuko tayari kuzungumzia mabadiliko haya na kuanza kuyataka yafanyike na hivyo kuendeleza woga wa kutojadili idara hii huku madhara yakiendelea kutokea. Ni sawa na kuogopa kuzungumza au kujadili walinzi wa jengo letu wakati tunaona tunashambuliwa wakati kuna watu wanalipwa kutulinda. <br />
<br />
Hivyo, kama kweli tunataka kuushinda ufisadi na kujenga taifa lenye kufuata kweli misingi ya sheria, utawala wa demokrasia na siasa safi hatuna budi kuboresha idara ya usalama wa taifa, kuiimarisha na kuweza kuijenga ili iweze kukabiliana na changamoto za dunia ya leo. Hivyo, kama kweli tunataka kusalimika huko mbeleni hatuna budi kuboresha idara hii ambayo kiukweli kabisa ni moyo wa taifa letu. <br />
<br />
Falsafa ya Usalama wa Taifa <br />
<br />
Tunaweza kuigawa historia ya falsafa inayoongoza idara yetu ya Usalama wa taifa katika sehemu kubwa tatu ambazo sitaziangalia kwa undani sana (nitawaachia wengine waje kufanya kazi hiyo). Kuna Kipindi cha 1961-1970, kipindi cha 1970-1985, na kipindi cha 1996-Sasa. Vipindi vyote hivi vimeakisi katika utendaji kazi wa idara hii na kwa namna fulani vinaingiliana. <br />
<br />
Kipindi cha 1961-1970 (Miaka ya majaribu- Trial Years)<br />
<br />
Wakati huu wa historia tulikuwa tunakabiliwa na changamoto kubwa kadhaa ambazo zilitishia uwepo wa taifa letu na uhuru wetu kwa ujumla. Kilikuwa ni kipindi kigumu zaidi kuongoza. Kwanza, ni kwa sababu nchi yetu ndio imepata uhuru wake na kuwa Jamhuri lakini ikiwa na wataalamu wachache na maafisa wachache wa Usalama wa Taifa ambao walikuwa wamesomea kazi hii. Kilichotegemewa zaidi wakati ule ni ile tunu ya “uzalendo” ambayo watendaji wa kwanza wa serikali yetu iliwaongoza kwani hakukuwa na kitu cha aibu kama kushindwa kulinda uhuru ambao taifa limeupata. <br />
<br />
Mapinduzi ya Zanzibar, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na Maasi ya Jeshi ya mwaka 1964 yalikuwa ni kilele cha udhaifu mkubwa na wakati huo huo somo kubwa zaidi la kuelewa jukumu la idara ya usalama wa taifa (wakati huo ikiwa kama chombo kilichojulikana kuwepo bila kuwa idara iliyojulikana dhahiri). Mambo hayo makubwa yalionesha uwepo wa haja ya kuwa na usalama wa taifa uliokomaa, kusambaa na kufanya kazi kwa nguvu zote:<br />
<br />
a. Kulinda serikali iliyo madarakani<br />
<br />
b. Kumlinda Rais na tishio lolote dhidi ya nafsi yake na ofisi yake<br />
<br />
c. Kulinda Nchi kutoka kwa maadui wa nje (hasa Utawala wa Kikaburu wa Afrika ya Kusini)<br />
<br />
Hivyo kipindi hiki kwa kweli kilikuwa na matukio ya kushtua na mengine yaliyotokana na uwoga mkubwa hasa baada ya Uasi wa Jeshi. Jambo hili siyo geni kwa nchi changa. Hata Marekani baada ya kupata uhuru wake kwa njia ya Mapinduzi dhidi ya Himaya ya Mwingereza viongozi wake walikuwa na jukumu kubwa sana la kuhakikisha kuwa wanaulinda uhuru huo kwa kuwa na watu wa usalama wa taifa waliokuwa na uwezo na nyenzo za kuilinda nchi yao. <br />
<br />
Kama Tanzania chini ya Mwalimu ilivyofanya makosa ya hapa na palekatika usalama wa taifa mwanzoni mwa jamhuri yetu ndivyo hata Marekani taifa lililoundwa kwa misingi ya usawa wa watu wote lilifanya makosa katika sehemu hiyo nyeti, makosa ambayo miaka karibu zaidi ya 200 baadaye Marekani ilifanya tena na kuligharimu taifa hilo lenye nguvu zaidi duniani matukio ya Septemba 11. Na baada ya hapo Wamarekani wakajikuta wanalazimika kuangalia tena sekta nzima ya ukusanyaji wa habari za kijasusi na suala la usalama wa taifa. <br />
<br />
Machafuko ya Rwanda na Burundi mwanzoni mwa miaka ya sitini, mauaji ya Lumumba n.k vyote vilimfanya Mwalimu na uongozi wetu wa awali kuwa na wasiwasi (nervous) na wakati mwingine woga usio na msingi (paranoid) kwa mtu yeyote ambaye alikuwa akionesha dalili ya kuipinga serikali au kuwa mkosoaji sana. Ni njia pia iliyofuatwa na Dr. Hastings Banda wa Malawi na baadhi ya viongozi wa mwanzo wa Afrika na hata sehemu nyingine duniani.<br />
<br />
Hivyo, kuangalia idara hii na kufanya mabadiliko siyo jambo la ajabu au mwiko. Hivyo, kipindi hicho cha mwanzo kilikuwa cha mafanikio makubwa lakini pia kikiwa na changamoto ambazo zimeandikwa katika kurasa zisizofutika za historia. Masuala ya kina Kambona, Hanga, kina Bibi Titi Mohammed, n.k yote yanahusiana moja kwa moja na mafanikio na mapungufu ya Idara hii. <br />
<br />
Ninaamini miaka ya mwanzo ya nchi yetu taifa letu lilikabiliwa na tishio la ndani zaidi kuliko ya nje na jukumu la kwanza la utawala uliokuwepo ni kuhakikishia kuwa Taifa letu halisambaratiki.<br />
<br />
Kipindi cha 1970-1985 – Miaka ya Utukufu (glory years)<br />
<br />
Kwa kipimo kikubwa ninaamini Usalama wetu wa taifa ulifanya kazi kubwa zaidi na ya kukumbukwa katika miaka hii 15. Ni miaka ambayo kwanza sheria tuliyoirithi kwa mkoloni ya “Official Secrets” ilifutwa na badala yake sheria ya Usalama wa Taifa ya Mwaka 1970 iliingizwa na kuongoza shughuli za usalama wa taifa.<br />
<br />
Tishio kubwa la wakati huu pamoja na matishio ya ndani (halisi au ya kudhaniwa) ni matukio nje ya Tanzania. Kuingia kwa Idi Amin madarakani nchini Uganda na kuendelea kwa majirani zetu kukaliwa na wakoloni kama huko Msumbiji na Zimbabwe na kuendelea kwa utawala wa kikaburu Afrika ya Kusini vilikuwa ni tishio kwa serikali zote za kusini mwa Afrika ambazo zilikuwa zimekwishapata uhuru wake. <br />
<br />
Uamuzi wa Tanzania kuongoza harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika na kukubali kutumiwa kwa ardhi yake na vikosi vya wapigania uhuru vililifanya taifa letu kuwa kama mnyama aliyewekwa alama na wawindaji, adui wa wakoloni, makaburu alikuwa wazi mbele yao. <br />
<br />
Ni kutokana na ukweli huo sheria hiyo ya mwaka 1970 iliingiza katika ibara ya 9 kutambua vikundi vya wapigania uhuru na kulinda maslahi yao. Hivyo katika miaka hiyo na chini ya sheria hiyo Usalama wa Taifa wa Tanzania ulikuwa unatumika siyo kulinda maslahi na usalama wa taifa letu tu bali pia kulinda maslahi na usalama wa vikundi vya wapigania uhuru ambavyo tumevitambua hivyo. Kwa misingi hiyo watu wetu wa usalama walikuwa pia wakiangalia usalama wa SWAPO, ANC, FRELIMO, n.k Hili halikuwa jambo dogo.<br />
<br />
Ni kutokana na hili mchango wa watu wetu wa Usalama wa Taifa wakati huo unatambulika hata leo katika baadhi ya nchi na unatambulika kwa shukrani. Ilikuwa ni miaka ya utukufu kwani ni pamoja na mchango wetu huo tuliweza kuchangia siyo damu tu kama wengi wanavyojua katika harakati za ukombozi lakini vile vile mchango wa taarifa na habari za kijasusi zilizowezesha vikundi vya wapigania uhuru kufanikisha malengo mbalimbali ambayo hatima yake kwa kiasi kikubwa ilikuwa ni kupatikana kwa utawala wa kidemokrasia na haki ya usawa kwa watu wote wa Afrika ya Kusini pale Nelson Mandela na wenzake walipofunguliwa kutoka katika shimo la giza la gereza la Kisiwa cha Robin walikotumikia jumla ya miaka ma-mia nyingi. <br />
<br />
Kipindi cha 1985-1996 – Miaka ya kukosa mwelekeo (Uncertainty Years)<br />
<br />
Mojawapo ya mabadiliko makubwa yalitokea baada ya baba wa taifa kung’atuka katika uongozi wa serikali (1985) na baadaye Uenyekiti wa CCM (1990). Kubadilika huku kwa uongozi kulikuwa pia na changamoto ya namna ya pekee kwa usalama wa Taifa. Miaka mitano ya mwanzo tunaye Rais mwingine ambaye kisheria ndio mkuu wa Usalama wa Taifa, lakini kisiasa nguvu zilikuwa kwa Mwenyekiti wa CCM ambaye katika mfumo wa chama kimoja alikuwa na nguvu ya aina ya pekee. <br />
<br />
Hivyo, utii (allegiance) ya watu wa usalama wa taifa kama ilivyokuwa kwa maeneo mengine ilikuwa ni ya kuchanganyikiwa kidogo; Kumtii Mwinyi ambaye alikuwa Rais au Nyerere ambaye alikuwa ni Mwenyekiti wa Chama? Je, Rais akifanya mambo fulani yaliyo ndani ya madaraka lakini yakagongana na mtazamo wa Mwenyekiti wa CCM watu wa chini wasimame na nani? <br />
<br />
Matokeo yake Usalama wa Taifa ulianza kugawanyika kwa kufuata mwelekeo wa itikadi; kizazi cha zamani kikiwa kinaongozwa na uzalendo wa aina ya pekee na dhana ya kulinda taifa kama miaka ile ya majaribu na utukufu lakini kizazi kipya cha wasomi zaidi kikianza kuona matundu ya mabadiliko ya kiuchumi aliyoyafungulia Mzee Mwinyi. <br />
<br />
Ni katika kipindi hiki tunaweza kuona kwa kiasi cha namna fulani kujipanga kwa vikundi ambavyo leo tunaweza kuviita vya kifisadi. Hili lilikuwa linaanza kuonekana zaidi miaka ile mitano ya utawala wa Rais Mwinyi. Katika kipindi hiki viongozi walianza kukaa kwa kujiamini zaidi na hasa baada ya Baba wa Taifa kuachia uenyekiti wa CCM vile vile na hivyo kumpa nguvu zote za kichama na kiserikali Rais Mwinyi.<br />
<br />
Matokeo yake ni kuvunjwa rasmi kwa azimio la Arusha, na kuruhusiwa kwa namna ya pekee vitendo vya kifisadi kuanzia uuzaji wa Loliondo na utoroshaji wa dhahabu. Kipindi hiki kwa baadhi ya watu kilikuwa ni cha neema kwani yeyote aliyetaka alipata endapo tu alicheza karata zake vizuri. <br />
<br />
Baada ya Afrika ya Kusini kupata utawala wa kidemokrasia na vyama vya ukombozi kutambulika kama vyama vya kisiasa na Tanzania kupunguziwa jukumu la kulinda maslahi ya vyama hivyo, watu wetu wakawa hawana tishio kubwa zaidi la kuangalia zaidi ya kuangalia usalama wa viongozi na serikali iliyoko madarakani na dola (state). <br />
<br />
Hii ilikuwa ni miaka ya kukosa mwelekeo kwa sababu adui yetu wakati huo alikuwa ni nani? Vita baridi vilikuwa vimekoma kwa kusambaratika kwa Shirikisho la Kisovieti la Urusi (USSR) na kuibuka kwa Marekani kama Taifa pekee lenye nguvu zaidi duniani; Afrika ya Kusini imerejea katika utawala wa demokrasia, na wimbi la mageuzi ya kisiasa lilikuwa linasambaa katika Afrika. Siyo wimbi la mapinduzi ya kijeshi bali mabadiliko ya kisiasa kwa njia za kidemokrasia. <br />
<br />
Je, watu wetu wa Usalama walikuwa wanalinda maslahi ya nani zaidi? Kwa wachache kilikuwa pia ni kipindi cha kuanza kushiriki katika vitendo vya kifisadi. Katika ripoti zinazokuja tutaangalia baadhi ya matukio ya wakati huu ambayo yalifungulia mlango wa ufisadi kuanzia Ikulu hadi nyumba ya mwisho kabisa karibu na shamba la kijiji!<br />
<br />
Kipindi cha 1996-Sasa – Miaka ya Aibu (Shameful Years)<br />
<br />
Sasa hivi tunaishi katika kipindi cha aibu. Kipindi ambacho nikisikia mtu anajiita mtu wa “usalama” nasikia kukereka (nilitaka nitumie neno jingine hapa!). Si kwamba ninawahukumu wote kuwa wameacha wito wao bali kuna kikundi kati yao ambacho kimeacha suala la usalama wa taifa na badala yake kimebakia kwenye “usalama wa wanasiasa”! Hiki siyo kitu kimoja.<br />
<br />
Kundi hili limegeuza “usalama wa taifa” na kuwa usalama wa “chama tawala” na hofu yangu ni kuwa wanatumia muda mwingi kufikiria Tanzania katika mwanga wa siasa za vyama na kusahau kuangalia Tanzania kama jamhuri. Wakati wowote usalama wa taifa unapoacha kuangalia taifa na kuhamisha macho yao kwenye vitu vingine, basi usalama huo wa taifa unakuwa umepotea na ni mabadiliko ya haraka na ya lazima ndiyo yanaweza kurejesha huko. <br />
<br />
Miaka hii ya aibu ilianza kwa kuundwa kwa Idara ya Usalama wa Taifa kwa sheria namba 15 ya Usalama wa Taifa ya 1996 iliyosainiwa na Rais Benjamin Mkapa Januari 20, 1997 kuwa sheria. <br />
<br />
Sheria hii ndiyo ilirasmisha uwepo wa idara ya usalama wa taifa na kuwatoa gizani watu waliokuwa wanajulikana uwepo wao lakini pasipo kuonekana. Iliweka msingi wa utendaji kazi wa idara hiyo, utaratibu wake hadi viapo vya wana usalama. Kwa juu juu sheria hii ukiangalia kwa haraka unaweza kufikiri ilikuwa ni nzuri. Kitu kizuri pekee ambacho naweza kusema kiko ndani ya sheria hii (zaidi ya vipengele vyake kadhaa) ni kujenga taasisi rasmi ya usalama wa taifa. <br />
<br />
Hata hivyo, mambo mengine yaliyomo katika sheria hiyo ni mambo ambayo mtu yeyote aliyesomea mambo ya ujasusi anaweza kujikuta anahuzunika kwani sheria hii imefungua mwanya wa ufisadi wa kimataifa na kuwafunga kwa minyororo watu wetu wa usalama. Ni sheria mbayo kama ningekuwa na uwezo ningeibadilisha siku ya kwanza Rais Kikwete anaingia madarakani.<br />
<br />
Ninaamini kwa moyo wangu wote kuwa sheria hii ilifikiriwa, kutungwa, na kubarikiwa na miungu ya mafisadi! Mtu mwenye akili timamu mwenye kulipenda taifa lake na kujali maslahi ya taifa lake asingeweza kuivumilia iwepo kwa zaidi ya saa moja! Ni sheria inayotishia usalama wetu wa taifa na natumaini kuna mtu ataamka na kutaka kuifanyia mabadiliko ya haraka kama tunataka tusalimike. <br />
<br />
Sheria hii kwa maoni yangu ni sawa na mtu ambaye ameamua kulinda mifugo yake, kajenga uzio mkubwa na kaweka lango kuu. Kaajiri na walinzi na kutoa maelekezo ya walinzi kuwa waangalifu. Tatizo ni kuwa baada ya kufanya haya yote, mtu huyo hakuweka lango la kuzuia watu kuingia na hivyo kuacha uzio ukiwa na uwazi huku yeye mwenye akijivunia kuwa amejenga “uzio” mkubwa sana! Anapoamka asubuhi anakuta nusu ya mifugo imetoweka na mlinzi akisimama upande mwingine wa jengo! <br />
<br />
Hatuwezi kwenda mbele kama taifa na hasa kukabiliana na changamoto zilizoko mbele yetu na hasa adui yetu mpya ambaye leo hii anatuchezea kama kucheza shere kwa sababu ya udhaifu wa sheria hii. Ni sheria ambayo wapiganaji wa CCM ningetamani wasema tunataka kuifanyia mabadiliko kwani ni mojawapo ya vitu vinavyotengeneza mfumo wa utawala wa kifisadi. <br />
<br />
Tutaingalia sheria hiyo ya TISS (Tanzania Intelligence and Security Service) katika sehemu ya pili ya hoja hii. Tutafanya hivyo baada ya kuangalia ni adui gani sasa hivi anayetishia uhuru wetu zaidi na kwanini ni adui wa hatari zaidi kuliko uvamizi wa Nduli au njama za Makaburu wa Afrika ya Kusini. <br />
<br />
Usikose sehemu ya pili.<br />
<br />
Niandikie: mwanakijiji@mwanakijiji.comKyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-44402760502400367212009-11-27T11:54:00.000+03:002009-11-27T11:54:04.927+03:00Ziwa Ngozi linalodaiwa kuhamishwa kwa jiwe la motoNa Thobias Mwanakatwe <br />
<br />
Tanzania ni nchi iliyobahatika kuwa na maziwa mengi hata hivyo kila ziwa lina historia yake jinsi lilivyojitokeza kwa maana ya chanzo chake. <br />
<br />
Ziwa Ngozi lililoko Rungwe ni moja ya maziwa ambayo wenyeji huogopa kulitembelea kutokana na imani walizonazo. Mwandishi Wetu, Thobias Mwanakatwe, anaandika zaidi. <br />
<br />
Yapo maziwa au maeneo ambayo ukianza kusimuliwa historia yake unaweza kabisa ukakata tamaa hata kulitembelea hasa kutokana na maajabu yaliyopo katika ziwa hilo. <br />
<br />
Mojawapo ya maeneo yenye historia ya maajabu ni ziwa Ngozi lililopo katika kijiji cha Mbeye One wilayani Rungwe katika mkoa wa Mbeya. <br />
<br />
``Mimi sijawahi kufika huko lakini siwezi kwenda kule kunatisha,`` anasema Uswege Mwakimbete alipoulizwa kama amewahi kufika kwenye ziwa hilo. <br />
<br />
Ziwa hilo liko urefu wa mita 150 kutoka kilele cha milima inayozunguka ziwa , ambapo kutoka usawa wa maji kina cha maji ni urefu wa mita 73 na ukubwa wa eneo lenye maji ni kilomita sita hadi 10 za mraba na lina ukubwa wa kilometa za mraba 3.75. <br />
<br />
Wataalam wanaeleza kuwa ziwa hilo limetokana na volkano , limezungukwa na misitu mizuri ya asili ya kitropiki hali nzuri ya hewa na tulivu. <br />
<br />
Ili kulifikia ziwa hilo unalazimika kutembea kwa mwendo wa kati ya dakika 45 na saa 1 kutoka kijijini Mbeye One ambacho kipo barabara kuu ya Mbeya-Kyela. <br />
<br />
Pia kutoka katika kilele cha milima inayozunguka ziwa hilo unalazimika kushuka kwa zaidi ya dakika 45 huku ukilazimika kushuka kwa kutumia mizizi migumu ya miti ya asili iliyopo katika msitu mnene kwasababu ya mteremko mkali kuelekea katika ziwa hilo. <br />
<br />
Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbeye One, Watson Mwakalinga anasema kuwa ziwa hilo liligunduliwa mwaka 1925 ambapo anasema kuwa ziwa hilo lilihama kutoka katika kijiji cha Mwakaleli wilayani humo baada ya kudaiwa kuwa baada ya kuchomwa na jiwe la moto na wakazi wa kijiji hicho. <br />
<br />
Anasema ziwa hilo la maajabu lilichomwa moto na wakazi wa kijiji cha Mwakaleli kwasababu lilikuwa likileta mikosi mingi kijijini hapo ikiwemo watu kufa kila mara hali iliyowalazimu wazee wa kijiji hicho kufanya uchunguzi na kubaini kuwa kunasababishwa na ziwa hilo la Ngozi. <br />
<br />
Hata hivyo unapowauliza wataalam wa masuala ya mazingira wanasema kisayansi ziwa haliwezi kuhama. <br />
<br />
``Kwa vile ziwa hili halikuwepo pengine wangesema kuwa halikuwepo mpaka volkano hiyo ilipokuwepo lakini ziwa haliwezi kuhama,`` anasema Prof .William Rugumamu , wa Idara ya Jiografia toka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. <br />
<br />
Mwakalinga anasema kuwa maajaabu ambayo yametokana na imani za kishirikina yanayodaiwa kuwepo katika ziwa hilo ni pamoja na watu wanaofika huku kudaiwa kupotea, sauti za vikohozi vya watu wasioonekana pamoja na miujiza ya watu wanaotwanga mahindi lakini hawaonekani. <br />
<br />
Anasema mbali ya maajabu mengine ya imani za kishirikina yaliyokuwepo, anasema kuwa ziwa hilo linatabia ya kubadilika rangi ambapo anasema ziwa hilo limekuwa likigeuka rangi mara kwa mara na kuwa na rangi za kijani, bluu, nyeusi na nyeupe. <br />
<br />
Anasema kubadilika kwa maji katika ziwa hilo kimsingi wananchi wameshindwa kufahamu kunatokana na nini ingawa waatalam waliowahi kufika kijijini hapo wanadai kunatokana na mabadiliko ya hali ya hewa ya eneo hilo. <br />
<br />
Prof. Rugumamu anasema hali ya kubadilika rangi kwenye ziwa Ngozi siyo kitu cha ajabu kwani ni hali inajitokeza kwenye maji ya bahari ambapo anasema wakati mwingine huweza kuonekana rangi ya bluu au rangi ya upinde kutegemeana na hali ya jua. <br />
<br />
`Kwenye maji ya bahari hali ya maji kubadilika ni jambo la kawaida pengine watu hawawi makini kuangalia tu,`` anasema Prof. Rugumamu ambaye ni mtaalam wa masuala ya mazingira na hali ya udongo. <br />
<br />
Hata hivyo unapofika eneo hilo misitu inayozunguka ziwa hilo ina hali nzuri pamoja na baadhi ya wanyama wakiwemo chui na nyani, ingawa ni nadra sana kuwaona chui katika misitu hiyo kwa kuwa wanajificha na hawajawahi kuleta madhara kwa binadamu. <br />
<br />
Anasema kutokana na maajabu hayo, wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakiogopa kabisa kufika katika ziwa hilo kutokana na maajabu hayo yaliyokuwa yakisemwa. <br />
<br />
Mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Mbeye 1, George Mbepe (65), anasema awali walikuwa wanahofia kufika katika ziwa hilo kutokana na madai ya kuwapo kwa imani za kishirikina. <br />
<br />
``Kulikuwa na imani kuwa mtu akija huku atasikia vikohozi vya watu wasioonekana huku wengine wakitwanga mahindi, lakini hawaonekani,`` alisema na kuongeza kuwa imani hizo zilisababisha watu wasifikirie kwenda katika ziwa hilo . <br />
<br />
Hata hivyo anasema, kuwa kutokana na maji hayo kuonekana yanafaa, yamekuwa yakitumiwa kama mradi na vijana ambao wamekuwa wakiuza kati ya shilingi 300 na 500 kwa lita. <br />
<br />
Wakazi wa Kijiji hicho, wanaamini maji ya ziwa hilo hutumika kama dawa kwa ajili ya kutibu watoto ambao wamekuwa wakistuka nyakati za usiku na kwamba pindi wanaponywesha maji hayo hali hiyo inakoma mara moja. <br />
<br />
Prof .Rugumamu anasema kuwa hakuna maelezo yoyote ya kisayansi ya Ngozi kuwa na uwezo wa kuponya magonjwa lakini anasema wenyeji kwenye maji mengi yanayotokana na volkano wamekuwa na imani za aina hiyo. <br />
<br />
``Hata sehemu nyingi ambako yanatoka maji moto yanayotokana na volkano watu wanaamini hiyo lakini hiyo ni imani tu, anasema .`` <br />
<br />
Ziwa hilo liliwahi kupandikizwa samaki aina ya perege mwaka 2001, hata hivyo hadi sasa hawajafanikiwa kuvua samaki hata mmoja kutokana na ukosefu wa vifaa vya uvuvi pamoja na ugumu wa kufika katika ziwa hilo . <br />
<br />
Hata hivyo imani hizo za kishirikina za wakazi wa Kijiji hicho zilifikia tamati mwanzoni mwa mwaka huu baada ya timu ya watafiti wa Kimataifa kutoka nchi za Ufaransa, Uingereza na Ubelgiji kufanikiwa kufika katika ziwa hilo na kufanikiwa kuingia ndani ya ziwa hilo na kuchota udongo kwa ajili ya kufanya utafiti wa kisayansi kuhusiana na ziwa hilo pamoja na mazingira yanayolizunguka. <br />
<br />
Watafiti hao walibaini kuwa ziwa hilo lina umri wa zaidi ya miaka 40,000.Ingawaje wataalam wengine wanasema kuwa ziwa hilo linaweza kuwa lilikuwepo hata miaka milioni 2 iliyopita. <br />
<br />
Kuna baadhi ya watalii wamekuwa wakitembelea ziwa hilo ambapo hulipia kiasi cha Sh 2,000 kwenda kuliona . <br />
<br />
Hata hivyo baadhi ya wananchi wanasema kuwa kiasi kinachotozwa cha sh.2,000 hakitoshi bali wangetozwa zaidi. <br />
<br />
``Watalii walitakiwa kutozwa shilingi 10,000 na watanzania walipe shilingi 2,000 ili mapato yatokanayo na shughuli za utalii yaweze kutumika kwa shughuli za maendeleo katika Kijiji na wilaya,`` anasema Jackson Mwakabuta,mkazi wa kijiji hicho. <br />
<br />
Mwakabuta anasema kuwa idadi ya watalii wanaotembelea vivutio vya utalii wilayani humo haitoshelezi, ambapo alisema kuwa kuna haja ya kufanyika kwa juhudi za makusudi kutangaza vivutio vilivyopo nchini pamoja na kuwahamasisha Watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii badala ya kuwategemea wageni tu. <br />
<br />
Mbali ya ziwa hilo kukosa watalii wanaotembelea kuangalia vivutio vilivyopo, pia wakazi wa Kijiji cha Mbeye One, wameshindwa kuendesha shughuli za uvuvi kutoka katika ziwa hilo kutokana na ukosefu wa vifaa vya uvuvi pamoja na ugumu wa kufika katika ziwa hilo la shimo ambalo limezungukwa na milima. <br />
<br />
Wananchi hao wanaiomba serikali iwasaidia kupata boti itakayotumika kwa shughuli za uvuvi katika ziwa hilo, ambapo alisema kuwa kuanza kwa shughuli za uvuvi kutasaidia kukuza uchumi wa kijiji hicho na hivyo kuinua maisha ya wananchi . <br />
<br />
Mwambata wa Ubalozi wa Ufaransa nchini, Dk. Raymond Latest ambaye alikuwa pamoja na timu ya utafiti wa ziwa hilo anasema kuwa wilaya ya Rungwe ina vivutio vizuri vya utalii kuliko mkoa wa Arusha lakini havifahamiki kutokana kwa kutotangazwa. <br />
<br />
Anasema awali kabla hajafika nchini, alikuwa akiifahamu zaidi nchi ya Kenya ambayo imekuwa ikijitangaza zaidi kwenye utalii, lakini alipofika nchini akagundua kuwa Tanzania ina vivutio vingi vya utalii ikiwamo misitu ya asili kuliko nchi yoyote ya Afrika Mashariki. <br />
<br />
Dk.Latest anasema vivutio hivyo vikitangazwa vizuri vitaweza kuchangia kukuza pato la Taifa kupitia sekta ya Utalii. <br />
<br />
Akilizungumzia ziwa Ngozi, Dk. Latest alisema kuwa amevutiwa na ziwa hilo lililozungukwa na milima na kuonekana lipo shimoni pamoja na kuzungukwa na misitu ya asili, ambapo alisema kuwa atahakikisha anaitangaza wilaya ya Rungwe ili iweze kufikiwa na watalii wengi kutoka nchini Ufaransa na watalii waweze kujionea maajabu ya wilaya hiyo. <br />
<br />
Kiongozi wa timu ya watafiti, Dk. David Williamson kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam anasema hiyo ilikuwa mara yao ya kwanza kufika katika ziwa hilo kwa lengo la kufanya utafiti ili kujua umri wa ziwa hilo, mabadiliko ya hali hewa na mazingira pamoja na kufahamu volkano ndogo ya mwisho ililipuka lini. Na kama maji ya ziwa hilo yanafaa kwa matumizi ya binadamu. <br />
<br />
Dk. Williamson anasema kuwa ziwa ngozi ni moja kati ya maziwa 10 ya volkano yaliyopo wilayani Rungwe ambayo wanafanyia utafiti wa kisayansi, aliyataja maziwa mengine kuwa ni pamoja na Ndwati, Kisiba, Chungululu, Ikapu, Itamba, Asoko, Ilamba, Kingili, Katubwi na Itende. <br />
<br />
Utafiti wao unajumuisha uchukuaji wa vumbi na tope lililopo chini ya ziwa hilo vitu ambavyo vitasaidia katika utafiti wao. <br />
<br />
Katika utafiti wao wa awali waligundua kuwa kina cha maji katika ziwa hilo kinazidi kupungua kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, mmonyoko wa udongo na kwamba hali hiyo inahatarisha uwepo wa ziwa hilo kwa miaka ijayo. <br />
<br />
Akieleza sababu za kuchukua tope lililochini ya ziwa hilo , alisema kuwa wanaamini kuwa tope lililoganda ndani ya maji linakuwa na mkusanyiko wa tabaka mbalimbali za taka, udongo na kwamba kiasi wanachochukuwa kitawawezesha kujua mambo muhimu wanayoyahitaji katika utafiti wao. <br />
<br />
Mtafiti mwingine kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,Edister Abdallah anasema kuwa utafiti huo utasaidia wakazi wanaosihi kuzunguka ziwa hilo kuendana na mabadiliko ya hali ya hewa hivyo kushiriki katika kuhifadhi mazingira ya eneo hilo na wilaya ya Rungwe na hivyo kufanya uwepo wa ziwa hilo kuwa endelevu. <br />
<br />
Anasema kuwa juhudi za dhati zinapaswa kuchukuliwa ili kuwajengea wananchi utamaduni wa kutunza mazingira tofauti na ilivyo sasa ambapo wananchi hawaoni wajibu wao wa kushiriki katika kutunza na kuhifadhi mazingira ambayo ni muhimu katika maisha ya mwanadamu na viumbe hai. <br />
<br />
Alisema kuwa wananchi wakipatiwa elimu na kujua umuhimu wa kuhifadhi mazingira kila mmoja atatimiza wajibu wake kwa kutunza mazingira. <br />
<br />
Anaongeza kuwa ukosefu wa elimu umekuwa ukisababisha wananchi wengi washiriki katika uharibifu wa mazingira bila wao kujua au wengine kuharibu kwa makusudi bila kujua athari za baadaye za uharibifu huo. <br />
<br />
Naye Mshauri wa Sekta ya Wanyamapori mkoa, Stanley Munisi anasema mkoa wa Mbeya unao vivutio vingi vya kitaalam, lakini vingi bado havijatangazwa na kwamba hivyo ipo mikakati ya kuanza kuzitangaza.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-17876890420707062562009-11-27T11:10:00.000+03:002009-11-27T11:10:26.867+03:00Vivutio vya Mbeya vina nafasi kubwa kukuza uchumi<div style="text-align: center;">Na Mwadishi Wetu<br />
</div><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw-IpI1HngI/AAAAAAAAAH4/5GBL-7_TJWw/s1600/Malamba_falls-_Suma.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw-IpI1HngI/AAAAAAAAAH4/5GBL-7_TJWw/s320/Malamba_falls-_Suma.JPG" yr="true" /></a><br />
</div><br />
<div style="text-align: center;"><span style="font-size: x-small;">Mh. Profesa Mark Mwandosya akitembelea maporomoko ya Malamba wilayani Rungwe ambayo ni mojawapo ya vivutio kibao vya utalii mkoani Mbeya. </span><br />
</div><br />
JIJI la Mbeya lina vitongoji vingi vyenye utajiri. Lina vivutio vingi kwa wageni waliopata fursa ya kulitembelea. Mbeya ina safu za milima iliyosheheni rasilimali za urithi tangu zama za kale. Rasilimali hizo ni pamoja na misitu mikubwa iliyo hifadhi wanyama na ndege wazuri wa kuvutia. <br />
<br />
Mbeya ni Mkoa ulioandika historia ya maajabu katika bara la Afrika na ulimwenguni, tangu kilipodondoka kimondo. Kimondo hicho kilidondoka katika Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.Vivutio vingine vinavyoipamba Mbeya ni mabwawa yenye matukio ya maajabu, kwa mfano bwawa lililopo Masoko, jirani na kilele cha Mlima Rungwe. <br />
<br />
Pia, Ziwa Ngozi na Daraja la Mungu ni baadhi ya vivutio vinavyotengeneza historia ya pekee ya Mbeya na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Ziwa Nyasa ni kivutio kingine, ambapo watu kutoka mataifa mbalimbali hufika kujionea ziwa hilo lenye hadhi kubwa katika bara la Afrika. <br />
<br />
Wageni mbalimbali hufika wilayani Kyela kujionea mandhari ya ziwa hilo, ambalo ni la tatu kwa ukubwa barani Afrika. Ziwa hilo pia lipo katika nchi tatu za Malawi, Msumbiji na Tanzania. Wananchi wa nchi hizo na wageni wengine, hunufaika na Ziwa Nyasa kwa uvuvi wa samaki na viumbe wengine waishio majini, kwa ajili ya chakula na biashara. <br />
<br />
Ziwa hilo pia limerahisisha usafiri kati ya bandari za Mbamba Bay na Itungi. Lakini, jambo kubwa la kujivunia katika Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ni kuwapo kwa pango la Matema na Hoteli ya Matema. Hoteli hiyo ya ufukweni imeboresha mazingira ya ufukwe wa Matema na kuufanya kuwa sehemu ya kuvutia kwa wageni wanaofika hapo. <br />
<br />
Matema ni eneo tulivu, lenye mandhari mwanana na mimea ya rangi ya kijani kibichi, iliyopambwa na safu za milima. Milima hiyo imesheheni misitu, inayopatikana ndege wazuri wa angani. Wageni wanaotembelea hotelini hapo, huvutiwa na mandhari hiyo. Hoteli ya Matema ipo katika mwambao wa Ziwa Nyasa. Eneo hilo lilikuwa pori, lakini sasa limegeuka kuwa lulu kwa watu wa makabila tofauti ya ndani na nje ya nchi. <br />
<br />
Eneo hilo limejaa utulivu na lina sauti za ndege. Baadhi ya wageni waliowahi kutembelea eneo hilo, wanadiriki kulifananisha na bustani ya Edeni. Kanisa la Uinjilisti lenye makao yake makuu Mbalizi, Mbeya Vijijini, ndicho chanzo cha kuwapo kwa hoteli hiyo, maarufu kama Matema Lake Shore Resort. <br />
<br />
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kanisa hilo, Mchungaji Marcus Lrhner, anasema kuwa Kanisa la Uinjilisti lilifanya utafiti na kugundua kuwa eneo hilo linafaa kuweka vivutio na vivutio hivyo vinaweza kukuza sekta ya utalii nchini. Anasema kumekuwa na mafanikio kutokana na kuwapo kwa kivutio hicho. <br />
<br />
Mafanikio hayo yanatokana na juhudi za kanisa hilo, kwa kupitia wafadhili wake, ambao kwa miaka nane sasa wamekuwa wakijitahidi kutunza mazingira. Mchungaji Lehner anasema kwamba utafiti uliofanywa pia ulizingatia kuwapo kwa eneo zuri la kuogelea, lenye mchanga safi na mzuri. Anasema Lake Shore Resort inatoa huduma za kulala na chakula cha asili, kinachoandaliwa kwa muda maalumu (kwa oda). <br />
<br />
Pia, ina nyumba mbalimbali zenye jumla ya vyumba 22, ikiwamo vyumba vya kujihudumia (self contained) na vyumba vya vitanda viwili hadi vitano. Zipo pia nyumba za ghorofa, zinazomwezesha mgeni kutazama vizuri ziwa, lilivyo na umbo lake, kabla ya kutumia usafiri wa boti, wa miguu au gari. Huduma hizo pia hupatikana hapo. <br />
<br />
Matema ipo katika eneo la Kaskazini, mwishoni mwa Ziwa Nyasa, ndani ya Wilaya ya Kyela. Ziwa lina upana wa wastani kilomita 60 na urefu wastani kilomita 550. Lipo kwenye Bonde la Ufa katika Afrika Mashariki na lina ujazo wa mita 500 kutoka usawa wa bahari. Ufukwe wa Matema unapambwa na safu za mlima Livingstone, wenye urefu wa mita 3,000.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-26729424786544757172009-11-27T10:48:00.000+03:002009-11-27T10:48:43.670+03:00Tutaboreshaje elimu katika shule za serikali?BY BENJAMIN NKONYA <br />
<br />
<br />
Chimbuko la maendeleo ya elimu nchini ni matokeo ya michakato ya sheria, falsafa na sera zilizoanzishwa katika vipindi mbalimbali kabla na baada ya uhuru. Baada tu ya kupatikana uhuru mwaka 1961, serikali ilitunga sheria ya elimu namba 83 ya mwaka 1962 iliyofuta sheria ya elimu ya mwaka 1927 ambayo iliruhusu utoaji wa elimu na mafunzo kwa mfumo wa ubaguzi wa rangi, dini na makabila.<br />
<br />
Katika sheria hii, serikali iliekeza mitaala, uongozi na ugharamiaji wa elimu na mafunzo ufuate usawa. Azimio la Arusha la mwaka 1967 lilianzisha falsafa ya elimu ya kujitegemea ambayo ilisababisha mabadiliko makubwa katika sera za jumla za kijamii na kiuchumi. <br />
<br />
Falsafa hii, ambayo iliasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ndiyo inaweka dira katika mfumo wetu wa elimu hadi leo, inaweka mkazo katika kuondoa matabaka kwenye utoaji wa elimu, utengano (alienation) kati ya shule na jamii na kusaidia kuondoa kasumba ya wasomi ya kujibagua na kutumia elimu waliyoipata kwa manufaa yao binafsi. <br />
<br />
Aidha falsafa hii inaelekeza katika kuunganisha nadharia na vitendo, kwa dhana kuwa elimu isipatikane vitabuni tu bali ijumuishe na ile ipatikanayo kutokana na uzoefu wa kutenda au kufanya kazi ya kuongeza tija. <br />
<br />
Ili kuhakikisha kwamba haya yanafikiwa na pia kuhakikisha kwamba wanafunzi wanawajibika na upatikanaji wa mahitaji yao, falsafa hii inaelekeza shule kuwa vituo vya kuzalisha mali ili kuchangia gharama za uendeshaji kwa asilimia ishirini na tano. Pia elimu inayotolewa katika ngazi zote iwe na maarifa na stadi za kumwezesha mhitimu kuishi na kufanya kazi yenye manufaa katika jamii.<br />
<br />
Katika kutekeleza falsafa hii, shule karibu zote zilitaifishwa na kuendeshwa na serikali kuanzia mwaka 1967. Ili kuondoa aina zote za ubaguzi, serikali ilikubali kugharamia elimu katika ngazi zote. Pamoja na hayo, kila shule ilianzisha mashamba ambayo yalikuwa maarufu kama mashamba ya elimu ya kujitegemea. Hali hii ilimfanya mwanafunzi wa Kitanzania kuwa tayari kujitegemea mara tu baada ya kuhitimu mafunzo ya elimu ya msingi. Kwa hakika falsafa hii ilishabikiwa sana na kila Mtanzania.<br />
<br />
Pamoja na uzuri wa falsafa hii, kuna changamoto zilizoukabili mfumo mzima wa elimu katika miaka kumi ya utekelezaji wa falsafa hii. Kama wote tunavyofahamu, katika nusu ya pili ya miaka ya 1970, ubora wa elimu yetu ulishuka sana kiasi kwamba serikali iliruhusu walimu wasio na sifa kuanza kufundisha katika shule za msingi. <br />
<br />
Changamoto hii iliambatana na ukosefu wa zana za kufundishia na kujifunzia kama vitabu, maabara, maktaba n.k. Sambamba na changamoto hii, ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi halikuenda sambamba na ongezeko la idadi ya vyumba vya madarasa na samani zake, achlia mbali nyumba za waalimu. <br />
<br />
Hivyo ililazimu chumba kimoja cha darasa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi kuliko idadi inayomfanya mwalimu alimudu darasa kiufundishaji. Pamoja na changamoto hizo, hata suala la usimamizi wa elimu nalo lilikuwa gumu kutokana na shule kuwa nyingi katika mtawanyiko wa kijiografia ambao una ufanisi mdogo. Matokeo ya hali hii ilikuwa ni kushuka kwa elimu kwa haraka sana.<br />
<br />
Serikali iling’amua changamoto hizi na kutafuta namna ya kuziondoa ili elimu iendelee kutolewa kwa ubora unaotegemewa. Mwaka 1978 Bunge lilitunga sheria mpya ya elimu namba 25 ambayo, pamoja na mambo mengine, iliruhusu watu binafsi, mashirika ya dini, asasi za kiraia na makampuni kuanzisha, kusajili na kuendesha shule. <br />
<br />
Kuanzishwa kwa sheria hii kulianza kuonyesha matumaini ya kunusuru ubora wa elimu kwani shule nyingi binafsi zilionyesha mafanikio. Kuna changamoto kadhaa ambazo zilijitokeza katika miaka kumi na tano ya kwanza ya utekelezaji wa sheria hii. <br />
<br />
Changamoto hizi zilirekebishwa kupitia sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 1995. Hivyo mfumo wetu wa sasa wa utoaji wa elimu na mafunzo nchini unaongozwa na sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 1995 (iliyopata nguvu kutokana na marekebisho ya sheria ya elimu Na. 25 ya mwaka 1978 iliyorekebishwa kwa sheria Na. 10 ya mwaka 1995), sera ya elimu ya ufundi ya mwaka 1996 na sera ya elimu ya juu ya mwaka 1999.<br />
<br />
Pamoja na ukweli kwamba shule za serikali zinaendeshwa kwa kodi za Watanzania pamoja na ufadhili mwingi sana kutoka mashirika mbalimbali ya ndani nje ya nchi, elimu yetu, hasa inayotolewa na shule za serikali, bado ina changamoto nyingi sana katika viashiria vya utoaji (input), mchakato (process) na matokeo (outputs).<br />
<br />
Baada ya marekebisho hayo na baada ya sekta binafsi kujiimarisha ipasavyo, Watanzania wameendelea kushuhudia kukua kwa haraka sana kwa elimu katika sekta binafsi licha ya ukweli kwamba shule hizi hazina ruzuku yoyote kutoka serikalini. Sasa ni zaidi ya miaka thelathini tangu kuruhusiwa kwa sekta binafsi kuingia katika utoaji wa elimu. <br />
<br />
Pengine ingekuwa busara kudurusu sababu hasa za tofauti hizi na kutafuta namna ambavyo elimu yetu katika sekta ya umma inaweza kuboreshwa.<br />
<br />
Ni ukweli usionpingika kwamba gharama za uendeshaji katika shule za serikali ni kubwa kuliko gharama katikashule binafsi. Hii inatokana na ukweli wa kiuchumi kwamba kadri mradi unavyozidi kuwa mkubwa ndivyo ufanisi kwa kila shilingi inayotumika unavyozidi kushuka. Hali hii inakabili vilivyo shule zetu za serikali. <br />
<br />
Moja ya viashiria vya kushuka kwa ufanisi ni hii hali ya waalimu kuwa na malalamiko yasiyoisha kuhusu mapunjo wanayopata katika malipo yao, baadhi ya wanafunzi kuvuka madarasa na vidato bila kujua kusoma na kuandika, kukosekana kwa maabara, maktaba, vitabu na vifaa vingine vya kujifunzia na kufundishia na mambo mengine yanayofanana na hayo.<br />
<br />
Sababu nyingine za kudorora kwa elimu katika shule za serikali ni kuingiliwa kupita kiasi na wanasiasa. Utakuta taarifa ya wakaguzi inaonyesha kabisa kwamba shule fulani haitakiwi kusajiliwa kutokana na kutotimiza baadhi ya vigezo vya usajili. Pamoja na taarifa hizo, utakuta mwanasiasa anaingilia kati na kulazimisha shule hiyo isajiliwe. <br />
<br />
Hivyo hata uendeshaji wake huenda kisiasa siasa tu bila kujali vigezo muhimu vya uendeshaji wa shule. Utakuta shule ya serikali imesajiliwa lakini haina hata kitabu kimoja wala maabara. Itakuwa ni ajabu isiyo kifani kukuta shule kama hii ikitoa elimu bora.<br />
<br />
Hali ni tofauti kabisa katika shule binafsi. Shule hizi husimamiwa na kwa ukaribu sana. Shule hizi hukaguliwa na kusajiliwa baada ya kutimiza vigezo vyote vya usajili. Huwezi kukuta shule binafsi inasajiliwa wakati haina maktaba yenye vitabu au maabara zenye vifaa vyote. Hata baada ya usajili, wakaguzi hufika katika shule hizi mara kwa mara kuangalia kama kila kigezo cha utoaji wa elimu kinazingatiwa. <br />
<br />
Sambamba na hili, utakuta mmiliki wa shule hizi anafuatilia kwa karibu sana kila kinachoendelea shuleni na kuhakikisha wanafunzi wake wanapata huduma zinazotakiwa. <br />
<br />
Kwaujumla wake ni kwamba shule binafsi huendeshwa kwa kufuata mahitaji ya wateja wake na kutimiza masharti yote yanayowekwa na serikali.<br />
<br />
Kurunzi haioni kama itatosha tu kukosoa bila kutoa mapendekezo ya ubereshaji. Njia ya kwanza ni kuondoa siasa katika uendeshajiwa usajili na uendeshaji wa shule. <br />
<br />
Hii inaweza kufikiwa kwa njia ya kuifanya idara ya ukaguzi kuwa wakala inayojitegema badala ya hali iliyopo ya kuwa idara katika Wizara Elimu na Mafunzo ya Ufundi. <br />
<br />
Itakuwa ni ajabu ya ngariba kujitia suna mwenyewe kama kitengo hiki kitatenda haki hasa wakati shule ya serikali inapofanya makosa. <br />
<br />
Njia ya pili ni kuweka ushirikiano kati ya wamiliki wa shule binafsi na serikali ili kuondoa tatizo la kushuka kwa ufanisi wa usimamizi unaotokana na kukua kwa idadi ya shule zinazosimamiwa na mmiliki mmoja. <br />
<br />
Katika hali hii, mmiliki wa shule binafsi anaweza kuwekwa kuwa meneja wa shule ya serikali (hasa hizi za kata) iliyo karibu naye. Kama meneja, atahakikisha kwamba anashirikiana na bodi ya shule katika kuhakikisha kwamba shule hii ya kata inatoa elimu bora kama ilivyo shule yake.<br />
<br />
Elimu ni mali ya umma na inatakiwa kugharamiwa na umma hata kama inatolewa na shule/chuo binafsi. Kurunzi inaamini kabisa kwamba, tukilizingatia hili, tutakuwa tumekata kabisa mizizi yote ya ufisadi dagaa, papa na nyangumi na tutakuwa tumeenzi na kuhuisha fikra sahihi za Baba yetu wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-35673228785218244312009-11-26T11:11:00.000+03:002009-11-26T11:11:20.729+03:00Vivutio vya Mbeya vina nafasi kubwa kukuza uchumi<div style="text-align: center;">Na Mwadishi Wetu<br />
</div><br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw43puPvCOI/AAAAAAAAAHw/QvgXh-gZYRI/s1600/d1.BMP" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw43puPvCOI/AAAAAAAAAHw/QvgXh-gZYRI/s320/d1.BMP" yr="true" /></a><br />
</div><div style="text-align: center;"><span style="font-size: xx-small;">Daraja la Mungu lililopo Wilayani Rungwe<br />
</span><br />
</div><br />
JIJI la Mbeya lina vitongoji vingi vyenye utajiri. Lina vivutio vingi kwa wageni waliopata fursa ya kulitembelea. Mbeya ina safu za milima iliyosheheni rasilimali za urithi tangu zama za kale. Rasilimali hizo ni pamoja na misitu mikubwa iliyo hifadhi wanyama na ndege wazuri wa kuvutia. <br />
<br />
Mbeya ni Mkoa ulioandika historia ya maajabu katika bara la Afrika na ulimwenguni, tangu kilipodondoka kimondo. Kimondo hicho kilidondoka katika Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya.Vivutio vingine vinavyoipamba Mbeya ni mabwawa yenye matukio ya maajabu, kwa mfano bwawa lililopo Masoko, jirani na kilele cha Mlima Rungwe. <br />
<br />
Pia, Kisiwa Ngozi na Daraja la Mungu ni baadhi ya vivutio vinavyotengeneza historia ya pekee ya Mbeya na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Ziwa Nyasa ni kivutio kingine, ambapo watu kutoka mataifa mbalimbali hufika kujionea ziwa hilo lenye hadhi kubwa katika bara la Afrika. <br />
<br />
Wageni mbalimbali hufika wilayani Kyela kujionea mandhari ya ziwa hilo, ambalo ni la tatu kwa ukubwa barani Afrika. Ziwa hilo pia lipo katika nchi tatu za Malawi, Msumbiji na Tanzania. Wananchi wa nchi hizo na wageni wengine, hunufaika na Ziwa Nyasa kwa uvuvi wa samaki na viumbe wengine waishio majini, kwa ajili ya chakula na biashara. <br />
<br />
Ziwa hilo pia limerahisisha usafiri kati ya bandari za Mbamba Bay na Itungi. Lakini, jambo kubwa la kujivunia katika Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ni kuwapo kwa pango la Matema na Hoteli ya Matema. Hoteli hiyo ya ufukweni imeboresha mazingira ya ufukwe wa Matema na kuufanya kuwa sehemu ya kuvutia kwa wageni wanaofika hapo. <br />
<br />
Matema ni eneo tulivu, lenye mandhari mwanana na mimea ya rangi ya kijani kibichi, iliyopambwa na safu za milima. Milima hiyo imesheheni misitu, inayopatikana ndege wazuri wa angani. Wageni wanaotembelea hotelini hapo, huvutiwa na mandhari hiyo. Hoteli ya Matema ipo katika mwambao wa Ziwa Nyasa. Eneo hilo lilikuwa pori, lakini sasa limegeuka kuwa lulu kwa watu wa makabila tofauti ya ndani na nje ya nchi. <br />
<br />
Eneo hilo limejaa utulivu na lina sauti za ndege. Baadhi ya wageni waliowahi kutembelea eneo hilo, wanadiriki kulifananisha na bustani ya Edeni. Kanisa la Uinjilisti lenye makao yake makuu Mbalizi, Mbeya Vijijini, ndicho chanzo cha kuwapo kwa hoteli hiyo, maarufu kama Matema Lake Shore Resort. <br />
<br />
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kanisa hilo, Mchungaji Marcus Lrhner, anasema kuwa Kanisa la Uinjilisti lilifanya utafiti na kugundua kuwa eneo hilo linafaa kuweka vivutio na vivutio hivyo vinaweza kukuza sekta ya utalii nchini. Anasema kumekuwa na mafanikio kutokana na kuwapo kwa kivutio hicho. <br />
<br />
Mafanikio hayo yanatokana na juhudi za kanisa hilo, kwa kupitia wafadhili wake, ambao kwa miaka nane sasa wamekuwa wakijitahidi kutunza mazingira. Mchungaji Lehner anasema kwamba utafiti uliofanywa pia ulizingatia kuwapo kwa eneo zuri la kuogelea, lenye mchanga safi na mzuri. Anasema Lake Shore Resort inatoa huduma za kulala na chakula cha asili, kinachoandaliwa kwa muda maalumu (kwa oda). <br />
<br />
Pia, ina nyumba mbalimbali zenye jumla ya vyumba 22, ikiwamo vyumba vya kujihudumia (self contained) na vyumba vya vitanda viwili hadi vitano. Zipo pia nyumba za ghorofa, zinazomwezesha mgeni kutazama vizuri ziwa, lilivyo na umbo lake, kabla ya kutumia usafiri wa boti, wa miguu au gari. Huduma hizo pia hupatikana hapo. <br />
<br />
Matema ipo katika eneo la Kaskazini, mwishoni mwa Ziwa Nyasa, ndani ya Wilaya ya Kyela. Ziwa lina upana wa wastani kilomita 60 na urefu wastani kilomita 550. Lipo kwenye Bonde la Ufa katika Afrika Mashariki na lina ujazo wa mita 500 kutoka usawa wa bahari. Ufukwe wa Matema unapambwa na safu za mlima Livingstone, wenye urefu wa mita 3,000.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-26560436562224884802009-11-26T10:45:00.000+03:002009-11-26T10:45:50.922+03:00Dk Salim: Ukiona nchi ina matatizo, wa kulaumiwa ni viongozi<div style="text-align: center;">Hawra Shamte <br />
</div><br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4xPcOEqeI/AAAAAAAAAHo/azHacfRhfU0/s1600/dr+salim+salim.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4xPcOEqeI/AAAAAAAAAHo/azHacfRhfU0/s320/dr+salim+salim.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div style="text-align: center;">Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) Dk Salim Ahmed Salim ambaye ameeleza kuwa nchi inapokuwa na migogoro mingi wanaostahili kulaumiwa ni viongozi.<br />
</div><br />
<br />
JITIHADA mbalimbali zinafanyika kuhakikisha kuwa nchi za Kiafrika zinafuata utawala wa sheria na pia kuzingatia haki za binadamu. <br />
<br />
Mbali na nhi wahisani, nchi zilizoendelea na hata mashirika ya umoja wa mataifa kusisitiza umuhimu wa utawala wa sheria na haki za binadamu, zipo taasisi huru zilizo ndani ya nchi za Kiafrika ambazo nazo zinashajiisha uwepo wa utawala bora katika nchi za Afrika. <br />
<br />
Mojawapo ya asasi za namna hiyo ni taasisi ya Mo Ibrahim ambayo mwanzilishi wake ni Dk Mohamed Ibrahim mzaliwa wa Sudan na tajiri aliyejikita katika masuala ya mawasiliano. <br />
<br />
Mjumbe wa bodi ya taasisi ya Mo Ibrahim, Dk Salim Ahmed Salim anasema tatizo la nchi nyingi za Afrika ni ukosefu wa Utawala Bora, katika Makala hii, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Nchi za Afrika (OAU) Dk Salim aliyezungumza na mwandishi wetu HAWRA SHAMTE anaeleza jinsi ukosefu wa utawala bora unavyokinza demokrasia barani Afrika... <br />
<br />
Swali: Bara la Afrika linakabiliwa na matatizo mengi ya kivita, ya kiuchumi, ya kisiasa na ya kijamii. <br />
<br />
Mwasisi wa taasisi ya Mo Ibrahim, Dk Mohamed Ibrahim, raia wa Sudan hivi karibuni alizungumza katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam na kusema kwamba tatizo kubwa la nchi za Kiafrika ni ukosefu wa utawala bora, lakini dhana ya utawala bora ni pana sana, je, wewe unazungumza nini kuhusu dhana hii? <br />
<br />
Jibu:Hakuna asiyetambua kuwa Bara hili lina nyenzo nyingi sana, lina kila aina ya mali, rasilimali yetu kubwa kuliko zote ni watu wetu ambao wanafanyakazi usiku na mchana tena katika mazingira magumu. <br />
<br />
Kuna kila aina ya madini katika bara letu, dhahabu almasi na kadhalika, pamoja na hayo tuna mafuta pia katika bara letu. Kuna ardhi kubwa sana katika Afrika, kuna mito na maziwa ya kila aina lakini bado nchi zetu, watu wetu ndio wenye umasikini kuliko watu wote duniani. <br />
<br />
Kwanini inakuwa hivyo? Kwa kweli hii inatokana na uongozi, kwa hiyo suala la uongozi bora ni suala la msingi, pale ambapo uongozi wa nchi umekuwa na uwezo wa kuhakikisha kwamba wanashughulikia maslahi ya watu wao, kunakuwa na tofauti kubwa. <br />
<br />
Katika utoaji zawadi kwa viongozi bora, mchakato unaofanywa na taasisi ya Mo Ibrahim tunaangalia kiongozi alifanya nini kuboresha hali ya watu wake wakati akiwa madarakani. <br />
<br />
Bara letu lina matatizo ya kiuchumi, lina matatizo ya rushwa kubwa sana, lina matatizo ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, lina matatizo ya uvunjaji wa haki za binadamu. <br />
<br />
Taasisi ya Mo Ibrahim inachofanya ni kusaidia mchakato wa kidemokrasia na utawala bora, kwani si kweli kama bara la Afrika ni matatizo tu, si kweli kwamba kila nchi ya Afrika inanuka rushwa. <br />
<br />
Kwa kweli kuna juhudi kubwa zinafanyika katika bara letu na mchakato wa kidemokrasia umepiga hatua nzuri pamoja na kwamba mwaka jana na mwaka huu tumepata misukosuko kidogo; matukio ya Guinea kwa mfano ambako wananchi wanauliwa na utawala wa kijeshi, matukio ya Mauritania, matukio ya Guinea Bissau na halafu zaidi matukio ya Somali na matukio ya Sudan. <br />
<br />
Kwa mfano Sudan siyo suala la Darfur tu lakini ni nini mustakabali wa Sudan na nini itakuwa taathira ya mambo yanayotokea Sudan kwa bara letu la Afrika. <br />
<br />
Kote unapoona kunakuwa na matatizo, kwa kweli wa kulaumiwa kwanza ni uongozi. Pale panapokuwa na uongozi safi, unaojitolea, uongozi usioshiriki ufisadi, uongozi unaojali zaidi maslahi ya watu wake, gurudumu la maendeleo linasonga mbele, lakini pale ambapo viongozi wanajilimbikizia mapesa, wanafanya mambo ya kidikteta na kadhalika, nchi hiyo hata ikiwa na nyenzo vipi haiwezi kwenda mbele. <br />
<br />
Swali: Umeeleza kuwa katika maeneo yenye matatizo kama vile ya kivita ni ukosefu wa uongozi, lakini je, nchi kama Somalia ambayo wanapigana wenyewe kwa wenyewe na mpaka sasa inaitwa nchi isiyokuwa na dola je, tatizo ni hilo tu la kukosa uongozi bora? <br />
<br />
Jibu:Ukitazama sana matatizo ya Somalia utaona kuwa ni ukosefu wa uongozi. Wanaopigana Somalia hivi sasa ni watu na wanaopata matatizo makubwa ni wananchi wa kawaida. Majemedari wa kivita ni viongozi mbalimbali wa Somalia na hawa walichofanya ni kuweka maslahi yao mbele kuliko maslahi ya watu wao. <br />
<br />
Kama kuna nchi ya Kiafrika ambayo haikutegemewa kuwa na matatizo kama haya ilikuwa ni Somalia kwa sababu ni nchi ambayo watu wake wana dini, moja, wana utamaduni mmoja na wanazungumza lugha moja, isingetegemewa kuwa watu kama hao itatokea siku watapigana wenyewe kwa wenyewe, familia moja inaua familia nyingine. <br />
<br />
Tatizo la Somalia ni ukosefu wa uongozi bora unaofikiria maslahi ya watu wake, lakini tatizo hilo si la Somalia tu, tazama Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) ni nchi moja ambayo pakiwa na utulivu, pakiendeshwa utawala bora itakuwa ni chachu ya maendeleo siyo ya Kongo tu bali ya sehemu kubwa sana ya bara la Afrika. <br />
<br />
Lakini Kongo haikupata amani kwa muda mrefu sana, ingawa hivi sasa Rais Kabila anajitahidi kujaribu kuleta amani kwa kiwango kikubwa lakini bado kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe, bado kuna watu wanafikiria maslahi yao, namna gani ya kupata fedha kwa njia za haramu kuwa ni jambo kubwa zaidi kuliko jambo jengine. <br />
<br />
Swali: Unafikiri ni nini suluhisho la matatizo haya? <br />
<br />
Jibu: Sidhani kama unaweza kuwa na suluhisho la namna moja kwa sababu kila pahala na mazingira yake. <br />
<br />
Chukulia Somalia kwa mfano, Somalia kuna Al Shabab, hawa wanasema wao ndio Waislam safi na wanataka kuleta Uislam, lakini ni upuuzi mtupu, kwa sababu haiwezekani kuwa brandi yako tu ya Uislam ndiyo iwe bora kuliko nyingine hufiki mbali. <br />
<br />
Lakini pia Somalia ilipuuzwa, baada ya matatizo yaliyotokea Mogadishu wakati wa Jenerali Aideed na Marekani kupata msukosuko; wanajeshi wa Kimarekani waliingia kwa dhamira ya kutoa misaada ya kibinadamu 'humanitarian' halafu humanitarian ikabadilika wakaanza kuingia katika mapambano, askari wa Kimarekani wakauliwa katika helikopta yao na wakaburutwa; toka wakati ule Marekani iliitenga kabisa Somalia. <br />
<br />
Nakumbuka nilipokuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Afrika, nikienda Marekani naweza kuzungumza tatizo lolote lakini si Somalia, ilikuwa ukitaja Somalia wanakwambia achana nao hao. <br />
<br />
Kwa hivyo ni nchi ambayo ilitengwa, Marekani waliitenga lakini na jamii kubwa pia waliitenga, tukaiachia inaendelea tu… <br />
<br />
Jingine ni kuwa viongozi wa nchi ile wakaanza kugawana; Somalia iliyokuwa jamii moja, wakaanza kugawana sasa kuna makabila, ukoo, familia na kadhalika. Ingawa hivi sasa Somalia kuna juhudi zinafanyika lakini juhudi zozote zinazofanyika lazima waishirikishe Al Shabab. Huwezi kupata ufumbuzi wa kivita pale lazima pawe na mazungumzo ya dhati kabisa… <br />
<br />
Kwa DRC juhudi kubwa imefanyika, hali iliyoko DRC sasa hivi tofauti sana na miaka mitatu, minne, mitano iliyopita lakini bado kuna matatizo Mashariki ya Kongo, kwanini? Moja ya matatizo yetu katika bara letu, imekuwa hizi rasilimali tulizonazo, nyenzo tulizonazo, madini tuliyonayo baada ya kuwa faida kwa watu wetu imekuwa kama ni dhambi, kama ni laana, sasa inakuwa pale palipo na mafuta matatizo, palipo almasi matatizo, palipo dhahabu matatizo, mimi nadhani changamoto kubwa ya bara letu ni namna gani ya kugeuza hizi rasilimali, hizi nyenzo tulizonazo, baada ya kuwa ni sehemu ya matatizo iwe ni sehemu ya kuleta maendeleo kwa bara zima na kwa manufaa ya watu wetu. <br />
<br />
Kwa upande wa Sudan kwanza tatizo lilikuwa baina ya Kaskazini na Kusini, vita viliendelea kwa muda mrefu sana na watu wengi walifariki, takwimu zinasema watu kama milioni nne walifariki katika vita vya wenyewe kwa wenyewe baina ya Kaskazini mwa Sudan na Kusini mwa Sudan. <br />
<br />
Mwaka pale. Mwaka 2005 yakapatikana makubaliano ya kijumla (Comprehensive agreement). <br />
<br />
Halafu kuna suala la Darfur, huko nako kuna matatizo makubwa, mpaka hivi sasa juhudi zilizofanyika kujaribu kutanzua hazijafanikiwa. <br />
<br />
Lakini hivi sasa hali ya Sudan imekuwa ngumu zaidi na mimi binafsi inanitisha kidogo, inanitisha kwa sababu siyo tu suala la Darfur lakini kuna uwezekano wa kuwa na fujo zaidi kama ndugu zetu wa serikali ya Sudan ya Kaskazini na ndugu zetu wa SPLM hawakuwa na makubaliano ili kura ya maoni ya mwaka 2011 ikafanyika katika mazingira mazuri na halafu wakaheshimu matokeo ya kura ile. <br />
<br />
Tatizo lililopo hivi sasa inaonyesha kuwa badala ya kuwa na umoja wa Sudan kuna uwezekano kuwa watu wengine wakataka kujitenga. <br />
<br />
Najua kama kuna watu wengine wanafurahia kujitenga, wanasema kujitenga ni nzuri, lakini ukianza suala la kujitenga katika bara letu na hasa katika nchi kubwa kama Sudan kuna taathira zinazoweza kutokea siyo tu ndani ya Sudan lakini pia katika majirani wa Sudan. <br />
<br />
Kwa hiyo mimi nafikiri hili jambo la Sudan kwa sasa Jumuiya ya Kimataifa na hasa nchi za Kiafrika zinapaswa kulipa uzito wake na kujaribu kuhakikisha kwamba katika huu muda uliobakia kila jitihada zinafanywa ili kuwafanya wananchi wa Sudan wajione kuwa ni wamoja na hasa ambao wanahisi kwamba wameonewa. <br />
<br />
Tatizo kubwa la Sudan ni kwamba wananchi walio katika pembezoni wanahisi kwamba wametengwa (siyo kama hawana sababu) na maslahi yote na maendeleo yote yanatokea katika sehemu moja tu ya Sudan. <br />
<br />
Jambo moja ambalo linaweza kuwa zuri ni kujaribu kuibana serikali ya Sudan kuzungumza na ndugu zetu wa SPLM waandae mazingira ili wananchi wa Kusini mwa Sudan watakaopiga kura waseme kwamba jamani tuhakikishe hili suala la umoja linapatikana. <br />
<br />
Lakini kama hilo halipatikani basi angalau waandae mazingira ya kuwa huo mchakato wa kura za maoni uwe wa amani na wakubaliane na mapema kama kuna kura ya maoni likitokea hili tutafanya nini, lisiachwe tu kama bomu likapasuka kwa sababu kama hakuna hivyo kuna hatari kabisa kwamba ufikapo mwaka 2011 bila mawasiliano, <br />
<br />
bila mapatano bila ushirikiano hali ya Sudan ikaendelea kuwa tete na inapoendelea kuwa tete haitokuwa tu Kusini mwa Sudan lakini itaathiri pia sehemu mbalimbali za Sudan ambazo pia zina matatizo yake, Darfur, Kordufan, Blue Nile na kadhalika. <br />
<br />
Swali: Kumezuka mtindo mwengine wa demokrasia barani Afrika, sasa hivi demokrasia mbali ya kuwa ni mchakato wa uchaguzi lakini mwisho wa siku inabidi lazima watu wakae katika meza za majadiliano. Na zimezuka hizi serikali za mseto kama Kenya na Zimbabwe, je, nini maoni yako kuhusu hilo? <br />
<br />
Jibu: Kila sehemu ina mazingira yake maalum. Demokrasia maana yake ni kwamba wananchi wenyewe wawezeshwe kuchagua viongozi wao na namna serikali wanayoihitaji na serikali hiyo iwaongoze kwa muda gani na wawe na uwezo wa kubadilisha viongozi wao muda ule unapofika. <br />
<br />
Lakini mazingira yatofautiana, kwa mfano; katika Kenya baada ya mauaji yaliyotokea mara baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 na kuleta taathira kubwa kwa maendeleo ya Kenya kulikuwa na umuhimu wa kutafuta usuluhishi na mawasiliano na maafikiano ya namna fulani, kwa hivyo serikali ya mseto iliyoundwa Kenya, ilikuwa na madhumuni hayo. <br />
<br />
Ukitazama mazingira yalivyokuwa, ukawa mkaidi tu ukasema hakuna haja ya kuwa na serikali ya pamoja kwa kweli unakosea, unawatakia ndugu zetu wa Kenya waendelee katika maafa tu. <br />
<br />
Zimbabwe kidogo tofauti na Kenya, lakini kama wenyewe wamekubaliana, tunapaswa kuheshimu makubaliano. Ukitazama uchaguzi wa Zimbabwe ulivyokwenda, Chama cha MDC katika uchaguzi wa wabunge kilishinda, suala lilikuwa je, uchaguzi wa Rais ulikuwaje? Bahati mbaya mazingira hayakuwa yanaruhusu kufanya uchaguzi ambao ungekuwa huru na wa haki. <br />
<br />
Kwa hivyo katika mazingira kama hayo, mimi nadhani ilikuwa ni busara kujaribu kuwakutanisha viongozi ili waweze kuona jinsi ya kuwa na muundo wa serikali ambao utazingatia maslahi ya watu wote wa Zimbabwe. <br />
<br />
Na pamoja na kuwa bado kuna matatizo nchini Zimbabwe, lakini nadhani hilo lilikuwa ni jambo la busara. Mimi nadhani pale ambapo kuna ushindani mkubwa sana wa kisiasa na ambapo bado watu hawajaweza kustahmiliana na kuweza kujua kuwa wewe unaweza ukawa chama fulani, mimi nikawa katika chama kingine, hata katika familia moja; baba akawa chama fulani, mama akawa chama kingine na watoto wakawa chama kingine na mkaendelea katika familia bila matatizo; pale ambapo ustahmilivu kama huo haupo. <br />
<br />
Ni muhimu sana kufanya utaratibu wa kushirikisha watu wote katika utawala, vinginevyo utaendelea katika mapambano tu na panapo mapambano ni muhali kupata maendeleo ya kudumu ya kiuchumi.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-55417647954212568692009-11-26T10:37:00.000+03:002009-11-26T10:37:26.499+03:00Jamani hatupungi mashetani hapa, tunasomaNa Brandy Nelson, Chunya <br />
<br />
<br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://4.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4v1NGzK6I/AAAAAAAAAHg/-B3lRY3YMuw/s1600/chini+ya+mbuyu.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://4.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4v1NGzK6I/AAAAAAAAAHg/-B3lRY3YMuw/s320/chini+ya+mbuyu.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">Wanafunzi wakiwa darasani wakiendelea na masomo<br />
</div><br />
<br />
HADI kufikia mwaka 2000 kijiji cha Udinde kilikuwa na shule moja ya msingi iitwayo Udinde iliyochukua watoto kutoka vitongoji vya jirani pia, lakini ulipoanzishwa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (Mmem) mwaka 2002 ilionekana haja ya kufanya maboresho. <br />
<br />
Shule hiyo ilipachuliwa ikazaa shule nyingine ya msingi katika kitongoji cha Iboma mwaka 2003. <br />
<br />
Uamuzi wa kujenga shule nyingine, mbali ya kufanya maboresho ulilenga pia kuwapunguzia wanafunzi adha ya kutembea umbali wa kilomita 10. <br />
<br />
Serikali ya kijiji hicho kilichopo kata ya Kapalala tarafa ya Kwimba wilaya ya Chunya mkoani Mbeya ikitumia pesa zilizotokana na Mmem ilifanikiwa kujenga darasa moja tu na hadi sasa halijakamilika wala halijaongezwa darasa jingine wala vyoo na nyumba za mwalimu. <br />
<br />
“Shule hii ilimegwa kutoka shule ya msingi Udinde ambapo hapa Iboma tuliletwa walimu watatu na mazingira yenyewe ni kama haya unavyoyaona. Wazazi walichangia kujenga darasa hili moja na serikali kupitia Mmem ikamalizia paa ingawa darasa lenyewe bado halina sifa ya kuwa darasa kwani halijakamilika,†anasema mwalimu Albert Juakali ambaye alikutwa akifundisha hisabati wanafunzi wa darasa la kwanza. <br />
<br />
Uamuzi wa haraka uliofanywa na walimu ni kuhamishia ‘mikoba’ yao kwenye mti wa mbuyu ulio jirani na kuweka mbao. Upande mmoja wanakaa darasa la kwanza, halafu upande mwingine darasa la pili, la tatu, la nne, la tano nk. Wakati wa juakali shida na wakati wa mvua ni likizo. <br />
<br />
Mwenye masikitiko zaidi ni mwalimu mkuu wa shule, Onesmo Mdamu ambaye anasema;"Sikiliza, shule hii ina muda wa miaka sita mpaka sasa lakini ina darasa hili moja tu na ambalo linatumika kwa ajili ya watoto wa darasa la sita na hawa wa madarasa mengine wanasoma kwenye mti wa mbuyu ambao pale kuna madarasa matano yaani la kwanza, pili, tatu, nne na tano kama mnavyoona wenyewe." <br />
<br />
Hayo ndiyo maisha ya wanafunzi wa shule hiyo na uamuzi wa kutumia mti huo kama darasa ulipitishwa na kamati ya shule. <br />
<br />
Madhara <br />
<br />
Mazingira hayo yamewasaidia zaidi watoto wasiopenda elimu maana huona heri kwenda kujishughulisha na uvuvi wa samaki kwenye Ziwa Rukwa lililojirani na shule hiyo badala ya kushinda kwenye juakali chini ya mti. <br />
<br />
"Mazingira ya shule hii ni magumu kutokana na kuwa na darasa moja ambalo linatumiwa na wanafunzi wa darasa la sita. Shule yenyewe kama unavyoiona iko kandokando ya Ziwa Rukwa hivyo inapelekea watoto kuamua kujishughulisha na ajira ya uvuvi wa samaki kutokana na mazingira magumu ya shule na ugumu wa maisha wa familia zao na hivyo kukosa haki ya kupata elimu bora," anaongeza Juakali. <br />
<br />
Aliyeamua kubadili matumizi ya mbuyu kutoka kwenye imani za asili kwamba ni makazi ya mashetani hadi kuwa darasa la wanafunzi 134 ni kamati ya shule. Kamati hiyo ya shule imeshindwa kuhamasisha wananchi yajengwe madarasa mengine. <br />
<br />
Kinachofanyika chini ya mti wa mbuyu, Mdamu anasema wanafunzi huchukua mabanzi na kuweka juu ya matofali na sehemu ya kuandikia wakitumia matofali kama meza na wengine wakishindwa kupata mabanzi hutumia matofali kama viti. <br />
<br />
"Hali hii ni mbaya kielimu kwani hata sisi walimu hatujui tumwachie nani hawa wanafunzi, basi tumeona tuungane na usemi usemao 'Ualimu ni Wito', lakini kwa ujumla hali ni mbaya sana. Hata mahudhurio ya wanafunzi ni finyu kutokana na kukatishwa tamaa na mazingira na kupelekea kujiingiza katika shughuli za uvuvi wa samaki,†anasema <br />
<br />
Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Leopard Ngairo mbali ya kuelezea historia anakiri kwamba mazingira ya ufundishaji ni magumu na yanachangia wanafunzi kukosa elimu bora na hivyo wengine kuamua kuacha shule na kujiingiza katika ajira ya shughuli za uvuvi wa samaki. <br />
<br />
"Shule ina darasa moja pekee, ina uhaba wa madawati, ofisi za walimu, vifaa vya kufundishia hakuna ambapo kwa sasa shule ina vitabu viwili kwa kila darasa, kwa kweli walimu wanashindwa kutoa elimu ipasavyo kwa wanafunzi," anasema Ngairo. <br />
<br />
“Hii shule ina matatizo makubwa huwezi kufananaisha na shule zingine kwani wazazi wengi wanakatishwa tamaa na mazingira yake na inasababisha wazazi kuwaruhusu watoto wao kutafuta ajira katika shughuli za uvuvi badala ya kwenda shule,†anasema <br />
<br />
Darasa la saba <br />
<br />
Septemba mwaka huu walimu na kamati ya shule walisugua vichwa kuona namna nzuri ya kuwasaidia wanafunzi wa darasa la saba waliotarajiwa kufanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi. Hapo tena, walimu na kamati ya shule walikubaliana kulihamishia darasa hilo Udinde kwa ajili ya kumalizia elimu yao ya msingi. <br />
<br />
"Hapa kwa kweli hakuna elimu bora inayopatikana kwani mazingira yote kwa ujumla ni magumu siyo kwa wanafunzi wala sisi walimu kwani hakuna hata vitendea kazi na tunaishi mbali na shule na inatulazimu kutembea umbali wa kilometa tisa ili kuweza kufika hapa shuleni," anasema Mdamu. <br />
<br />
Mahitaji ya shule hiyo ni kuwa na walimu watano lakini waliopo wanaofanya kazi ni wawili pekee, hakuna vitabu vya kufundishia kwani vilivyopo ni vitabu viwili kila darasa na kwamba madawati ni tatizo kubwa hali inayopelekea watoto hao kukaa kwenye matofali. <br />
<br />
Walimu hao wamekuwa wakifundisha kwa moyo wote na wamekuwa wakipeleka ripoti kila mwezi kwa afisa elimu wa halmashauri kuwajulisha hali halisi ya shule, lakini hakuna kinachofanyika na kuifanya shule hiyo kutokuwa na maendeleo yoyote. <br />
<br />
Mdamu analalamika pia kwamba hali hiyo kwa kiasi fulani inachangiwa na baadhi ya wazazi katika kitongoji hicho kukosa mwamko wa kuwapeleka watoto wao shule na badala yake wamekuwa wakijikita zaidi kwenye shughuli za uvuvi kuliko suala la elimu kutokana na mazingira ya shule hiyo. <br />
<br />
Mwalimu mkuu anadhani kwamba ufumbuzi wa haraka juu ya matatizo ya shule umo kwenye mikono ya viongozi wa wilaya na mkoa. <br />
<br />
"Kama viongozi wa serikali ya wilaya na mkoa wangetembelea na kushuhudia mazingira ya shule na kuwahamasisha wananchi wajitolee nguvu zao kujenga shule ni jambo ambalo lingesaidia watoto hao kupata elimu bora badala ya bora elimu ambayo wanaipata kwa sasa," anasema. <br />
<br />
Wanafunzi nao wamefikia hatua ya kuuona ukweli kwamba hakuna wanachopata katika mazingira kama haya. Adela Alex, mwanafunzi wa darasa la sita anasema mazingira ya shule hiyo ni magumu na hivyo kupelekea kushindwa kupata elimu bora na kusabibasha baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo kukatamaa na kuendelea na shule na kujiingiza katika shughuli za uvuvi wa samaki kwa kufanya vibarua na kujipatia fedha kidogo. <br />
<br />
"Kwa kweli sisi wanafunzi tunaona hali hii ni mbaya kwetu tunaona kama tumetengwa labda sisi siyo raia wa Tanzania au labda serikali inatuona kama wanyama, haiwezekani tukawa tunasoma shule katika mazingira haya ya chini ya mti wa mbuyu halafu tukasema kuna kitu tunakipata; hakuna tunachokipata hapa chini ya mti,"anasema kiongozi wa wanafunzi Emanuel Mkombe. <br />
<br />
Anasema kuwa mazingira hayo hayawawezeshi kusoma vizuri yanawakatisha tama ndiyo maana kuna baadhi ya wanafunzi wamekimbia na kuamua kufanyakazi ya vibarua ziwani. Lakini kuna wanafunzi wengine ambao wana nia ya kusoma ndiyo maana wameendelea kuwa wavumilivu na kukubali kusoma chini ya mti wa mbuyu. <br />
<br />
Mkombe anasema kuwa kuna hatari ya wanafunzi wote wasichana kwa wanaume kukimbilia ziwani kwa ajili ya kupata ajira katika shughuli za uvuvi ambako wanalipwa fedha kidogo kuanzia kati ya Sh 500 hadi Sh 200 kwa kazi wanazopewa ikiwa ni pamoja na kupasua samaki, kutafuta kuni, kuosha nyavu na kukausha samaki. <br />
<br />
Anasema kuwa ajira hiyo ni mbaya kwa watoto na ni hatari kutokana na wengi wao kupata ajali mbalimbali ziwani ikiwa ni pamoja na kukamatwa na mamba na kupoteza maisha bado wakiwa na umri mdogo. <br />
<br />
"Tunaiomba Serikali iliangalie suala hili la mazingira ya shule yetu ili na sisi tuweze kupata haki ya kupata elimu kama wanavyopata wenzetu ili tuweze kuokoa maisha yetu na kujinusuru na ajira hii mbaya ya watoto katika Ziwa Rukwa kwani sidhani kama kuna watoto wenzetu wengine wanasoma katika mazingira kama haya," anasema. <br />
<br />
Mtazamo huo ndio alionao Ngairo kwamba: "Kama unavyoona tunaendelea kuomba wananchi na wadau wa Elimu kutuchangia ujenzi wa shule yetu na na sasa tumeanza kujenga darasa lingine na nyumba za Walimu kwa mchango wa nguvu za wananchi lakini bado tunahitaji msaada mkubwa kutoka kwa wananchi,wadau wa elimu na Serikalini." <br />
<br />
Katibu wa Elimu, Uchumi, Malezi na mazingira wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Chunya, Philipo Mulugo anasema mazingira ya Iboma yanatia uchungu. <br />
<br />
"Mazingira ya shule ya Iboma yanatia uchungu sana kwani serikali kupitia ilani ya CCM inapaswa kuliangalia hili na sisi kama viongozi wa chama na wadau wa elimu tunatakiwa kulipokea kwa masikitiko ikiwa ni pamoja na kushiriki kwa kuisaidia serikali katika ujenzi wa shule hii ya Iboma," anasema <br />
<br />
"Sidhani kama kuna mtu ambaye atasikia taarifa ya mazingira ya shule ya Iboma ataamua kukaa kimya, basi huyo atakuwa siyo mpenda maendeleo ya elimu na mimi nitakwenda huko kama katibu wa elimu na nitapeleka mifuko ya saruji 10 ili iweze kuwasaidia,"anasema <br />
<br />
Mulugo ametoa wito kwa wanachi wa Iboma na wale wa kata ya Kapalala wanaoishi nje kujitoa kwa hali na mali ili kuisaidia shule hiyo kuwanusuru wanafunzi kusoma chini ya mbuyu ili waweze kupata elimu bora. <br />
<br />
Lakini Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya Maurus Sapanjo amesema kuwa haifahamu hiyo shule na hajawahi kufika katika shule hiyo. <br />
<br />
"Kwa kweli lazima niwe mkweli na muwazi siifahamu hiyo shule na wala afisa elimu wangu hajawahi kunipa taarifa ya shule hiyo kwamba kuna shule ina darasa moja na wanafunzi wanasoma chini ya mti wa mbuyu. Ndiyo kwanza nimeisikia kupitia gazeti la Mwananchi na imenisikitisha sana kuona katika wilaya yangu kuna shule yenye matatizo kama haya,"anasema. <br />
<br />
Sapanjo anasema kuwa siyo nia yake na hajafurahishwa na taarifa hizo kwani malengo yake ni kuhakikisha baada ya miaka 10 watoto wa wilaya ya Chunya wanafika vyuo vikuu. <br />
<br />
Anasema angekuwa anaijua shule hiyo asingekimbilia kujenga shule za sekondari za kata 18 wakati kuna shule ya msingi ina darasa moja na wanafunzi wanasomea chini ya mti wa mbuyu. <br />
<br />
"Nimemwagiza afisa elimu wangu pamoja idara nzima ya elimu kuhamia shuleni hapo na kuhakikisha madarasa yanajengwa kwa haraka ili kuondokana na adha hiyo," anasema juu ya hatua alizochukua. <br />
<br />
Kuhusu wanafunzi kujishughulisha na uvuvi wa samaki badala ya masomo, amesema msako mkali unafanyika kuhakikisha watoto wote wanarudi shuleni haraka na kuwachukulia hatua za kisheria wazazi wote watakaobainika wanashiriki katika kuwaruhusu watoto wao kufanya kazi ya vibarua ya uvuvi wa samaki na shughuli nyingine ziwani.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-62260913900625474612009-11-26T09:35:00.000+03:002009-11-26T09:35:56.811+03:00Mtikisiko wazuka Baraza la MawaziriMwandishi Wetu <br />
Raia Mwema<br />
<br />
Novemba 25, 2009<br />
<br />
<ul><li>Kikwete yaanza kumshinda</li>
<li>Sasa hata Dk. Shein azoza</li>
</ul><br />
SIKU chache tu baada ya kutuma ujumbe kwamba akipita mwakani hatabeba mawaziri wazee, Rais Jakaya Kikwete ameanza kutekeleza azma hiyo kwa kuwatangazia mawaziri wake kwamba amechoshwa nao kwa kuwa hawamsaidii, imefahamika.<br />
<br />
Habari ambazo Raia Mwema imepata zinasema kwamba Rais Kikwete na hata wasaidizi wake, Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wamekuwa wakali isivyo kawaida yao katika vikao vyao vya kazi.<br />
<br />
Kwa mujibu wa habari hizo, katika kipindi kiasi cha wiki mbili zilizopita, Rais Kikwete amekutana na mawaziri wake mara mbili na katika vikao hivyo amesema waziwazi kwamba mawaziri wake hawamsaidii kama alivyotarajia wakati akiwateua.<br />
<br />
"Hakikua kikao cha baraza, lakini alizungumza kwa ukali akiwaambia kwamba alipowateua alikuwa na matumaini makubwa nao kwamba atakuwa amepunguza kwa kiasi kikubwa uzito wa kazi. <br />
<br />
"Akawaambia amekuwa akilazimika kufanya mambo mengi ambayo yangeweza kufanywa na mawaziri wake aliowaamini na akawapa dhamana," anaeleza ofisa mmoja wa serikali aliyezungumza na Raia Mwema wiki kwa masharti ya kutotajwa gazetini.<br />
<br />
Mtoa habari huyo amesema wiki iliyopita Rais Kikwete alikuwa mkali kwa wasaidizi wake kuliko ilivyopata kutokea tangu aingie madarakani mwishoni mwa mwaka 2005.<br />
<br />
Imefahamika kwamba kabla ya kikao cha wiki iliyopita, kilichofanyika nje ya Dar es Salaam, Rais Kikwete aliwaita mawaziri wake ghafla katika hatua ambayo ilizua hofu miongoni mwao wakiamini kwamba huenda alitaka kuvunja Baraza lake.<br />
<br />
Habari zaidi zinasema katika kikao cha awali waziri mmoja mwanamke alikwepa kuhudhuria baada ya kupata fununu kwamba Rais Kikwete alikuwa amekerwa na baadhi ya kauli zake za hivi karibuni. <br />
<br />
Habari zinaeleza kwamba, hata Dk. Shein ambaye anafahamika ya kuwa mara nyingi hana hulka ya ukali amebadilika, na sasa naye ameanza kuwa mkali waziwazi katika vikao vya utendaji. <br />
<br />
"Kuna kikao kimoja ambacho baada ya Rais kumbana waziri mmoja kutokana na kuwasilisha waraka uliokuwa umejaa mapungufu, Makamu naye alizungumza kwa ukali akimtaka waziri huyo kuacha kufanya mambo bila kufuata taratibu," anasema mtoa habari huyo.<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://4.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4hRc-6DeI/AAAAAAAAAHY/f-XPUTNck-c/s1600/JK.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; cssfloat: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://4.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4hRc-6DeI/AAAAAAAAAHY/f-XPUTNck-c/s320/JK.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<div style="text-align: left;"><br />
</div><div style="text-align: left;"><span style="font-size: xx-small;">Rais Jakaya M. Kikwete</span><br />
</div><br />
Anaongeza: " Katika kikao hicho Rais alimkatiza waziri huyo mara kwa mara akitaka ufafanuzi na wakati mwingine kumlazimisha waziri huyo kubadili baadhi ya mambo ambayo aliona yana makosa mengi katika waraka wake.”<br />
<br />
Ukali wa ghafla wa Rais Kikwete, Dk. Shein na Pinda unatajwa kuwa umechochewa na utendaji usioridhisha wa mawaziri wengi unaosababisha viongozi hao wa juu kabisa kulazimika kufanya kazi ya ziada. <br />
<br />
Katikati ya habari hizo ni hali kwamba mawaziri wengi wanashindwa kuitetea na kuisimamia Serikali ndani na nje ya Bunge, mbele ya umma na katika shutuma nyingi zinazotajwa kwenye vyombo vya habari. Anasema mtoa habari huyo: "Rais alieleza wazi kwamba anakerwa na taarifa za mara kwa mara katika vyombo vya habari zikionyesha udhaifu mkubwa wa Serikali yake huku wasaidizi wake wakiwamo mawaziri wakishindwa kutoa hoja zenye nguvu au mkakati mahususi wa kukabiliana na taarifa hizo.”<br />
<br />
Japo tathmini inaonyesha kwamba si rahisi katika muda mfupi uliobaki kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu kuwa na mabadiliko katika Baraza la Mawaziri, Raia Mwema imearifiwa ya kuwa tayari mchakato umeanza ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa wa kuchunguza mienendo ya watu wakiwemo wajumbe wa sasa wa Baraza la Mawaziri na wajumbe watarajiwa ikibidi kufanyika kwa mabadiliko.<br />
<br />
Habari zaidi zinaeleza kwamba yamekuwapo mapendekezo kwa Rais Kikwete ya kutaka abadili baadhi ya mawaziri waliopo kwa baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakitajwa kuwa wako msitari wa mbele katika inayotajwa kuwa ni vita ya ufisadi katika hatua ya kukisafisha Chama cha Mapinduzi (CCM) katika tuhuma za ufisadi na migawanyiko ya dhahiri ili kuvutia kura katika uchaguzi wa mwakani.<br />
<br />
Mbali ya kuingiza sura mpya na kupunguza baadhi ya mawaziri, kuna taarifa kuwa yapo mapendekezo kwa Rais ya uwezekano wa kupandisha ngazi naibu mawaziri walioonyesha uwezo mkubwa.<br />
<br />
Haya yakiendelea zimekuwapo taarifa za wizara mbalimbali ambako wafanyakazi wanawalalalimikia mawaziri wao kwa utendaji kazi usioridhisha.<br />
<br />
Kati ya waliotajwa na wafanyakazi hao ni pamoja na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, John Chiligati; Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya na Naibu wake, Dk. Makongoro Mahanga; Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsha Mwangunga na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utawala Bora, Sophia Simba.<br />
<br />
Lakini akizungumza na Raia Mwema wiki iliyopita Chiligati alisema “hawezi kufanya mtihani na kujisahihishia mwenyewe.” <br />
<br />
“Hayo maoni ya watu siwezi kuyaingilia, mimi siwezi kufanya mtihani na kujisahihisha mwenyewe lakini naamini watendaji ofisi wanajua naingia ofisini saa ngapi na natoka saa ngapi,” alisema Chiligati na alipoulizwa kuhusu shughuli za chama kuingilia majukumu ya serikali, alisisitiza kutotaka kujisahihishia mtihani.<br />
<br />
Katikati ya mwezi huu akizungumza na vijana wa kutoka nchi mbalimbali za Afrika mjini Dar es Salaam, Rais Kikwete alituma salamu za mwanzo kwa wateule wake kwa kuwaambia vijana hao ya kuwa endapo atajaliwa kuongoza tena Tanzania mwakani, atafanya jitihada kubwa kuondokana na sura za wazee ambao atawabadilisha na vijana.<br />
<br />
Akizungumza katika mkutano wa vijana hao wa kulea viongozi wa Afrika, Rais Kikwete alisema atafanya mabadiliko makubwa kwenye Serikali yake akshinda uchaguzi ujao.<br />
<br />
Alisema Kikwete: “Wale viongozi wa rika langu, lazima waanze kuwaachia nafasi vijana. Tunahitaji wakuu wa wilaya vijana zaidi, wakuu wa mikoa vijana zaidi na hata mawaziri vijana zaidi. Ndivyo ilivyotokea kwetu sisi wakati tukiwa vijana.”Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-61947174306165079312009-11-26T09:28:00.000+03:002009-11-26T09:28:21.587+03:00Mheshimiwa Rais Kikwete na first Lady wakitalii huko Jamaica<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://3.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4fn6z3nfI/AAAAAAAAAHQ/BbTsT4pIoII/s1600/kikwete+bembea.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://3.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw4fn6z3nfI/AAAAAAAAAHQ/BbTsT4pIoII/s320/kikwete+bembea.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">Rais Jakaya na mkewe Salma wakibembea hewani kutalii vivutio nchini Jamaica pamoja na Waziri wa Utalii nchini humo,Edmund Barlett (kulia) na Horace Clarke, mmiliki wa bembea hilo lipitalo meta 50 hewani umbali wa kilometa mbili.<br />
</div>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-22350530003031697122009-11-25T16:06:00.000+03:002009-11-25T16:06:40.059+03:00Mabadiliko huja kwa dhamira ya kweli ya Kutekeleza Ahadi.<div class="separator" style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none; clear: both; text-align: center;"><a href="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw0rAIRCSUI/AAAAAAAAAHI/54qYXCrXQns/s1600/kikwete.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/Sw0rAIRCSUI/AAAAAAAAAHI/54qYXCrXQns/s640/kikwete.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;"><br />
</div><div style="text-align: center;"><span style="font-size: xx-small;">Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania </span><br />
</div><div style="text-align: center;"><span style="font-size: xx-small;">Jakaya Mrisho Kikwete.</span><br />
</div>Sijui kama kweli tunataka mabadiliko au tunaombea mabadiliko yatokee. Sijui kama tunafanya ili kusababisha mabadiliko au tunasubiri wengine wafanye ili tufurahie mabadiliko; Sijui hata kama tunajua vizuri ni mabadiliko gani hasa tunayataka na kama tunataka ni juhudi gani tumezifanya kushiriki kwenye mchakato wa kuleta mabadiliko hayo.<br />
<br />
<br />
Tunaweza kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kujaribu kubadilishana mawazo mchana kutwa na usiku kucha lakini mabadiliko hayaji kwa kusema. Mabadiliko hayaji kwa kupigiwa magoti au kwa kukemea giza usiku. Mabadiliko husababishwa na kutekelezwa.<br />
<br />
Tukijifunza kwenye kampeni ya Obama utaona kuwa Wamarekani hawakuombea tu kuwa kiongozi mzuri au wamtakaye aje na alipojitokeza hawakukaa pembeni kuombea kuwa afanye vizuri ili hatimaye "alete mabadiliko" wanayoyataka. Wamarekani walishirikishwa katika kampeni kuanzia kuchangia fedha, muda wao, vipaji vyao n.k<br />
<br />
Je kwanini tunafikiri sisi Tanzania tutapata mabadiliko kwa kubishana vijiweni na kwenye mitandao na kuoneshana nani anajua nini na anahusika na nini? Mabadiliko ndugu zangu hayaji kwa kunuia au kuwa "kusudio zuri" au kwa kujua ufisadi ulivyo mbaya na fisadi ni nani!!<br />
<br />
Mabadiliko huletwa na watu waliokusudia kuleta mabadiliko hayo. <br />
<br />
Je una mawazo yoyote kuhusu kushiriki katika mabadiliko tunayoyataka au kutoa mchango wa aina yoyote? <br />
<br />
Niandikie utupe mawazo yako.<br />
<br />
<a href="mailto:kyelacommunity@live.com">kyelacommunity@live.com</a>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-28062508204668209982009-11-25T10:58:00.000+03:002009-11-25T11:19:27.549+03:00Huu si wakati wa Kukata tamaa<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><br />
</div><div class="separator" style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none; clear: both; text-align: center;"><a href="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwzjJGbbc_I/AAAAAAAAAHA/xEV3IYwsvf4/s1600/mwakyembe6.jpg" imageanchor="1" style="cssfloat: left; height: 338px; margin-left: 1em; margin-right: 1em; width: 218px;"><img border="0" src="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwzjJGbbc_I/AAAAAAAAAHA/xEV3IYwsvf4/s320/mwakyembe6.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div class="" style="clear: both; text-align: center;"><span style="font-size: xx-small;">Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe</span><br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;"><br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;">Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha yanaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu familia zetu, jamii zetu, au nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?". <br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;"><br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;">Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kujihisi kuvunjwa moyo (discouraged) na hivyo kuona kuwa hakuna lolote na chochote kinachoweza kufanyika Tanzania ambacho kinaweza kuturudisha kwenye matumaini?<br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;"><br />
</div><div style="text-align: left;"><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;">Je huu ndio wakati wa kukata tamaa na kuwaachia mafisadi wafanye wapendavyo? Je huu ndio wakati wa kukubali viongozi wabovu na wasio na uwezo alimradi tuendelee katika hali ya utulivu, amani na mshikamano? Je huu ni wakati wa kusalimu amri na kukubali kile ambacho kimetuangukia na kuwa yote ni "mapenzi ya Mungu"?<br />
</div><br />
</div><div style="text-align: left;">Je unajihisi kukata tamaa ukiangalia mambo yanayoendelea katika nchi yetu?<br />
</div><div style="text-align: left;"><br />
</div><div style="text-align: left;">Niandikie:<br />
</div><div style="text-align: left;"><br />
</div><div style="text-align: left;"><a href="mailto:kyelacommunity@live.com">kyelacommunity@live.com</a><br />
</div>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-45184542272714424952009-11-25T10:17:00.000+03:002009-11-25T10:17:56.107+03:00Tabia za Watoto zinatokana na Makuzi.Na Africar T Kagema<br />
<br />
<br />
<br />
<div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;"><a href="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwzY7uHItAI/AAAAAAAAAGo/5Kk6_DORpQc/s1600/children+4.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; cssfloat: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwzY7uHItAI/AAAAAAAAAGo/5Kk6_DORpQc/s320/children+4.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><div style="border-bottom: medium none; border-left: medium none; border-right: medium none; border-top: medium none;">Makuzi ya mtoto yanaweza kugawanywa katika nyanja kadhaa mfano makuzi ya kimiwili, kiakili, kimaono,kimaadili n.k. Katika makala hii tutajaribu kuona jinzi marafiki wanavyoweza kuathri ukuaji wa mtoto kimaadili. Upo msemo kuwa tabia ya mtu inaweza kueleweka vyema kwa kuzingatia tabia ya rafiki yake au marafiki zake. Msemo huu unatilia mkazo dhana nzima ya kuchagua marafiki wema ili kujenga tabia njema. <br />
</div><br />
Malezi ya mtoto huanzia nyumbani kwa wazazi wake. Kipindi cha awali cha maisha ya mtoto (miaka 0-2) mtoto huishi zaidi katika mazingira ya nyumbani na tabia zake zote hutegemea tabia za watu wa nyumba husika. Baada ya hapo mtoto huanza kutoka na kuchanganyika na watoto wa nyumba jirani pamoja na watu wa vimo tofauti na yake. <br />
<br />
Pia kwa hali ilivyo sasa watoto huanza kwenda shule za awali au madrasa (miaka 3-6). Baadaye hujiunga na shule za msingi kuanzia miaka 7 - 14 na hatimaye kuingia sekondari akiwa na umri wa miaka 15-19. Tutaona kuwa umahiri wa stadi mbalimbali kama lugha, michezo,hobi na mengineyo hupatikana katika kipindi ambacho mtoto ameshaanza kuwa na maingiliano na watu wa nje ya familia yake. <br />
<br />
Tutakubaliana kuwa wazazi kama waalimu wa mwanzo kabisa wa motto (Nursery Teachers) watahusika sana na mustakabali mzima wa tabia za mtoto wako. Hawa ndiyo wenye jukumu ya kumjengea msingi mzuri wa maadili ya jamii ambapo chimbuko la tabia njema hupimwa kutokana na jinsi mtu anavyoweza kutenda mambo yake kwa kuzingatia maadili ya jamii husika. <br />
<br />
Katika nyumba ambayo maadili huchungwa watoto hujifunza pia kuchunga maadili. Marafiki katika familia hizi hulingana kabisa na familia husika katika suala zima la kuzingatia maadili. <br />
<br />
Utakapofika wakati wa mtoto kutoka nyumbani na kuingia mitaani tayari kuwa amejengewa msingi ambao utamsaidia kupata marafiki wema. Awali wazazi humsaidia mtoto kuchagua marafiki ambao huwa ni wale wanaotoka katika familia zenye maadili mema. <br />
<br />
Msingi huu pia humsaidia mtoto kuchagua hobi nzuri ambazo haziendi kinyume na maadili ya jamii. Izingatiwe kuwa tabia za wizi, uvutaji wa bangi, madawa ya kulevya, utoro shuleni n.k. huigwa na watoto wakiwa katika vikundi. Kama wazazi watawaacha watoto wao bila kuwapa muongozo bora wa namna ya kupata marafiki wema basi wasishangae watoto wao kukosa kabisa makuzi mema katika hii nyanja ya maadili na hivyo kuishia kuwa watu mizigo "liability" katika jamii. <br />
<br />
Hivyo natoa wito kwa wazazi kukaa na watoto wao bila kuchoka kung’amua mabadiliko ya tabia zao ili waweze kuzibadilisha mapema kabla hazijazoeleka na kuonekana ni kitu cha kawaida kwao. Ni vema pia kufuatilia mafundisho wanayopewa watoto wawapo shule za awali ili kutambua maadili yanayoizunguka shule hiyo na kuchukua hatua mapema. <br />
<br />
Kanisa au Misikiti ni sehemu muhimu sana kwa watoto kuhamasishwa kuhudhuria ili waweze kujifunza maadili ya Mungu. Watoto wanaoshindwa kuhudhuria makanisani au Misikitini huwa wanakosa mengi kwani zile ni sehemu zinazofundisha watoto maadili mema katika jamii. Vipindi kama vya Sunday School kwa wakristo na madrassa kwa waislam ni vipindi vizuri sana katika maadili ya watoto katika umri wao mdogo.<br />
<br />
Watoto wakalishwe chini na waelezwe kipi cha kufanya na wakati gani, na kipi cha kutofanya na katika mazingira gabi. Wazazi wasipuuzie na kuacha tabia mbaya za watoto zikiendelea kukomaa, kwani kwa kufanya hivyo kutasababisha kushindwa kuwarekebisha mara wakiachwa na tabia zao. Kama wazee wasemavyo ‘’mkunje samaki angali mbichi’’, kwani akikauka (akikomaa awezi kufunzika tena).<br />
<br />
Watoto wadogo wanahitaji watu wazima ili waweze kuwaongoza na kuwasaidia ili wajifunze tabia na maadili yanayokubalika na yale yasiyokubalika. Wanahitaji pia watu wa kuwasaidia ili wajifunze namna ya kushirikiana na wengine. Jinsi tunavyotoa muongozo wa namna hii inategemea malengo yetu kwa watoto tunaowafundisha, tunataka watoto hawa wawe watu wa aina gani? Je wawe na nidhamu ya woga na kutojiamini au wafundishwe tabia ya kutegemeana na yale yanayokubalika na yasiyokubalika. <br />
<br />
Kumuongoza mtoto kunahitaji muda na uvumilivu, ni jambo muhimu sana iwapo mzazi anatumia muda fulani katika kuchunguza tabia na mwenendo na kujitahidi kurekebisha kwa upole. Hasira na ukali havisaidii; kama maji yazimavyo moto, upole hurekebisha tabia ya mtoto haraka sana. Tukumbuke pia watoto ni wanafunzi siku zote, wanahitaji uzoefu kutoka kwetu. Ni juu yetu basi kuwapa kilicho bora na muhimu katika uanafunzi wao.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-63556490143689751592009-11-25T09:55:00.000+03:002009-11-25T09:55:18.693+03:00Kawambwa ahimiza ujenzi wa Kiwanja cha ndege Songwena Gordon Kalulunga, Mbeya<br />
<br />
<br />
WAZIRI wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, amehamasisha ukamilishaji wa Kiwanja cha Ndege cha Songwe, kilichopo mkoani Mbeya, baada ya kutembelea uwanja huo na kuukagua, kisha kuzungumza na mkandarasi na mhandisi mshauri wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini uwanjani hapo. <br />
<br />
Kawambwa alitembelea na kuukagua uwanja huo juzi na kuwahimiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Mkandarasi Kampuni ya Kundan Singh Construction Ltd ya nchini Kenya na mhandisi mshauri kutoka Falme za Kiarabu kuhakikisha ujenzi wa uwanja huo unakamilika mapema iwezekanavyo. <br />
<br />
Waziri huyo alisema kuwa kwa sababu awali kikwazo cha uendelezaji wa ujenzi wa uwanja huo kilikuwa ni kutolipwa malipo ya awali mkandarasi anayejenga uwanja huo, lakini kwa sasa tayari serikali imekwisha kulipa deni hilo, hivyo hatarajii kuendelea kusuasua kwa ujenzi katika kiwanja hicho. <br />
<br />
“'Kwa sababu serikali imelipa fedha zote za malipo ya awali kwa mkandarasi, hivyo hatutarajii kuona ujenzi wa uwanja huu ukisuasua kama mwanzo, maana kikwazo kilikuwa ni fedha,”' alisema Waziri Kawambwa. <br />
<br />
Aidha, alifafanua kuwa ifikapo Januari mwaka 2010 anatarajia kupata taarifa nzuri zaidi za maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo, ambao ni tegemeo kubwa la wananchi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na taifa kwa ujumla. <br />
<br />
“'Kwa kipindi cha mwaka wa bajeti 2008/2009 serikali imetenga sh bilioni 18 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa kiwanja hiki ambacho kina umuhimu sana kwa taifa letu, hivyo ni muhimi pia nanyi kama wataalamu mkaona kuwa ni jinsi gani serikali ilivyoupa kipaumbele uwanja huu,” alisema Kawambwa kwa matumaini ya kumalizika kwa uwanja huo kama matarajio ya serikali yalivyo. <br />
<br />
Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa kiwanja hicho mbele ya Waziri huyo wa Miundombinu kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Prosper Tesha, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi na Uhandisi, White Majula, alisema mkandarasi tayari amemaliza kukata na kujaza udongo njia za kuruka na kutua ndege ambazo waziri alizitembelea na kuzikagua. <br />
<br />
“Maeneo yote ya usalama katika njia ya kuruka na kutua ndege yenye urefu wa mita 1,800 tayari mkandarasi ameyakamilisha kwa asilimia 65 na amekamilisha kazi ya ufungaji wa mitambo ya kusaga mawe kwa ajili ya kokoto na ameanza kufunga mtambo wa lami,” alisema Majula. <br />
<br />
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya uhakika vya habari, imeelezwa kuwa kampuni hiyo kutoka Falme za Kiarabu tayari imelipwa shilingi bilioni 3.1, ambapo kiwango hicho cha fedha kinajumuisha gharama za kazi za kufanya marejeo ya usanifu wa njia za kuruka na kutua ndege pia usimamizi wa utekelezaji wa ujenzi unaoendelea. <br />
<br />
Kandarasi ya kumalizia kazi za ujenzi wa kiwanja hicho cha Songwe ilisainiwa Septemba 12 mwaka 2008 na kukabidhiwa Oktoba 19, mwaka huo huo, inatakiwa kazi hiyo ikamilike kwa kipindi cha miezi 18 kwa gharama ya sh bilioni 32.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-52414936742689597562009-11-24T12:25:00.000+03:002009-11-24T12:25:22.932+03:00Ufisadi chanzo cha wananchi kupoteza imani kwa CCMNA MWANDISHI WETU <br />
<br />
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwumLlyKsGI/AAAAAAAAAGI/qKC8VV0GBto/s1600/Makamba2.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; cssfloat: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://2.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwumLlyKsGI/AAAAAAAAAGI/qKC8VV0GBto/s320/Makamba2.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<span style="font-size: xx-small;">Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Yusuf Makamba</span>.<br />
<br />
Watanzania wanasifika katika bara la Afrika kwa uvumilivu wao hata nyakati zisizoweza kuvumilika. Dhana hii inaweza kuwa ni matunda aliyotuachia Hayati Mwalimu Julius Nyerere. <br />
<br />
Dalili za uvumilivu zinaonekaka wakati wa Utawala wa Serikali ya awamu ya nne. Serikali na viongozi wake wamekuwa wanaendesha serikali kinyemela kana kwamba haikuchaguliwa na wananchi. <br />
<br />
Mdororo wa uchumi haukuanza leo katika dunia hii. Tofauti ya mdororo wa uchumi unaotuathiri sasa ni kwamba una miale mikali kuliko midororo ya uchumi iliyopita. <br />
<br />
Ni katika mvurugano huu wa uchumi, Watanzania walitegemea kwamba viongozi waliowachagua na hatimaye kuunda serikali wangetafuta mbinu mbadala ili kulinasua Taifa na watu wake ili miale ya mdororo wa uchumi uliopo usingewaumiza sana. Matokeo yake ni kwamba wanaongeza joto la miale na waathirika wa miale hiyo ni Watanzania asilimia 85 waliotopea katika ufukara ndio wanaoumia kwenye joto la mdororo huo. <br />
<br />
Wizi uliojitokeza na unaofanywa na vigogo wa Serikali ya CCM ni dalili fika zinazoonyesha kuwa maadili na itikadi iliyozoeleka ya CCM vyote hivyo vimewekwa kando. <br />
<br />
Watuhumiwa wote wa wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ni vigogo wa CCM na wale wa serikali yake. <br />
<br />
Katika orodha hiyo ya watuhimiwa hakuna hata mwananchi mmoja aliye fukara ametuhumiwa na wala hakuna hata mwanachama mmoja wa vyama vya upinzani amediriki kujihusisha na ufisadi. <br />
<br />
Ufisadi wote unaozungumzwa ni wa viongozi wa serikali ambao wamefikishwa mahakamani jambo ambalo Watanzania wanaona ni mchezo wa kuigiza. <br />
<br />
Watanzania wanaona ni mchezo wa kuigiza kwa sababu vigogo wote waliofikishwa mahakamani ukijumulisha kile kinachodaiwa wameiba haifiki sh. bilioni 133. Hapa panajitokeza swali ambalo halina majibu kwamba hao wengine ambao wanatuhumiwa kinadharia tu watafikishwa lini mahakamani? <br />
<br />
Tanzania inashuhudia amani ya mioyo tuliyorithi kutoka kwa Mwalimu Nyerere imetoweka kabisa. Watanzania wanapozungumza amani sio lazima zilie bunduki. <br />
<br />
Ukosefu wa amani ni pamoja na kukosa mitaji, kukosa milo mitatu kutwa, dhuluma, rushwa na ufisadi vikiwa mstari wa mbele kuzidi nchi zote zilizo chini ya jangwa la Sahara.<br />
<br />
Kukosekana kwa ajira, kuongezeka kwa ujambazi na ujangili si dalili nzuri ya kudumisha amani katika Taifa. Matatizo haya yote yalipaswa kurekebishwa na serikali. <br />
<br />
Viongozi wetu wakiwa chini ya mwamvuli wa Rais Jakaya Kikwete hawaonekani kukemea maovu haya ambayo Watanzania hawakuzoe kuwa nayo. <br />
<br />
Wazee wetu kama Peter Kisumo, Pancrasi Ndejembi, Joseph Butiku, Mohamed Raza, John Malecela, wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Waandishi maarufu kama Jenerali Ulimwengu wao wamekuwa wanayavalia njuga maovu yote yanayovurundwa na viongozi wetu kwa bahati mbaya serikali na chama chake imekuwa haitoi msisitizo ili kuafikiana na mawazo hawa.<br />
<br />
Kwa mfumo huu wa falsafa na siasa ambazo ni za nadharia tu zimekuwa hazina tija kwa Watanzania. Hotuba za majukwaani zimekuwa haziendani na vitendo na hatimaye kudumaza usalama katika nchi na kuwaacha Watanzania wakijiuliza, wanakokwenda. <br />
<br />
Suala zima katika Taifa ni kwamba nchi haina amani kwa sababu, wananchi hawana mlo uliokamilika, mafukara wa kutupwa wakati viongozi wao wanajinafasi kana kwamba wako mbinguni, usalama majumbani umekuwa haupo kwa sababu ya ujambazi uliokirithiri na polisi ina vitendea kazi duni ukifananisha na silaha zilizomo mikoni mwa majambazi. <br />
<br />
Tatizo jingine Taifa halijaongeza ajira kwa polisi. Polisi tuliyonayo sasa ni ileile aliyotuachia Mwalimu Nyerere. <br />
<br />
Kukosekana kwa utawala bora katika Taifa kumeathiri sana suala zima la usalama katika nchi. Watendaji wa tarafa, mitaa, vitongoji na kata wamekuwa tishio kubwa kwa usalama wa Raia.<br />
<br />
Watendaji hawa wanajiita watunza usalama madaraka ambayo hata katika Katiba ya nchi hayapo. Kwa mshangao wa Watanzania wengi watendaji wamekuwa wanachukua sheria mikononi huku wakijua sio stahili yao, lakini wakuu wa mikoa na wilaya licha ya kushindwa kukemea, wamekuwa hawawachukulii sheria za nidhamu hivyo kuhalalisha vitendo vibaya vinavyofanywa na watendaji hao. Ukosefu wa utawala bora na sheria katika Taifa ndio umehatarisha usalama wa nchi. <br />
<br />
Dhana ya kudumisha demokrasia endelevu katika Taifa haipo. Serikali pamoja na CCM kama alivyosema Rais Kikwete wakati wa kuadhimisha miaka kumi ya kifo cha Mwalimu Nyerere ni kwamba viongozi wameacha kabisa kusikiliza kero za wananchi na kuwasaidia. <br />
<br />
Kinachobaki sasa ni porojo nyingi za siasa zisizokuwa na tija na kujilimbikizia mali ili kuja kugombea uongozi mwaka 2010. <br />
<br />
Wanasiasa wengi wamebadili dira na maendeleo ya kisiasa na hatima yake wamegeuza siasa mradi wa kujinufaisha wao na familia zao. <br />
<br />
Kwa sababu wakati wanagombea hivyo vyeo vya siasa wanatumia rushwa kwa hiyo wakivipata wanahakikisha fedha yao yote iliyotumika katika rushwa inarudishwa kwa nyakati mbalimbali. Hii ina maana kwamba, maendeleo ya wapiga kura yanawekwa pembeni. <br />
<br />
Watanzania ambao kusema kweli wamechoshwa na siasa za CCM zenye poroja nyingi na zisizokuwa na tija. Ili wajinasue kutoka kwenye matatizo hayo wanadhani ni wakati muafaka wa kukiweka Chama Cha Mapinduzi na watafute ustarabu mwingine ambao pengine unaweza ukaleta neema ambayo itawanufaisha wao na vizazi vijavyo. <br />
<br />
Suala ni kwamba Siasa za Tanu na CCM zimekuwa katika Tanzania kwa miaka 48 bila maendeleo yoyote kwa wananchi.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-44164868127827651722009-11-24T12:22:00.000+03:002009-11-24T12:22:20.487+03:00Tutaboreshaje elimu katika shule za serikali?BY BENJAMIN NKONYA <br />
<br />
Chimbuko la maendeleo ya elimu nchini ni matokeo ya michakato ya sheria, falsafa na sera zilizoanzishwa katika vipindi mbalimbali kabla na baada ya uhuru. Baada tu ya kupatikana uhuru mwaka 1961, serikali ilitunga sheria ya elimu namba 83 ya mwaka 1962 iliyofuta sheria ya elimu ya mwaka 1927 ambayo iliruhusu utoaji wa elimu na mafunzo kwa mfumo wa ubaguzi wa rangi, dini na makabila.<br />
<br />
Katika sheria hii, serikali iliekeza mitaala, uongozi na ugharamiaji wa elimu na mafunzo ufuate usawa. Azimio la Arusha la mwaka 1967 lilianzisha falsafa ya elimu ya kujitegemea ambayo ilisababisha mabadiliko makubwa katika sera za jumla za kijamii na kiuchumi. <br />
<br />
Falsafa hii, ambayo iliasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ndiyo inaweka dira katika mfumo wetu wa elimu hadi leo, inaweka mkazo katika kuondoa matabaka kwenye utoaji wa elimu, utengano (alienation) kati ya shule na jamii na kusaidia kuondoa kasumba ya wasomi ya kujibagua na kutumia elimu waliyoipata kwa manufaa yao binafsi. <br />
<br />
Aidha falsafa hii inaelekeza katika kuunganisha nadharia na vitendo, kwa dhana kuwa elimu isipatikane vitabuni tu bali ijumuishe na ile ipatikanayo kutokana na uzoefu wa kutenda au kufanya kazi ya kuongeza tija. <br />
<br />
Ili kuhakikisha kwamba haya yanafikiwa na pia kuhakikisha kwamba wanafunzi wanawajibika na upatikanaji wa mahitaji yao, falsafa hii inaelekeza shule kuwa vituo vya kuzalisha mali ili kuchangia gharama za uendeshaji kwa asilimia ishirini na tano. Pia elimu inayotolewa katika ngazi zote iwe na maarifa na stadi za kumwezesha mhitimu kuishi na kufanya kazi yenye manufaa katika jamii.<br />
<br />
Katika kutekeleza falsafa hii, shule karibu zote zilitaifishwa na kuendeshwa na serikali kuanzia mwaka 1967. Ili kuondoa aina zote za ubaguzi, serikali ilikubali kugharamia elimu katika ngazi zote. Pamoja na hayo, kila shule ilianzisha mashamba ambayo yalikuwa maarufu kama mashamba ya elimu ya kujitegemea. Hali hii ilimfanya mwanafunzi wa Kitanzania kuwa tayari kujitegemea mara tu baada ya kuhitimu mafunzo ya elimu ya msingi. Kwa hakika falsafa hii ilishabikiwa sana na kila Mtanzania.<br />
<br />
Pamoja na uzuri wa falsafa hii, kuna changamoto zilizoukabili mfumo mzima wa elimu katika miaka kumi ya utekelezaji wa falsafa hii. Kama wote tunavyofahamu, katika nusu ya pili ya miaka ya 1970, ubora wa elimu yetu ulishuka sana kiasi kwamba serikali iliruhusu walimu wasio na sifa kuanza kufundisha katika shule za msingi. <br />
<br />
Changamoto hii iliambatana na ukosefu wa zana za kufundishia na kujifunzia kama vitabu, maabara, maktaba n.k. Sambamba na changamoto hii, ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi halikuenda sambamba na ongezeko la idadi ya vyumba vya madarasa na samani zake, achlia mbali nyumba za waalimu. <br />
<br />
Hivyo ililazimu chumba kimoja cha darasa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi kuliko idadi inayomfanya mwalimu alimudu darasa kiufundishaji. Pamoja na changamoto hizo, hata suala la usimamizi wa elimu nalo lilikuwa gumu kutokana na shule kuwa nyingi katika mtawanyiko wa kijiografia ambao una ufanisi mdogo. Matokeo ya hali hii ilikuwa ni kushuka kwa elimu kwa haraka sana.<br />
<br />
Serikali iling’amua changamoto hizi na kutafuta namna ya kuziondoa ili elimu iendelee kutolewa kwa ubora unaotegemewa. Mwaka 1978 Bunge lilitunga sheria mpya ya elimu namba 25 ambayo, pamoja na mambo mengine, iliruhusu watu binafsi, mashirika ya dini, asasi za kiraia na makampuni kuanzisha, kusajili na kuendesha shule. <br />
<br />
Kuanzishwa kwa sheria hii kulianza kuonyesha matumaini ya kunusuru ubora wa elimu kwani shule nyingi binafsi zilionyesha mafanikio. Kuna changamoto kadhaa ambazo zilijitokeza katika miaka kumi na tano ya kwanza ya utekelezaji wa sheria hii. <br />
<br />
Changamoto hizi zilirekebishwa kupitia sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 1995. Hivyo mfumo wetu wa sasa wa utoaji wa elimu na mafunzo nchini unaongozwa na sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 1995 (iliyopata nguvu kutokana na marekebisho ya sheria ya elimu Na. 25 ya mwaka 1978 iliyorekebishwa kwa sheria Na. 10 ya mwaka 1995), sera ya elimu ya ufundi ya mwaka 1996 na sera ya elimu ya juu ya mwaka 1999.<br />
<br />
Pamoja na ukweli kwamba shule za serikali zinaendeshwa kwa kodi za Watanzania pamoja na ufadhili mwingi sana kutoka mashirika mbalimbali ya ndani nje ya nchi, elimu yetu, hasa inayotolewa na shule za serikali, bado ina changamoto nyingi sana katika viashiria vya utoaji (input), mchakato (process) na matokeo (outputs).<br />
<br />
Baada ya marekebisho hayo na baada ya sekta binafsi kujiimarisha ipasavyo, Watanzania wameendelea kushuhudia kukua kwa haraka sana kwa elimu katika sekta binafsi licha ya ukweli kwamba shule hizi hazina ruzuku yoyote kutoka serikalini. Sasa ni zaidi ya miaka thelathini tangu kuruhusiwa kwa sekta binafsi kuingia katika utoaji wa elimu. <br />
<br />
Pengine ingekuwa busara kudurusu sababu hasa za tofauti hizi na kutafuta namna ambavyo elimu yetu katika sekta ya umma inaweza kuboreshwa.<br />
<br />
Ni ukweli usionpingika kwamba gharama za uendeshaji katika shule za serikali ni kubwa kuliko gharama katikashule binafsi. Hii inatokana na ukweli wa kiuchumi kwamba kadri mradi unavyozidi kuwa mkubwa ndivyo ufanisi kwa kila shilingi inayotumika unavyozidi kushuka. Hali hii inakabili vilivyo shule zetu za serikali. <br />
<br />
Moja ya viashiria vya kushuka kwa ufanisi ni hii hali ya waalimu kuwa na malalamiko yasiyoisha kuhusu mapunjo wanayopata katika malipo yao, baadhi ya wanafunzi kuvuka madarasa na vidato bila kujua kusoma na kuandika, kukosekana kwa maabara, maktaba, vitabu na vifaa vingine vya kujifunzia na kufundishia na mambo mengine yanayofanana na hayo.<br />
<br />
Sababu nyingine za kudorora kwa elimu katika shule za serikali ni kuingiliwa kupita kiasi na wanasiasa. Utakuta taarifa ya wakaguzi inaonyesha kabisa kwamba shule fulani haitakiwi kusajiliwa kutokana na kutotimiza baadhi ya vigezo vya usajili. Pamoja na taarifa hizo, utakuta mwanasiasa anaingilia kati na kulazimisha shule hiyo isajiliwe. <br />
<br />
Hivyo hata uendeshaji wake huenda kisiasa siasa tu bila kujali vigezo muhimu vya uendeshaji wa shule. Utakuta shule ya serikali imesajiliwa lakini haina hata kitabu kimoja wala maabara. Itakuwa ni ajabu isiyo kifani kukuta shule kama hii ikitoa elimu bora.<br />
<br />
Hali ni tofauti kabisa katika shule binafsi. Shule hizi husimamiwa na kwa ukaribu sana. Shule hizi hukaguliwa na kusajiliwa baada ya kutimiza vigezo vyote vya usajili. Huwezi kukuta shule binafsi inasajiliwa wakati haina maktaba yenye vitabu au maabara zenye vifaa vyote. Hata baada ya usajili, wakaguzi hufika katika shule hizi mara kwa mara kuangalia kama kila kigezo cha utoaji wa elimu kinazingatiwa. <br />
<br />
Sambamba na hili, utakuta mmiliki wa shule hizi anafuatilia kwa karibu sana kila kinachoendelea shuleni na kuhakikisha wanafunzi wake wanapata huduma zinazotakiwa. <br />
<br />
Kwaujumla wake ni kwamba shule binafsi huendeshwa kwa kufuata mahitaji ya wateja wake na kutimiza masharti yote yanayowekwa na serikali.<br />
<br />
Kurunzi haioni kama itatosha tu kukosoa bila kutoa mapendekezo ya ubereshaji. Njia ya kwanza ni kuondoa siasa katika uendeshajiwa usajili na uendeshaji wa shule. <br />
<br />
Hii inaweza kufikiwa kwa njia ya kuifanya idara ya ukaguzi kuwa wakala inayojitegema badala ya hali iliyopo ya kuwa idara katika Wizara Elimu na Mafunzo ya Ufundi. <br />
<br />
Itakuwa ni ajabu ya ngariba kujitia suna mwenyewe kama kitengo hiki kitatenda haki hasa wakati shule ya serikali inapofanya makosa. <br />
<br />
Njia ya pili ni kuweka ushirikiano kati ya wamiliki wa shule binafsi na serikali ili kuondoa tatizo la kushuka kwa ufanisi wa usimamizi unaotokana na kukua kwa idadi ya shule zinazosimamiwa na mmiliki mmoja. <br />
<br />
Katika hali hii, mmiliki wa shule binafsi anaweza kuwekwa kuwa meneja wa shule ya serikali (hasa hizi za kata) iliyo karibu naye. Kama meneja, atahakikisha kwamba anashirikiana na bodi ya shule katika kuhakikisha kwamba shule hii ya kata inatoa elimu bora kama ilivyo shule yake.<br />
<br />
Elimu ni mali ya umma na inatakiwa kugharamiwa na umma hata kama inatolewa na shule/chuo binafsi. Kurunzi inaamini kabisa kwamba, tukilizingatia hili, tutakuwa tumekata kabisa mizizi yote ya ufisadi dagaa, papa na nyangumi na tutakuwa tumeenzi na kuhuisha fikra sahihi za Baba yetu wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-68255609667170247552009-11-24T12:10:00.000+03:002009-11-24T12:10:49.285+03:00Lishe duni inadumaza ukuaji wa watotoNA MWANDISHI WETU <br />
<br />
<br />
24th November 2009<br />
<div align="left" class="separator" style="clear: both; text-align: center;"><a href="http://3.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwuioHTBPLI/AAAAAAAAAGA/tSBO-mKW074/s1600/watoto.jpg" imageanchor="1" style="clear: left; cssfloat: left; float: left; margin-bottom: 1em; margin-right: 1em;"><img border="0" src="http://3.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwuioHTBPLI/AAAAAAAAAGA/tSBO-mKW074/s320/watoto.jpg" yr="true" /></a><br />
</div><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
Watoto wakisubiri mgao wa chakula.<br />
<br />
Utapiamlo kwa watoto bado ni tatizo kwa nchi zinazoendelea duniani ingawa wataalam wanasema nchi nyingi zimeweza kupiga hatua .<br />
<br />
Moja ya tatu ya vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kwenye nchi hizo zinahusishwa na ulaji duni , ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto (Unicef) inasema.<br />
<br />
UNICEF wanasema pia kuwa katika watoto wapatao milioni 195 mmoja kati ya watatu amedumaa kutokana na kukosa lishe bora , ingawa kiwango chao kimekuwa kikipungua kuanzia mwaka 1990.<br />
<br />
Ripoti hiyo inaeleza pia kuwa idadi ya watoto ambao wana uzito mdogo ukilinganisha na umri wao imebakia kubwa huku nchi nyingi zikifanya jitihada ili kuweza kufikia malengo yanayotakiwa walao kupunguza idadi hiyo ifikie nusu yake. <br />
<br />
Kiwango cha watoto wanaodumaa kukua kinaweza kuwa kikubwa kwa sababu wakati watoto wengine wana uzito wa kawaida wako pia watoto ambao wana uzito mkubwa zaidi- hii ni kutokana na kuwa chakula wanachokula ni duni na hivyo kuathiri ukuaji wao. <br />
<br />
Wataalam wanaonya kuwa mara nyingi hali kama hiyo ikitokea ni kitu kisichoweza kurekebishwa na mara nyingi inamfanya mtu kama huyo abakie na afya mbaya maisha yake yote.<br />
<br />
Kiongozi wa Unicef, Ann Veneman anasema kuwa : " Lishe duni inawanyima watoto nguvu kiasi kwamba baadhi ya magonjwa ambayo mwili ungeweza kupambana nayo unaweza ukashindwa na hiyo ni hatari kwao”. <br />
<br />
"Kama hatua za lazima hazitachukuliwa ili kuhakikisha kuwa mama na mtoto wanapata chakula bora tujue kuwa gharama yake itakuwa kubwa siku za baadaye.."<br />
<br />
Tunawezaje kumaliza tatizo hilo <br />
<br />
Moja ya maeneo ambayo yamefanyiwa kazi ni huko Peru, Amerika ya Kusini ambako tatizo la lishe duni lilikuwa kubwa.<br />
<br />
Mwaka 1999, serikali ya nchi hiyo kwa kushirikiana na Unicef walianzisha kwa pamoja na shirika la Maendeleola Marekani mradi wa kuwahudumia watoto katika umri mdogo.<br />
<br />
Mradi huo uliweza kuwatumia wafanyakazi wa afya kutoa huduma kwa akina mama baada ya kujifungua kwa kuwahimiza kunyonyesha watoto na kutoa chakula cha kulikiza katika majimbo matano ya vijiini.<br />
<br />
Ilipofika mwaka 2004, zaidi ya watoto 75,000 waliokuwa chini ya miaka mitatu ambao walikuwa wananufaika na mpango huo kiwango cha watoto wengi kudumaa kilipungua kutoka asilimia 54 hadi kufikia 37.<br />
<br />
Mpango huo kwa sasa unaendeshwa kwa nchi nzima ambapo wataalam wanaeleza kuwa siku za kwanza 1,000 za mtoto ambazo ni sawa na miaka mitatu ya mwanzo ni muhimu ili kuweza kutatua tatizo hilo.<br />
<br />
Wataalam hao wanasema kuwa suala la kuhimiza unyonyeshaji katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo ni muhimu.<br />
<br />
Hata hivyo Unicef wanasema kuwapatia watoto pia vyakula vya ziada ni suala litakalosaidia tatizo la lishe duni <br />
<br />
Mipango mingi inayohusiana na lishe imekuwa ikiongeza madini ya joto kwenye chumvi ili kuwasaidia watoto kupata madini hayo yanayochangia katika ukuaji wa ubongo pia kuwapatia vitamini Ambayo inasaidia katika ukuaji wa mifupa na kuuwezesha mwili kupambana na maambukizo.Hatua kama hiyo repoti hiyo ya Unicef inasema itasaidia kupunguza moja ya tano ya vifo vya watoto.<br />
<br />
Unicef inasema kuwa kwa kushirikiana na wadau wengine zikiwemo na serikali husika na mashirika ya misaada imekuwa ikipiga hatua katika kuboresha lishe kwa watoto kwenye nchi 150 zinazoendelea.<br />
<br />
Kuanzia mwaka 1990 uwiano wa watoto ambao wanakuwa na uzito mdogo imepungua kwa kiwango cha moja ya sita ,kulingana na mipango na takwimu ambazo Unicef na mashrika menginge wanayofuatilia suala hilo kama Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia. <br />
<br />
Hata hivyo pamoja na hatua hizo zote kuchukuliwa kwenye baadhi ya nchi hali ni mbaya kwani takwimu zinaonyesha kuwa kati ya nchi 117 ambazo zina tatizo hilo ni nchi 63 tu ndizo zitaweza kufikia Malengo ya Milenia katika kipengere hicho ambapo lengo ni kupunguza nusu ya idadi ya watoto wanaokuwa na uzito mdogo ifikapo 2015. <br />
<br />
Kwa upande wa Afrika hali ya mafanikio bado siyo makubwa wakati nchi za Asia zina afadhali kidogo na wakati Amerika ya Kusini imekuwa ikipiga hatua zaidi. <br />
<br />
Kitty Arie, mtaalam wa masuala ya sera kwenye shirika la Save the Children, anasema kuwa lishe duni ina madhara ya muda mrefu ikiwemo mtoto kushindwa kufanya vizuri shuleni.<br />
<br />
"Hili ni suala muhimu sana na linawezakana na ni lazima litafutiwe dawa.."Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-7242836472194416882009-11-23T08:52:00.000+03:002009-11-23T09:06:18.718+03:00Mwakyembe akataa kuzungumzia hoja za Rostam Aziz<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Fidelis Butahe na Mussa Mkama </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">MBUNGE wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe jana aliamua kutozungumzia sakata la Richmond, na hasa hoja za hivi karibuni za mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ya kutaka uchunguzi mpya wa kashfa hiyo kwa kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge ni ya uongo na haikuwa na baadhi ya nyaraka muhimu. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Katika siku za karibuni, Rostam amenukuliwa akitaka uchunguzi mpya wa kashfa hiyo ufanyike, akipendekeza kazi hiyo ifanywe na jopo la majaji na kwamba endapo jopo hilo litamkuta na hatia, atakuwa tayari kujiuzulu nyadhifa zake zote, hoja ambayo imepingwa kwa maelezo kuwa maamuzi ya Bunge hayawezi kuchunguzwa upya na muhimili mwingine wa dola. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Dk Mwakyembe, mmoja wa wabunge wanaojilikana kama makamanda wa vita ya ufisadi, ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo teule ya Bunge ambayo ripoti yake ilisababisha Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake wa waziri mkuu na mawaziri wengine wawili. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Lakini jana, mbunge huyo wa Kyela alikataa kata kata kuzungumzia suala hilo pamoja na hoja za Rostam. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Dk Mwakyembe aliombwa kuzungumzia suala hilo wakati wa mkutano mkuu wa kwanza wa Mfuko wa Maendeleo wa Watu wa Kyela (KDF), uliofanyika Chuo Cha Ufundi (Veta) jijini Dar es Salaam. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">"Hapana siwezi kuzungumza lolote leo hapa ni masuala ya KDF tu... nisingependa kuzungumza mambo ambayo sikupanga kuyasema na wala hayahusiani na mkutano huu,"alifafanua na Dk Mwakyembe. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">"Nimetoka Mbeya leo na kule kuna ugeni wa Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa, lakini watu wa Kyela wameniambia nije kwa sababu ya umuhimu wa mkutano huu. Kwa hiyo siwezi kuzungumza mada iliyo nje ya mkutano huu, samahani sana." </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">Mwenyekiti wa KDF, Gray Mwakalukwa alisema katika ufunguzi wa mkutano huo kuwa lengo la kuanzishwa kwa mfuko huo ni kuchangia juhudi za serikali katika maendeleo hasa katika elimu. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">"Tangu kuanza kwa mfuko huu mwaka 2006 hivi sasa Kyela kuna maendeleo makubwa, hasa katika sekta ya elimu... sasa kuna shule nyingi za sekondari tofauti na kipindi cha nyuma," alisema Mwakalukwa ambaye pia ni mkurugenzi mkuu wa Shirika la Taifa la Madini (Stamico) na ambaye alikuwa kamishna wa madini. </span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;"><br />
</span><br />
<span style="font-family: Georgia, "Times New Roman", serif;">"KDF imefanya mengi Kyela, ilinunua vitanda 60 kwa ajili wa wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Kiwira Coal Mines, lakini pamoja na hayo tumefanya mengi sana ambayo kuyasema yote inahitaji muda wa kutosha."</span>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-62060312176574108632009-11-20T15:38:00.000+03:002009-11-20T15:42:43.466+03:00Umasikini wa Tanzania ni wa Kujitakia<strong><span style="color: lime;">Africar T Kagema</span></strong><br />
<br />
<strong><span style="color: lime;"><span style="font-size: 85%;">UNDP inatoa taarifa juu ya "The concentrated poverty". Yaani umaskini wa kutisha, kwa bahati mbaya Tanzania ni moja ya nchi zilizo chini ya mstari mwekundu wa umaskini ambao wao wanaita "below poverty level" au absolutely poverty". Huu ni umaskini unaozidi kawaida ya umaskini, waweza kuita umaskini sana, au umaskini zaidi, ama umaskini mno, lakini yote hayo yanaashiria neno moja tu nalo ni kwamba umaskini unaoikabili nchi yetu ni sawa kabisa na ugonjwa wa ukimwi kwa maana ya kwamba umaskini wetu sasa hautibiki.</span> </span></strong><br />
<br />
KATIKA kuufafanua umaskini, mtu aweza kuuweka ama kuugawanya katika mafungu mawili, umaskini wa nchi (au taifa) na umaskini wa watu au "mass poverty" yaani walio wengi katika ujumla wao. Enzi za mkoloni nchi yetu ilikuwa na umaskini wa watu tu yaani "individuals" lakini haikuwa na umaskini wa dola kama uliopo sasa ambapo takribani asilimia 50 ya bajeti ya serikali inatoka kwa wahisani.<br />
<br />
Katika uhalisi wa mambo nchi yetu ni ombaomba, hata wanaodai Mkapa amerudisha heshima ya Tanzania kimataifa sijui wanatumia vigezo gani kwani katika ukweli wa maisha hakuna omba omba yeyote aliyepata kuheshimika. Heshima ya Tanzania italetwa kwa kujitegemea na kujitosheleza, kwanza kwa chakula na baadaye kwa mahitaji mengine, yaliyo muhimu kwa taifa. Enzi za mkoloni Tanganyika ilikuwa nchi ya kwanza kwa uzalishaji wa mkonge ambapo ilitoa asilimia 28 ya mahitaji ya dunia ukiacha mazao mengine kama nyonyo, karanga, pamba na ngozi, na kahawa. <br />
<br />
Kwa mapato hayo serikali ya mkoloni haikuwa lofa iliweza kujenga mabarabara, njia za mawasiliano, na kutoa elimu bora kwa hao waliobahatika kusoma. Kwa maneno mengine walau serikali iliweza kujitegemea, lakini sasa kila kitu kiko nyang'anyang'a na hoi bin taabani. Hakuna mradi wowote wa kitaifa ambao ungeweza kutoa ajira ya maelfu kama ukoloni, hakuna watu wabunifu ndani ya hiyo kada ya watawala badala yake umahili wao uko kwenye kudhibiti wapinzani na kuendesha mizengwe ya kuwawezesha kubaki madarakani. Wao watawala, ushindi wanaouona muhimu ni ule tu wa uchaguzi mkuu. Ule ukweli kwamba wao baada ya kuwashinda wapinzani, nao wameshindwa na umaskini hawaujali wala hawaoni aibu. <br />
<br />
Inapotokea kwamba dola imekuwa maskini hadi kuendeshwa kwa misaada toka nje ya nchi na watu (wananchi) nao wakawa maskini hadi kufikia kiwango cha kushindwa kufanya lolote na kubaki kama walemavu kungojea kudra za Mungu basi hapo kuna tatizo mara mbili yaani tatizo la umaskini na tatizo la watu wenyewe. Lakini papo hapo viongozi wakuu wa serikali wanapokuwa ni matajiri kuliko serikali yao, basi hapo ndipo kinapoinuka kitendawili cha uongozi bora. <br />
<br />
Mawaziri walio matajiri, wakuu wa mikoa walio tajiri, makatibu wakuu walio tajiri, na wabunge walio tajiri, je, wamefanya biashara gani madarakani hadi wakaupata utajiri walio nao? Kisha je wameulipia kodi ya mapato? Maana inaonyesha kwa utajiri wao basi wanavyo vyanzo vya uhakika vya mapato na kwa kuwa katika nchi yetu kuna sera ya kutoza kodi ya mapato (wakati mwingine hata kabla ya mtu hajapata) basi na wao watoe mchanganuo wao kuthibitisha kwamba nao ni raia wema wanaoilipa serikali mapato sawa na sheria za nchi zinavyoagiza!! <br />
<br />
Kitendawili hiki ni kigumu kuteguliwa ingawa jibu lake liko wazi, kitendawili chenyewe ni kwamba hapa kuna nchi yenye rasilimali za kila namna lakini bado nchi hiyo ni maskini ya kupindukia duniani, nchi hiyo ilipotawaliwa na Wakoloni haikuwa maskini kama ilivyotawaliwa na watawala waliopo sasa, wakati nchi ni maskini, na watu ni maskini mno. Viongozi ni matajiri wa kupindukia. Je kuna mchezo gani umechezwa kuyaleta haya? Jibu wanalo wenyewe watawala, wanajua jinsi walivyofanya hata kuupata utajiri walio nao sasa isipokuwa wanajifanya hawajui wafanye nini ili kuondoa umaskini kwa nchi yao na watu wao, kwa kuwa akili yao imeishia kujitajirisha wao na siyo nchi. Vijana wapatao laki nne wanamaliza elimu ya msingi kila mwaka lakini uongozi uliopo madarakani haujui ufanye nini au uwapeleke wapi,hivyo baada ya kutoka darasani wanaishia "vijiweni".<br />
<br />
Viwanda vingi vimekufa, na mashirika ya umma mengi yameanguka waliokuwa wafanyakazi nao inabidi waungane kwenye vijiwe na vijana wao wanaotoka darasani hadi vijiweni. Kutokana kukosekana sera ya uhakika ya kilimo, kilimo kimebaki duni toka enzi za Mwalimu Nyerere hadi sasa na kwa uduni huo.Kilimo kimejiunga kwenye siasa na kutengenezewa majina mazuri ya kisiasa kama ‘’KILIMO KWANZA’’ wakati uhalisia sio huo. Tumebaki kudanganyana tu ili mradi siku iende. Hakuna elimu ya kuwaelimisha wananchi hasa vijana wajue umuhimu wa kilimo. Mikopo ya Kikwete inatolewa kwa wafanyabiashara badala ya wakulima, na wafanyabiashara wenyewe sio wahitaji halisi wa mikopo hiyo kwania tayari walishakuwa na mitaji ya kutosha. Wakulima wanaachwa kama walivyo, vijana wanaona kilimo kama hakiwezekani kwani hakiwaondoi katika dimbwi la umasikini wa kutupwa. Wakulima hawapendelewi wala hawajengewi mazingira mazuri ya kufanya shughuli zao kama wanavyofanyiwa wafanyabiashara, hivyo vijana wanaona ni bora kufanya biashara ili wajiingize kwenye mazingira mazuri kuliko kiliko kulimo. Kizazi kipya cha vijana wanakimbia kilimo vijijini na kuja mjini kubahatisha maisha mapya. Wale vijana wanaozaliwa mijini, wao wanakimbilia majuu (wanazamia meli), kizazi cha kale cha wakulima kinazeeka na kudhoofu na hakuna wa kuziba pengo, hivyo usemi wa kwamba Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi umebaki kauli za maandishi tu, lakini katika uhalisi wa mambo Tanzania haina wakulima ndiyo maana ni nchi inayoumwa njaa kila mwaka. Pia Tanzania si nchi ya wafanyakazi maana hakuna kazi nyingi za kufanya kwa sababu hakuna viwanda wala makampuni au mashirika ya kutoa ajira.<br />
<br />
Yale yaliyokuwepo yameuawa na watawala waliopo madarakani. Sasa inabidi wote wenye kutazama mambo katika umakini wajiulize nchi ambayo imepukutisha maelfu ya askari wake toka jeshini baada ya kulazimishwa na sera za IMF za kuwa na jeshi dogo, na hivyo kuwalazimisha askari hao kujiunga na walalahoi wengine vijiweni, nchi ambayo imeua mfumo wake wa elimu na kuwafanya vijana wake wasipate elimu ya kuwasaidia kuishi badala yake vijana wake wakawa na elimu ya nadharia ambayo baada ya mtu kumaliza shule (kutoka darasani) anashindwa kuitumia (to apply) aidha hapo kijijini au mjini, mwisho anaishia kijiweni kuvuta bangi au kulamba unga. Ndio vijana hawa wanalaghaiwa na wafanyabiashara wakubwa kujiingiza katika biashara haramu.<br />
<br />
Nchi ambayo inashindwa kuzalisha kizazi kipya cha wakulima na waliopo inawaacha wawe wachovu zaidi kwa kuvuruga mfumo wa masoko ya mazao yao na kuwasababishia umaskini usiomithilika, nchi ambayo haina mpango wowote wa kuongeza ajira kwa maelfu ya wananchi wake, nchi ambayo imeua mfumo wa utoaji haki na kusababisha magereza kufurika wafungwa na mahabusu, nchi ambayo haina mikakati yoyote ya kuwatumia wafungwa kuzalisha mali ili kujikimu wawapo magerezani badala ya kutegemea pesa kutoka serikalini, na mahakama zake kuwa na mafuriko ya kesi za jinai. Je nchi ya namna hiyo ina uhakika gani wa kudumisha amani yake wakati inayaacha mabomu yanayongojea wakati wake ufike yalipuke? <br />
<br />
Kwa hakika nchi yetu ni mfano wa mtu anayetembea sambamba na gema ambaye kuna uwezekano wa kutumbukia wakati wowote. Hata hivyo ieleweke wazi kwamba tatizo la umaskini ni matokeo tu ya uzembe wa watawala, endapo nchi itapata utawala ulio makini na ulio dhamiria kuondoa tatizo hili, umaskini wa Tanzania unaweza kufutika baada ya muda mfupi na Tanzania ikawa miongoni mwa nchi tajiri na zenye uchumi imara au "economic giant" katika dunia hii. <br />
<br />
Mtu hawezi kuamini akielezwa kwamba umaskini wa Tanzania ni sera ya makusudi kabisa ambayo lengo lake kuu ni kudhibiti wananchi na kuwawezesha watawala kuendelea kudumu madarakani hadi siku ya kufa. Watawala wa nchi hii wanajua wazi kwamba wakiwaondoa watu wao katika dimbwi la umasikini hawawezi kutawalika na pia hawawezi kuburuzwa, kwa hiyo umaskini ni silaha yao nzuri ya kuendelea kutawala. <br />
<br />
Fikiria kama Watanzania wangekuwa na elimu, shibe, na utajiri, ni wazi kwamba asingekuweko mgombea yeyote wa ubunge, urais, au udiwani wa kuhonga watu soda, pilau, khanga au pombe za kienyeji. Pasingekuweko na mtu wa kuuza shahada yake ya kupigia kura kwa Tshs: 2,000. Hapo ndipo yangekuweko mashindano ya sera na programu za kuendeleza nchi, majimbo, maeneo, au mitaa. <br />
<br />
Kwa ajili hiyo umaskini kama ulivyo katika nchi hii ni kikwazo cha mengi, ni kikwazo dhidi ya demokrasia, ni kikwazo dhidi ya utawala bora kutokana na ukweli kwamba wezi wa mali za umma na walaji rushwa na mafisadi ndio wenye tabia za kuwanunua wapiga kura walio hoi kwa njaa na umaskini wa kupindukia. Pia umaskini ni kikwazo dhidi ya mabadiliko yoyote.<br />
<br />
Sasa kwa bahati mbaya tatizo la umaskini haliwezi kuondoshwa na utawala unaoona kwamba kuwatawala watu masikini ni raha zaidi kuliko kuwatawala watu walioridhika kimaisha, wakoloni walijitahidi kuwagawa wananchi ili wabaki hawaelewani kati ya walionacho na wasionacho, waliosoma na wasiosoma ili wapate kinga ya kuwafanya waendelee kutawala bila shida. Wao walihakikisha wananchi wanaowatawala wanabaki wajinga. Wagonjwa, na maskini ili wasiwe na ubavu wa kuwaondoa madarakani. Cha kushangaza ni kwamba takribani miaka 48 (2009-1961) tangu tupate uhuru wetu kutoka kwa Mwingereza watawala wetu bado wanaendeleza mbinu za wakoloni za kutawala za kutufanya tuwe wajinga, masikini na tunaosumbuliwa na magonjwa kila wakati.<br />
<br />
Kwa mfano Maasi ya Maji Maji 1905-1907 yalifanya Mjerumani kuyaelewa makabila ya kusini kwamba ni ya watu jeuri na wagumu kutawalika endapo wataachiwa kutulia pasipo kuvurugwa na njaa, umaskini au magonjwa alichokifanya ni kutokupeleka maendeleo makubwa kama vile reli, shule, na mahospitali makubwa. Serikali ya TANU pia ilifuata nyayo za Mjerumani, ilijua wazi kwamba watu wa kusini, Wangoni, Wapangwa, wamatengo, Wamakua, Wamwera, Wanyasa, Wamakonde, Wayao, na Warufiji kwa asili yao ni watu jeuri na wagumu kuburuzwa endapo wataachiwa wawe na uimara wowote ule aidha uimara wa kiuchumi, au uimara wa kielimu au uimara wa kuwa na mshikamano, hivyo basi sera ya ‘’gawanya utawale’’ ikabidi iendelezwe na juu ya hiyo iongezwe sera ya kuwafanya wawe maskini zaidi na pia kuwatenga ama kuwabomolea misingi yote ya maendeleo kwani kama wangekuwa na maendeleo walau nusu tu ya yale yaliyoko kaskazini ingekuwa vigumu kutawalika. Kwa hiyo kwa makusudi kabisa reli ya TAZARA ambayo kimsingi ingekuwa kama ilivyo reli ya kati kwa mikoa ya kusini ikapitishwa porini badala ya kupita Rufiji, Mtwara,Lindi, Songea hadi Itungi Port (Kyela) na kuingia Zambia. Reli ilikwepeshwa maeneo hayo ili tu kuzuia kasi ya maendeleo ya kusini na pia kuzuia kukua kwa uchumi wa kusini. <br />
<br />
Kusini ambayo ina rasilimali nyingi na utajiri mwingi kuliko kaskazini na pengine maeneo mengine yote ya nchi hii sasa imekuwa chemi chemi ya kutoa Wamachinga kwa sababu tu watoto wake wamenyimwa elimu. Rasilimali zake zinaoza na huenda siku za usoni watapewa wageni kama ilivyotokea kwa SongoSongo na machimbo ya Alexandrite huko Tunduru. <br />
Baadhi ya wasomi wachache wa kusini walipewa nyadhifa katika serikali ili ziwe kama takrima na uchawi wa kuloga akili zao wasijejali tena maendeleo ya kusini wala kuwahurumia ndugu zao ambao wanahitaji ukombozi kwa njia ya maendeleo. <br />
<br />
<strong><span style="color: #351c75;">Niandikie:</span></strong><br />
<span style="color: #351c75;"><br />
</span><br />
<strong><span style="color: #351c75;">kyelacommunity@live.com</span></strong>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-36100241870817477272009-11-20T15:33:00.000+03:002009-11-20T15:33:06.433+03:00WANUFAIKA, WAATHIRIKA NA WANUSURIKA WA MFUMO WA UTAWALA WA KIFISADINa. M. M. Mwanakijiji <br />
<br />
Katika sehemu ya kwanza tuliangalia kwa ujumla kuwa utawala wa kifisadi unaonekana katika maeneo makubwa matatu yaani kisheria, kiuchumi na kisiasa. Tukatambua kwamba ili utawala wa aina hiyo ufanikiwa ni lazima upenye katika maeneo hayo matatu na mabadiliko yoyote ya kuumomonyoa utawala huo ni lazima yalenge kugusa maeneo hayo matatu. Tumeuangalia kwa nje utawala huo na pole pole katika sehemu hii ya pili tujaribu kuangalia utawala huo kwa karibu na kuangalia ni vitu gani hasa vinaustawisha utawala huo kiasi cha kuweza kutengeneza mfumo unaofanya kazi na watu wakaishi ndani yake na kukubali kama namna ya maisha yao (lifestyle). <br />
<br />
<em>Mfumo wa utawala wa kifisadi hausimami hewani na hautokei kama ukungu asubuhi au umande</em> <em>wa alfajiri.</em> Ufisadi hujengwa na kutengenezwa pole pole katika jamii kwa kuanzia katika sehemu au maeneo madogomadogo na pole pole kuanza kupenya kwenye maeneo mbalimbali ya maisha na kuwa ni sehemu ya utamaduni na hatimaye kuwa mfumo uliorasmishwa de facto. <br />
<br />
Ufisadi (mfumo) hujengwa na WATU. <br />
<br />
Kama nilivyosema hapo juu ufisadi hautokei hivi hivi tu na hatuwezi kumsingizia shetani; ufisadi hujengwa, hupaliliwa, na kulelewa na watu. Lakini siyo watu hivi hivi tu bali kuna mazingira yanayowatengenezea watu hao sababu ya kuanza kujihusisha na vitendo vya kifisadi na matokeo yake kuanza kujenga utamaduni wa kifisadi ambao huanza kuchimbwa na kusimikwa taratibu katika sheria, siasa na katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kimaisha kijumla. <br />
<br />
Katika mfumo huu wa kifisadi watu hugawanyika katika matabaka kama ilivyo katika mifumo mingine ya kimaisha iliyopo duniani. Kwenye utumwa wapo mabwana na watumwa; kwenye ubepari wapo manyonyaji na wanyonywaji, n.k Kwenye ufisadi kuna matabaka makubwa matatu ambayo yanaingiliana na kuhusiana kila siku na hivyo kuendelea kufanikisha kwa namna ya kila mmoja wao kudumisha na kukoleza mfumo huu dhalimu wa utawala wa kifisadi. <br />
<br />
Makundi hayo ni <strong>Wanufaika, Waathirika na Wanusurika</strong> wa ufisadi. Na ndani ya kila kundi kuna makundi madogo madogo ambayo ndiyo yanaunda kundi hilo kubwa. <br />
<br />
<strong>WANUFAIKA WA UFISADI</strong> <br />
<br />
Kundi hili linajumuisha watu wote ambao moja kwa moja (directly) wananufaika na uwepo wa mfumo wa kifisadi. Kama tukitumia mfano wa shamba, basi wanufaika ni wale wakulima waliolima shamba la ufisadi ambamo ndani yake wakapanda mazao mbalimbali. Ni wao ndio huvuna na kunufaika moja kwa moja na mavuno ya matunda ya shamba lao. Siyo tu wao ni wamiliki wa shamba hilo, bali ndio wakulima, wavunaji na walaji wa kwanza wa matunda ya ufisadi. Kundi hili linajumuisha makundi madogo mawili. <br />
<br />
<strong>WANAONUFAIKA MOJA KWA MOJA</strong> <br />
<strong></strong><br />
<strong>a. watawala serikalini</strong> <br />
<br />
Hawa ni wale wanaosimama kama wenye madaraka serikalini; ni viongozi wa ngazi za juu katika nafasi mbalimbali kuanzia Ikulu, Mahakama, Majeshi, vyombo vingine vya usalama, n.k Tunapozungumzia watawala hatuzungumzii wafanyakazi wa serikali au maafisa wa ngazi za chini; la hasha! Tunazungumzia kundi lile la watu wenye uamuzi juu ya maisha yetu, sera gani tufuate, tutozwe kodi kiasi gani na tusipolipa tuadhibiweje; hela zetu ziende wapi na kwanini, ni wale wenye uamuzi kwa kweli juu ya hatima ya maisha ya mtu mmoja mmoja kama vile wana uamuzi wa mwisho juu ya maisha ya jamii nzima. <br />
<br />
Nilipoliingiza hili neno “watawala wetu” sikuwa namaanisha ni watawala wetu “kisiasa” kama ambavyo tumekuwa tukiwaita zamani tukimaanisha “viongozi” bali ni watawala wetu wa jumla ya maisha yetu. Ni wao ndio wanatuamulia barabara gani zijengwe, shule zetu ziweje, mwekezaji gani apewe nini na kwa muda gani. Hili ndilo kundi la kwanza la wanufaika wa ufisadi. Ukifikiria sana utaona kuwa hawa ndio watu wana nguvu zaidi katika maisha yako kuliko hata familia yako au wale unaowapenda; na yawezekana tunawaona au kuwadhania kuwa wana nguvu kuliko Mungu. <br />
<br />
Hawa Watawala wametujaza fikra za kujiona duni na tusiojua kiasi kwamba wametengeneza utegemezi mbaya wa kifikra juu yao. Ndani yetu tumejawa fikra ya “serikali” kama dudu fulani lenye kumiliki maisha yetu na lenye kuamua matokeo ya maisha yetu; dudu hili serikali basi “likisema” au likifanya jambo basi watawaliwa hawana budi kukubali kwani kupinga kokote kule kutaambatana na matokeo mabaya. <br />
<br />
Ni roho hii ya kujiamini iliyosababisha kwa muda mrefu watu kukubali maelezo na visingizio vya “serikali” pale ambapo mambo hayaendi sawasawa. Ikafikia mpaka mahali watu walishindwa kuhoji zaidi. Watawala wakapewa ufunguo wa maisha yetu kiasi kwamba katika upotovu wa fikra zao walikuwa ni kama wakoloni tuliowakataa; wakitukebehi hadharani, wakitutukana kama watoto wadogo na wengine hata kutuzaba vibao utadhani vile vya “kelbu” vya mbwa. <br />
<br />
Watawala ndio wanufaikaji wa kwanza wa mfumo huu wa kifisadi na kutokana na hilo haiwezekani kwa wao kuubomoa au kuuvunja vunja mfumo unaowahakikishia uwepo wao usiokoma na chakula chao na cha watoto wao. Tukielewa ukweli huu tutambue ni kwanini kundi la wanufaika wa ufisadi walioko serikalini siyo wa kuwategemea kuutokomeza mfumo wa ufisadi. Hawawezi kukata tawi wanalokalia. <br />
<br />
<strong>b. Chama tawala</strong> <br />
<strong><br />
</strong>Katika mfumo wa ufisadi mahali popote duniani ni chama tawala kilichounda serikali ndiye pia mnufaika wa kwanza na wa moja kwa moja wa mfumo wa utawala wa kifisadi. Ukweli huu ulionekana Mexico chini ya Utawala wa Chama cha Mapinduzi cha Mexico kwa karibu miaka 70, na ni ukweli unaonekana huko Syria chini ya utawala wa Baath, na ndio ulionekana kwa muda mrefu katika utawala wa Kikomunisti wa Shirikisho la Kisovieti la Urusi. Ni ukweli pia ulionekana kwa miongo karibu minne ya utawala wa chama cha Baath cha Iraq chini ya Sadam Hussein. <br />
</strong><br />
Katika mfumo huo wa utawala wa kifisadi mafanikio ya mtu au kikundi cha watu yanahusishwa moja kwa moja na uwepo wao au ushiriki wao katika chama tawala. Kwa wao hao chama tawala ndio mlango rahisi, wa haraka na wa uhakika wa kuwahakikishia mafanikio yao na usalama wa maisha na mali yao. Hivyo, chama tawala katika utawala wa kifisadi hutukuzwa kuliko Bunge, Mahakama, au Urais; chama tawala kiko juu ya vyombo vingine vinavyofanya kazi katika nchi ya utawala wa sheria na demokrasia. <br />
<br />
Hivyo, katika mfumo huo wa kifisadia wanachama waandamizi wa chama tawala ndio wanaonesha mafanikio ya mfumo huo. Hawa ndio wabebaji wa kwanza na watetezi wa sera mbalimbali za chama chao na hivyo zawadi ya utii na kujitoa kwao kukitetea chama chao huzaa zawadi ya mafanikio katika mambo mbalimbali. Utawakuta ndio wao wabia wakuu katika makampuni mbalimbali, wananunua viwanja vya ujenzi kwa njia rahisi kuliko mtu mwingine, wanapata taarifa za ndani za mambo mbalimbali yenye manufaa katika biashara zao na hupewa kipaumbele wao na watoto wao (wakati mwingine hata wajukuu) katika nafasi mbalimbali za mafanikio. <br />
<br />
Ukitaka kujua kama kweli mfumo wa kifisadi unanufaisha chama tawala, angalia wanachama wake wakuu wana mafanikio gani na jinsi gani wamepata mafanikio hayo, halafu sogea pande zote nne za huyo mwanasiasa na uone jinsi gani watu wa karibu yake nao walivyofanikiwa. <br />
<br />
Katika Tanzania basi mfumo huu unanufaisha chama tawala; CCM. Mtu yoyote akitaka kunufaika na kufanikiwa pasipo shaka au kuvutia udadisi usio wa lazima ni lazima ahusiane kwa namna moja au nyingine na Chama cha Mapinduzi. Ukitaka mambo yako “yakunyokee” jiunge nacho; ukitaka usisumbuliwe sana naserikali yake toa michango ya hapa na pale; ukitaka ukumbukwe katika “ufalme” wao hakikisha hukosi unapoitwa na wakubwa wake. <br />
<br />
Ukitaka wakutambue uwepo wako jioneshe kuwa ni “mkereketwa”. Nunua nguo kadhaa (na kofia) za kijani na manjano; wakishangilia “CCM, CCM” hakikisha sauti yako ni ya juu zaidi; hata kama unajua kuna madudu ndani ya chama hakikisha “hukichafui” chama bali laumu watu wengine na vitu vingine nje ya chama na ukitetea chama kwa mujibu wa Ibara ya 15:1 ya Katiba ya CCM. <br />
<br />
Ukifanya hivyo na kujionesha mapenzi yako yasiyo na shaka kwa CCM basi jiandae kwa neema; jiandae kwa “wema na fadhili” kutoka CCM. Utafanya mambo yako kwa uhakika, utaendesha biashara zako bila kubughudhiwa sana, utawaona na kukutana na vigogo ambao watakufungulia milango ya ajabu ilimradi tu uendelee kutukuza chama tawala. <br />
<br />
Na katika hilo utaona kuwa CCM itaendelea kutimiza lengo lake la kushinda uchaguzi na kushika serikali. Wataendelea kutunga na kusimamia sheria ambazo zinawahakikishia kuwa wao ndio watawala milele; hawatabadilisha muundo wa tume ya Uchaguzi ili iwe huru zaidi; hawatabadilisha sheria ya uchaguzi ili kuhakikisha nafasi sawa kwa vyama vyote, hawataruhusu wagombea binafsi, na kwa hakika kabisa watahakikisha kuwa Bunge halipati nguvu ya kuweza kutishia uwepo wa serikali yao madarakani. Itatengeneza mbinu na mikakati ya kushinda chaguzi mbalimbali, haijalishi wanafanya vipi au kwa namna gani. Watashirikiana na watumishi walioko serikalini katika kuhakikisha kuwa mambo yanakuwa vizuri. Mtumishi yoyote atakayejaribu kuonekana yuko huru au anataka kutoipendelea CCM atapewa onyo lisilo na utata naye atanywea kama jani la mgomba lililokatwa na kutupwa nje katika jua la kiangazi. <br />
<br />
<strong>WANAONUFAIKA KWA NJIA NYINGINE</strong> <br />
<br />
Katika mfumo huu wapo wanufaika wengine wa ufisadi ambao kwao mfumo huu unawahakikishia maisha yao na hivyo hawana maslahi ya kuubomoa au kuuvunja vunja. Ni wanufaikaji wa pili wa mfumo wa utawala wa kifisadi na maslahi yao yamefungamana moja kwa moja na uwepo wa mfumo wa utawala wa kifisadi (MUK). Wanufaika hawa wa MUK ndio kwa namna moja wanachochea sana uwepo wa mfumo huu na ni kama mbolea ya kuurutubisha mfumo huo. <br />
<br />
<strong>a. Wawekezaji wa Kimataifa </strong><br />
<br />
Hawa hujionesha kwa kuingiza makampuni ya kibepari ya kimataifa ambayo lengo lake kubwa ni kuchota raslimali kwa ajili ya makampuni yao mama huko kwao. Hawa hawaji kwenye nchi yoyote kirahisi rahisi; wanakuja baada ya kuhakikishiwa mambo kadhaa ambayo hutumika kama chambo cha kuyavutia makampuni haya. Mambo hayo katika Tanzania yamepewa jina la “mazingira ya kuvutia wawekezaji wa kimataifa”. <br />
<br />
Sasa mazingira tunayowatengenezea hawa wawekezaji ambao miongoni mwao ni makuwadi wa ufisadi wa kimataifa ni yale ya kuwakaribisha kwenye raslimali zetu muhimu zaidi hasa madini, mafuta, maliasili na fedha. Ili waweze kuingia katika nchi kama ya kwetu tunatakiwa kufungua milango yetu, kuwahakikishia mambo kadha kadha wa kadha kama kusafirisha kwa asilimia mia moja faida wanayopata nchini, kutatua migogoro ya kibiashara katika nchi zao, uwezo wao wa kuajiri watu wa kwao hata katika nafasi kama za kwetu, na kuwahakikishia kuwa ije mvua au jua hatutataifisha au kuingilia kazi za makampuni yao nchini. Na wakati mwingine (kama walivyofanya Bulyanhulu, Buzwagi, Tarime, na sasa Loliondo-kama ilivyokuwa miaka ya tisini) wanataka tuwahakikishie kuwa tuko tayari kuwatimua wananchi wetu (kama nitakavyoonesha hapa chini) kutoka katika ardhi yao ili “kuwapisha wawekezaji”. <br />
<br />
Hawa wanapoanza kuzalisha watatumia kila mwanya kutorosha mabilioni ya utajiri wa urithi wa watoto wetu kwenda kwenye nchi zao kujenga maisha ya watu wao kama walivyofanya wakati wa Ukoloni na wakati wa Utumwa. Kama vile makampuni ya watawala wa Kikoloni leo hii makampuni ya kimataifa kutoka kwa nchi zilizoendelea yanaendelea kufanya kitu kile kile nacho ni kupenya katika nchi maskini, kuwaahidi mbingu lakini kuwaacha wakiwa jehanamu. <br />
<br />
Nchi yenye kutegemea MUK imejiambia katika fikra zake na kuamini kwa dhati kabisa kuwa bila ya kulegeza masharti na kufungua mlango kwa hawa wawekezaji basi nchi haiendi. Hivyo, kwa jina la “ubinafsishaji” Tanzania ikafungua mlango wake kwenye TTCL, Tanesco, Buhemba, NBC, Dawasco, ATCL, TRL, n.k na kuwakaribisha wageni kuendesha nchi kwa namna ya kushangaza. Na watawala wakithibitisha kuwa wao ni watumishi wazuri wa ufisadi hawafikirii njia nyingine ya kutatua matatizo haya isipokuwa kuendelea kupiga magoti mbele ya mafisadi wa kimataifa kama machangudoa mbele ya wateja wao. <br />
<br />
<strong>b. Wafanyabiashara wakubwa</strong> <br />
<br />
Wanufaika wengine wa MUK ni wafanyabiashara wakubwa ambao katika mazingira ya mfumo huu faida yao inahakikishwa. Wafanyabiashara hawa ndio ambao kwa kiasi kikubwa hujijengea utajiri mkubwa na wa haraka haraka wakiwa na uhakika wa usalama wao na wa mali zao. Wafanyabiashara wa aina hii kama wangekuwa na uwezo wangetaka nchi isiwe na sheria yoyote na vitu kama kodi, sheria za mazingira, haki za wafanyakazi n.k zisingekuwepo na wao wangeruhusiwa kufanya wanalotaka. <br />
<br />
Lakini kutokana na kuelewa kuwa ufisadi ndio utawala wenyewe basi wafanyabiashara wa aina hii wanatumia mapengo mbalimbali ya kiutawala na kiungozi ambayo yamejitokeza kwa wao kupanua biashara zao mbalimbali na hata kujenga himaya za biashara. <br />
<br />
Wanaponogewa na hili utaona kuwa wafanyabiashara hawa wanataka kunufaika mara mbili na hapo hujiingiza kwenye siasa na kuanza pia kushiriki katika kutunga sheria na kusimamia sheria ambazo zinagusa biashara zao. Matokeo yake utakuta wafanyabiashara wamegeuka wanasiasa na katika kofia zao mbili hizo wanauwezo wa kujua na kufanya lolote. <br />
<br />
Ni kwa sababu hiyo basi utaona kuwa mahali penye MUK wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa wamefungamana sana kama chanda na pete na wanategemeana sana kama vile mti na matawi yake. Mtu yeyote ambaye atajaribu kupendekeza mabadiliko yoyote yale atapata mapingamizi makubwa toka kwa wanasiasa na wafanyabiashara wa aina hii. <br />
<br />
Ili kutuliza munkari wa watu wafanyabiashara hawa hujikuta wakimwaga misaada ya hapa na pale ili kupunguza maumivu kwa watu (hasa waathirika). Katika biashara zao watatumia mazingaombwe ya hapa na pale kuendelea kuvutia wateja huku wakichuma faida ambayo ikiangaliwa kwa karibu utaona ni kama kufuru. Lengo lao ni kutengeneza jina jema mbele ya jamii. Lakini hawa hawatapigia kelele mabadiliko ya kiutendaji au kisiasa kwani yaliyopo yanawafaa sana. <br />
<br />
Katika MUK wafanyabiashara wakubwa hutengeneza utajiri wa kutisha kwa njia za mchoromchoro, ukwepaji kodi, uvunjaji mbalimbali wa sheria na wanayafanya yote haya wakati mwingine kwa kushirikiana na makuwadi wa ufisadi wa kimataifa (wawekezaji uchwara). Hawa wanasukumwa (kama mabepari wengine) na lengo la kupata faida kwa njia yoyote ile (by any means necessary). <br />
<br />
Hata hivyo kundi la wanufaika wa mfumo wa utawala wa kifisadi mahali pote duniani ni dogo sana ukilinganisha na idadi ya watu katika nchi hiyo. Mara zote ni kikundi cha watu wachache lakini chenye nguvu kubwa ya kiuchumi, kisiasa na madaraka. <br />
<br />
Vile vile lipo kundi la wanufaika wa mfumo wa ufisadi ambao naweza kuwaita ni machangudoa wa ufisadi. Hawa nimeandika makala inayojitegemea juu yao. <br />
<br />
<strong>WAATHIRIKA WA MFUMO WA UTAWALA WA KIFISADI</strong> <br />
<br />
Pamoja na wanufaika wa ufisadi, katika mfumo huu dhalimu wapo waathirika wa mfumo wa ufisadi. Hawa ni wale ambao kutokana na uwepo wa mfumo wa ufisadi wanajikuta wakinyanyaswa katika nchi yao, wakipata kibarua cha ziada kupata nafasi ya kufanikiwa na mara zote huishi kama wahamiaji au wapangaji ambao hutegemea mara zote kupiga magoti na kuomba omba mbele ya wanufaika wa mfumo huu. <br />
<br />
Kundi hili mara zote huombea wale wanufaika wa ufisadi watawakumbuka na kuwasaidia au kuwarahisishia kwa namna fulani kupata nafasi ya wao nao kufanikiwa. Kundi hili katika nchi zote duniani ni kubwa zaidi na huundwa na watawaliwa. Hawa ni ndio watu wengi zaidi katika nchi. Tuangalie baadhi ya makundi yanayojikuta yakiathirika katika mfumo huu wa kifisadi. <br />
<br />
<strong>1. WAKULIMA</strong> <br />
<br />
Hakuna waathirika wakubwa zaidi wa mfumo wa kifisadi kama wakulima. Hawa ambao ni wengi wanajikuta wanakabiliwa na athari kubwa za ufisadi kwa sababu kubwa tatu. Kwanza, bado wanatumia pembejeo na nguvu kazi ya kijima. Hutumia nguvu nyingi kuzalisha kitu kidogo na wengi wao bado hulima kilimo cha kujikimu (subsistence farming) na ni kile kidogo cha ziada ndio hutegemea kwa mauzo. Pili, wengi wao wako vijijini ambako miundo mbinu ya uhakika bado ni ya kijima. Bado wakulima wetu husafiri umbali mrefu, hutumia muda mwingi, na huhenyeka katika kuhakikisha kuwa mazao yao yana ubora na hatimaye kumfikia mlaji au mnunuzi. Tatu, wakulima wetu wengi bado hawana ufahamu na uelewa wa mahusiano mbalimbali ya siasa, uchumi, maisha, na kilimo chao. Bado wanawategemea wanasiasa kuwaambia nini cha kufanya na jinsi gani ya kukifanya. Matokeo yake wamekuwa wakijikuta wakirubuniwa, kuzugwa na mara kadha wa kadha kuvutiwa na maneno matamu na ahadi hewa. <br />
<br />
Mahali pote duniani ambapo mfumo wa kifisadi umekomaa, wakulima hulisha mafisadi na huhimizwa kuzalisha zaidi lakini wakati huo huo kuwekwa nje ya mduara wa madaraka. Huombwa kura zao kila chaguzi zikifika, na husauliwa hadi uchaguzi mwingine. Hawana nafasi ya kubadilisha mwelekeo wa siasa zao kwani hufanywa duni na watawala na kuoneshwa kuwa wao ni “washamba”. Tumefika mahali ukulima umekuwa ni kama kazi ya fedheha na aibu kiasi kwamba vijana wetu wengi sasa na hata watu wazima hujaribu kutafuta sababu ya kuachana na kilimo na kukimbilia mijini kutafuta shughuli nyingine mbadala ya kilimo. <br />
<br />
<strong>2. WANAWAKE NA WATOTO</strong> <br />
<br />
Waathirika wa kwanza wa mfumo huu wa kifisadi ni kundi la kina mama na watoto. Kundi hili linabeba athari za moja kwa moja za ufisadi kwanza kutokana na kutokuwa katika nafasi za juu ya madaraka, biashara, na mahali pa kufanya maamuzi ya kubadili mwelekeo wa taifa na pili kutokana na mfumo dume ambao umejenga utamaduni wa manyanyaso dhidi ya wanawake. <br />
<br />
Hatuzungumzii wanawake “wote” kwamba wanapata athari za moja kwa moja kwani wapo wanawake ambao ni sehemu ya wale wanaonufaika na mfumo uliopo sasa; wanawake tunawaozungumzia kwanza ni wale kina mama wa kijijini ambao ndio nguvu kazi kubwa zaidi iliyopo nchini ambayo bado inatumia mbinu na zana za kizamani huku ikiwa imebebeshwa majukumu makubwa ya malezi ya familia. <br />
<br />
Kundi hili halina wasomi wengi, na wale wachache waliopo wanajikuta wanaangukia kwenye kundi la tatu la matabaka yaliyopo kwenye MUK. Hili ni kundi la kina mama na kina dada ambao kutokana na matatizo mbalimbali hawakuweza kupata nafasi ya kuendelea na masomo, walijikuta wakianza maisha ya malezi ya watoto mapema, na wale ambao kutokana na tamaduni na mila za mahali walipo wanajikuta hawana sauti ya maamuzi ya mambo mbalimbali yanayohusu maisha yao. <br />
<br />
Japo kuna juhudi katika Tanzania ya kuwaongezea wanawake nguvu zaidi kama vile uanzishwaji wa vyama vya kukopa (SACCOS), benki ya wanawake, asasi mbalimbali n.k bado tunaweza kuona kuwa nguvu ya maamuzi (power to decide) inabakia mikononi mwa watu wachache ambao wengi wao bado wanaangukia katika kundi la wanufaika wa ufisadi. Kina mama hawa kama ilivyo sehemu nyingine zenye MUK huwa wanatulizwa na vitu mbalimbali vinavyowafanya watulie na wasiwe na muda kupiga kelele ya mabadiliko. <br />
<br />
Athari zinazowakuta kina mama hawa ni ukosefu wa huduma bora na za kina za kijamii na kimaisha, kuendelea kuishi maisha duni ya kutumia muda mrefu wa siku kutafuta kuni, maji, na chakula, na vile vile kufuatilia maisha ya maendeleo ya familia. Kina mama kama hawa hata wale walioko mjini hujikuta hulazimika hata kujidhalilisha na kujifanya duni ili waweze kuokoa maisha ya familia zao na kutoa msaada wa kifamilia. <br />
<br />
Watoto wao wanajikuta wanapata athari za ufisadi kwa sababu vitu vingi ambavyo vingeweza kufanywa na watoto katika kuwaandaa kwa maisha bora vimeachwa kufanywa au kufanywa kiuvivu na kwa uzembe. Nitolee mfano hali ya lishe (nutrition) kwa watoto wetu katika Tanzania katika nchi ambayo ina ubwelele wa nyama, maziwa, samaki, mboga, matunda, na nafaka nyingi tu. <br />
<br />
Takwimu mbalimbali za hivi karibuni (angalia ripoti ya REPOA kuhusu lishe kwenye mwanakijiji.com sehemu ya vielelezo) zinaonesha kuwa asilimia 40 ya watoto wetu chini ya miaka mitano wamedumaa – urefu wao hauendeni na umri wao (stunted) na hiyo ni mojawapo ya ishara ya lishe ya kiwango cha chini; asilimia tatu wana uzito wa chini ukilinganisha na urefu wao – dalili ya utapiamlo wa hali ya juu, na karibu asilimia 22 ya watoto wetu wana uzito wa chini ukilinganisha na umri wao – ambayo ni dalili ya ukosefu wa lishe ya kutosha kwa muda mrefu. Takwimu hizo zinaonyesha pia kuwa kuna tofauti kubwa kati ya lishe ya watoto wa mjini na wa kijijini ambapo asilimia 26 ya watoto wa mjini wanaupungufu wa lishe na wamedumaa wakati kule vijijini ni asilimia 41. <br />
<br />
Wakati haya tunayaangalia utashangaa kuona nchi yetu ina chakula cha kutosha cha kila aina. Miaka ya zamani tulikuwa na kampeni za “mtu ni afya”, “kuleni chakula bora”, n.k na tulifika mahali tukaweza hata kutoa maziwa kwenye shule zetu za chekechekea hata shule za msingi. Leo hii tukiuliza juu ya mlo kwa watoto wetu jibu la haraka litakuwa ni “hatuna fedha” au “tunatafuta wafadhili”. <br />
<br />
Ipo na mifano mingine ya takwimu za afya na masuala mengine ya jamii ambazo zinaonesha jinsi gani watoto wetu wanalipa gharama kubwa ya vitendo vya kifisadi. Matokeo yake huwa tunashangazwa inakuwaje watoto wetu hawafaulu vizuri darasani, na wanafanya vibaya kwenye mitihani tumeshindwa kuoanisha hali ya lishe na ukuaji wa kiakili (cognitive development). Tunafikiri yote haya yanatokea katika ombwe! <br />
<br />
<strong>3. VIJANA</strong> <br />
<br />
Mojawapo ya waathirika wakubwa wa mfumo huu ni vijana. Kundi hili lina vijana wa kati ya miaka 18 na 35 na ambao kutokana na sababu mbalimbali wamekosa nafasi ya kujiendeleza kielimu au kuwa katika mazingira ya kupata mafunzo rasmi na hivyo kulazimika kuishi kwa “kujishughulisha” katika kile ambacho kimebatizwa jina la “ajira zisizo rasmi” a.k.a kubangaiza na kuhangaika. Kundi hili la vijana wanatumia nguvu nyingi ya mwili kufanya vitu ambavyo vingetumia mbinu rahisi au utaalamu rahisi, na wakati mwingine wanajikuta wanatumia nguvu zaidi za misulu kuliko za ubongo katika maisha yao. <br />
<br />
Hawa (ambao wengine utotoni hawakupata milo mizuri) wanajikuta wamekua kimwili lakini kiakili na kifahamu bado ni watu wa kusukumwa na hisia au nawatu wanaojiita “wataalamu”. Kundi hili ni kundi ambalo ni hatari kwenye taifa lolote lenye mfumo wa utawala wa kifisadi. Kundi hili halihitaji kushawishiwa kuona ubovu wa maisha yao; wanaoishi maisha hayo. Kundi hili haliitaji kuhubiriwa juu ya kile kilicho bora; wanakiona kwa wengine. <br />
<br />
Matokeo yake utaona kuwa kundi hili halitoi mchango unaostahili katika kujenga taifa kwani hakuna mtu ambaye anaamini kwa dhati kuwa linamchango; matokeo yake limebakia kuwa ni kundi kubwa lililo nje ya madaraka na nje ya mfumo wa maisha ya kawaida. Mamilioni ya vijana wetu wanajikuta wakizunguka kila kukicha wakitafuta nafasi katika maisha yao. Na mambo yanakuwa mabaya zaidi pale kundi hili linapoanza kuona watawala wanaendelea kujenga mbingu zao hapa hapa duniani huku wao wakiendelea kuwa kituko katika mitaa yao na maeneo yao. <br />
<br />
Baadhi yao hulazimika kuanza kuishi maisha ya kujidhalilisha na uhalifu; wanageukia wizi, ubakaji, na uporaji na wengine hasa kina dada hujiingiza katika biashara ya ngono kama hatua za mwisho za kusalimisha utu wao na hadhi yao kama binadamu. <br />
<br />
Vijana ndio wanabeba uzito mkubwa wa athari ya utawala wa kifisadi kwani ni hawa ambao wanajikuta wamesukumwa nje ya malango ya mafanikio, na kama ombaomba wanalazimika kukinga mikono yao ili kuweza kupata nafasi ya kula matunda ya urithi wa taifa lao. <br />
<br />
<strong>4. WENYE KIPATO NA ELIMU YA CHINI</strong> <br />
<br />
Wananchi wenye kipato cha chini ambao wana elimu duni hujikuta wakiathirika zaidi na ufisadi kwani hawa njozi yao ya maisha ya manufaa na yenye unafuu inabakia katika vichwa vyao lakini isiyotimilika. Hawa hujikuta wakiwa kama abiria wanaoenda uwanja wa ndege kuangalia ndege za walionufaika zikipaa huko wao wameachwa wameduwaa. Hubakia kuambizana tu kuwa “siku moja nikipata nauli na mimi nitaruka”. <br />
<br />
Mfumo wa ufisadi huwatengenezea mazingira ya kuwatuliza kwa kuwapa ajira ndogo ndogo, misaada ya hapa na pale na kuwaahidi mema huko mbeleni. Hawa hujikuta wakiambiwa kila siku na watawala kuwa wafanye kazi “kwa bidii na maarifa” bila ya kujiuliza kuwa ulimwengu wa leo kazi hufanywa kwa akili, utaalamu, na weledi wa hali ya juu na maarifa ambayo hubadilika kila kukicha. Matokeo yake kundi hili hujaribu kujiendeleza kwa fani mbalimbali na ujuzi wa aina tofauti lakini wakiamka asubuhi hujikuta wako katika hali ile ile. <br />
<br />
<strong>WANUSURIKA WA MFUMO WA UFISADI</strong> <br />
<br />
Vile vile lipo kundi la wanusurika wa MUK. Kundi hili linawajumuisha wale wote ambao kutokana na nafasi zao wanajua madhara ya ufisadi, uovu wa mfumo wa kifisadi na wanajua kabisa kuwa nini kinapaswa kufanyika. Kundi hili linawajumuisha watu ambao wanauwezo wa kubadilisha mambo lakini kutokana na kujikuta wakiwa wananufaika vile vile na mfumo huo hujikuta wakifanya kazi ndani yake kwa manung’uniko na kukerwa nao lakini hawawezi kuuacha kwani kwa kufanya hivyo watajikuta kuwa ni waathirika. <br />
<br />
Hawa hawataki kuonekana ni mafisadi na huwabeza mafisadi sirini (siyo hadharani); lakini hawawezi kutoka kwenye mfumo huo wa kifisadi kwani na wao ni wanufaika aidha kutokana na ajira zao, nafasi zao za kisiasa, biashara au mahusiano yao ya karibu na watawala. Wanusurika wa ufisadi ni majeruhi wa mfumo huo lakini wasiopona. Baadhi ya wanusurika wa ufisadi wako katika makundi yafuatayo. <br />
<br />
<strong>1. WATUMISHI WA UMMA</strong> <br />
<br />
Hawa ni watumishi ambao wanauona kila kukicha mfumo wa ufisadi ukifanya kazi; ni wao ndio kwa namna ya pekee wanatumika pasipo matakwa yao kuundeleza mfumo huu. Ni hawa ambao kutokana na nafasi zao hutekeleza maagizo na maelekezo mbalimbali hata wakijua kuwa yana matokeo maovu kwa “waathirika”; badala ya kupinga au kuyafichua mambo hayo hujikuta wakikubali (hata kama kwa shingo upande) kupitisha sera, kutekeleza maamuzi ambayo kwa kweli wanajua mioyoni mwao kuwa si yenye maslahi kwa taifa au kwa wananchi moja kwa moja. <br />
<br />
Ndio hawa ambao tumeona mambo yao kwenye kashfa za BoT, ni hawa tumewaona kwenye kashfa za ATCL, TRL, Tanesco na kwingine. Hawawezi kuachia nafasi zao kwani ukiwauliza watasema “sasa mimi nile wapi?” <br />
<br />
Kwa vile wanajua madudu yanayofanywa na vikaragosi vya ufisadi (mabosi wao) basi hujikuta na wenyewe kutumia nafasi hizo hizo na wao kula. Huandaa visemina uchwara, mikutano ya “tathmini” na kozi za “kujiendeleza” ambazo wakati mwingine hurudiwa kwa jina jingine na kwenye hoteli nyingine. Hujikatia posho za kila namna ilimradi waweza kufuja fedha za umma bila kumuogopa yoyote. <br />
<br />
Lakini ni hawa hawa upande mwingine wanachukizwa na vitendo vya ufisadi mkubwa na ndio wamekuwa wa kwanza vile vile kufichua ufisadi mkubwa katika taasisi zao kwani wanajua kabisa na kwa undani mambo yanayofanywa na makuwadi wa ufisadi wenyewe. Katika mikutano mbalimbali na pembeni hulalamika sana juu ya vitendo vya rushwa na milungula ya aina mbalimbali, lakini wakati huo huo na wenyewe hujikuta kupokea au kukubali vitu hivyo ili “maisha” yaende mbele. Hawa kama ingepatikana jinsi ya kuondoa rushwa na kunufaisha maisha yao kihalali wangeachana na vitendo vya kifisadi kwani baadhi yao wanaporudi nyumbani ni watu wa imani, na maadili lakini wanapokuwa kazini au maofisini hujihusisha na vitendo hivyo kwa kisingizio kuwa “kila mtu anafanya hivyo”. <br />
<br />
<strong>2. VYOMBO VYA HABARI</strong> <br />
<br />
Kama kuna kitu ambacho ninakielewa vizuri sasa hivi zaidi kuliko miaka karibu minne iliyopita ni kuwa vyombo vya habari vinanufaika na ufisadi lakini kwa namna ya kunusurika. Vyombo hivi hujionesha kuwa vinapigana na ufisadi na vinaandika sana habari ya ufisadi; tatizo ni kuwa ili viendelee kuwepo vinategemea mafisadi hao hao! <br />
<br />
Hivyo, utaona baadhi ya magazeti hata ambayo husifiwa kwa kupiga vita ufisadi hutegemea matangazo ya biashara kutoka kwa watawala na wakati mwingine huenda kubembeleza kwa watawala hao hao ili “walete” matangazo kwenye magazeti au vyombo hivyo vya habari. Na watawala wanajua udhaifu huu. Kuna wakati watawala huamua kuvisusia vyombo kadhaa vya habari kwa sababu vinaziandika wizara, idara au vyombo Fulani vibaya na hivyo hawapeleki matangazo yao mbalimbali huko. <br />
<br />
Na cha kusikitisha zaidi ni kuwa watawala wale wale ambao ndio wanufaika wa ufisadi wamekamata vile vile vyombo vya habari huku wengine wakiwa na maslahi ya wazi kabisa katika vyombo hivyo. Hawa huajiri waandishi wa habari kufanya kazi ya habari lakini wakati huo huo hupeleka matangazo ya idara, wizara au serikali kwenye vyombo vyao bila ya kutangaza maslahi (without declaring interest). <br />
<br />
Sasa, utaona kuwa vyombo vya habari vinanufaika pia kwa namna nyingine; kwa kuandika habari kwa hisia na wakati mwingine kwa kama kuchonganisha. Magazeti haya hupata wasomaji wengi wenye hamu na kiu ya kujua mambo mengi. Mfano mzuri wa jinsi gani magazeti yanacheza mchezo huu ni katika sakata la Mengi na Rostam, na suala la Mwakyembe na Mwakipesile, n.k Ni jambo moja kutoa habari na kuburudisha watu lakini ni jambo jingine kabisa kuchochea ugomvi na wakati huo huo kutengeneza fedha. <br />
<br />
Inakuwa kama watu wanaochonganisha watu huku wao wakikaa pembeni kusubiri nani ashinde ili wawe upande wake na waendelee kumchuna. <br />
<br />
Vyombo vimenusurika kwa sababu, baadhi yake vingeweza kuendeshwa kwa biashara ya kuuza magazeti na mambo mengine vingekuwa kweli huru na vingependa kuwa hivyo lakini kutokana na ukweli kuwa bado serikali ndiyo yenye biashara kubwa kwenye vyombo hivyo basi vyombo hivyo vya habari hujikuta vinapiga magozi na kucheza ngoma ya mafisadi. <br />
<br />
<strong>3. TAASISI ZA KIDINI</strong> <br />
<br />
Kwa muda mrefu taasisi za kidini zimeweza kukua na kunufaishwa sana na mfumo wa kifisadi. Nilipoandika barua yangu ya kwanza kwa wachungaji na makala zilizofuatia baadaye zilikuwa na lengo la kuamsha kundi hili ili watoke katika kile nilichokiita wakati ule “kitanda cha ufisadi” ambao viongozi wetu wa dini na wanasiasa wamelala huku wakijifunika blanketi moja. Kwa muda mrefu viongozi wetu wa dini hawakuwa tayari kuunyoshea mkono utawala wa kifisadi zaidi ya kukiri uwepo wa vitendo vya rushwa na uvunjaji wa sheria wa hapa na pale. Lakini wakati huo huo viongozi hao wa dini na taasisi zao walijua kabisa wakitaka baadhi ya mipango na miradi yao ifanikiwe hawana budi kuimba nyimbo za watawala. <br />
<br />
Katika siku za karibuni tumeanza kuona mwamko wa aina yake ambapo viongozi wa dini wakiwa kama watu waliochelewa stesheni ya garimoshi wameanza kudandia mjadala dhidi ya ufisadi kwa namna ya pekee zaidi; kuuita uovu huo kwa jina lake mbele ya watawala. <br />
<br />
Jawabu la watawala tuliliona kwenye jaribio la kujaribu kutishia mapato na shughuli za taasisi hizo za kidini katika mapendekezo ya kufuta misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini isipokuwa kwa mambo ya ibada. Ile ilikuwa ni kama onyo na sitoshangaa huko mbeleni watawala wakaamua kufanya kweli na hivyo kutishia taasisi hizo za dini kukaa pembeni ya mambo ya siasa. <br />
<br />
Pamoja na hilo bado taasisi na viongozi wa kidini hawajaacha kunufaika kwa namna moja au nyingine na mfumo huu wa ufisadi. Ili miradi yao, makanisa, misikiti, mashule na mahospitali yao yafanikiwe na misaada yao isipate shida bandarini ni lazima wawe tayari kula “sahani moja” na watawala. <br />
<br />
Lakini viongozi hawa hawa hujikuta wanalazimishwa na ukweli wa mambo kukemea ufisadi hadharani na kuukataa. Lakini jambo moja ambalo hawawezi kulifanya ni kupambana na ufisadi hadharani; hawatoandamana kupinga mafisadi, hawatokataa kuwapigia magoti watawala, na kamwe katika MUK usitarajie viongozi wa dini kuchukua msimamo mkali unaoambatana na vitendo vya kiupingaji ambavyo vina lengo la kuamsha dhamira ya wananchi. <br />
<br />
Taasisi hizi za kidini nazo zimenusurika na ufisadi lakini pia zinanufaika na uwepo wake. <br />
<br />
<strong>4. ASASI MBALIMBALI</strong> <br />
<br />
Mojawapo ya wanusurika wa ufisadi ni asasi mbalimbali za kijamii. Hizi leo hii zimegeuzwa kuwa mitaji ya kujitengenezea utajiri wa haraka haraka kwa kutumia visingizio vya kutoa misaada au kusaidia jamii. Hivyo, haishangazi kuona kuwa wanufaika wa ufisadi na wao wenyewe wameanzisha asasi zao mbalimbali ambazo zinapokea misaada mbalimbali kama makanisa lakini hizi haziongozwi na imani (japo nyingine ni za kidini); zinaongozwa na kile kinachodhaniwa kuwa ni huruma kwa watu. <br />
<br />
Sizijumuishi asasi zote za makanisa au viongozi wote wa dini na kuwaweka kwenye kundi la wasio wa kweli na wenye malengo zaidi ya yale yaliyomo kwenye asasi zao; nazungumzia wale ambao kama wanasiasa waliopotoka au polisi waliopotoka wamejikuta wakitumia nafasi ya uwepo na ukomavu wa mfumo wa kifisadi kujenga na kujijenga wao wenyewe wakitumia shida na mahangaiko ya watu wengine. <br />
<br />
Hawa huwa na urafiki wa karibu na wanufaika wa ufisadi na utakuta wakijitangaza aidha kupitia makampuni yao au asasi zao wakigawa misaada ya kila aina na kutoa misaada wakati wa sherehe za kidini na matukio mbalimbali. Lengo lao ni kujenga jina “jema” la asasi, mashirika au makampuni yao mbele ya wananchi na mbele ya watawala. Lakini, wakati huo huo wanatumia kila aina ya ujanja kutumia misaada vibaya na kwa maslahi yao wenyewe nje ya yale ya watu wanaosema wako tayari kuwasaidia. <br />
<br />
<strong>NI MFUMO WA HATARI</strong> <br />
<br />
Mfumo huu kwa kila kipimo ni mfumo ambao hatuwezi kuuvumilia, kuuendeleza, wala kuutafutia udhuru wa uwepo wake. Ni mfumo ambao hauna budi kubomolewa na kuvunjwa vunjwa na kutupwa katika shimo la usahaulifu la historia. Ni mfumo ambao hudumaza jamii kubwa huku ukinufaisha kikundi cha watu wachache ambao kutokana na nguvu zao za kisiasa na kiuchumi huharibu hata nafasi ya utawala wa sheria. <br />
<br />
Kimsingi kabisa mfumo huu haupatani (incompatible), hauwezi kupatana sasa na hata milele na utawala wa kidemokrasia hauwezi kushikana na utawala wa sheria na kamwe hauwezi kuwa sehemu moja na jamii ya watu walio huru na sawa. <em>Ni mfumo ambao huinua katika jamii tishio kubwa zaidi la mafanikio ya taifa na wananchi, ukiahidi uongo huku ukibeza ukweli, ukigeuza udhalimu kuwa haki na uonevu kuwa maelewano. <br />
</em>Ukweli huo unanifanya niamini kuwa mfumo huu hauwezi kuvunjwa majukwaani, kwa kusoma magazetini au kwa kulumbana mitaani. Mfumo huu hauwezi kuvunjwa na kuharibiwa kwa kuandika na kujadiliana kwenye mitandao ya intaneti au kwa kutumiana barua pepe kusimuliana kilichojiri. <br />
<br />
Mfumo wa aina hii huangushwa kisayansi na kitaalamu kwa kutumia nguvu za kisiasa na mikakati yenye matokeo mema. Hauwezi kuangushwa kwa kusubiri bahati itokee. Tutaendelea kuangalia mbele katika masomo mengine zaidi ya huu mfumo. <br />
Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-36990117844660343662009-11-19T21:33:00.000+03:002009-11-19T21:33:00.281+03:00Wabunge wamshangaa Rostam• Kimaro asema anaweweseka kutaka Dowans inunuliwe<br /><br />na Deogratius Temba<br /><br />KAULI aliyoitoa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), akiliomba Bunge liunde kamati huru kuchunguza upya sakata la kuhusika kwake na Kampuni ya Richmond Development LLC ili apate nafasi ya kusikilizwa, imewatibua baadhi ya wabunge wa chama chake.<br /><br />Wabunge hao walisema Rostam anaweweseka na kashfa ya Richmond, na kumtaka akasome vizuri kanuni za Bunge ili ajue kwamba suala likishaamuliwa na Bunge, haliwezi kuundiwa tume nyingine nje ya Bunge.<br /><br />Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana katika mahojiano maalum na Tanzania Daima, Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro, James Lembeli (Kahama) na Lucas Selelii (Nzega), walisema Bunge likishahitimisha hoja, haliwezi kurudi nyuma kuijadili upya, na kwamba Rostam anapaswa kufuata kanuni za Bunge.<br /><br />Kimaro alisema hakuna sheria wala kanuni ya Bunge inayotamka kuwa kamati teule ya Bunge ikifanya kazi yake na Bunge likaridhia, inaweza kuundiwa tena kamati nyingine nje ya Bunge.<br />“Bunge limeshamaliza kazi yake, hakuna cha kurudia hapo, wala kanuni za Bunge haziruhusu kufanya vile, nafikiri hajakisoma kitabu cha kanuni za Bunge ndiyo maana anaweweseka, vinginevyo asingesema hayo.<br /><br />“Ninawashauri Watanzania kutojiingiza katika mjadala huo, umeshafungwa na Bunge likatoa mapendekezo yake, na sasa tunaisubiri serikali itekeleze na si mtu mwingine aje tena bungeni kuleta hoja hiyo hiyo, hapana sisi tunapiga hatua nyingine mbele,” alisema.<br /><br />Alisema kama kuna watu hawakuridhika na kazi iliyofanywa na kamati teule ya Bunge iliyokuwa ikiongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, wasifikiri kuwa kuna huruma tena au wakipiga kelele watapata msamaha.<br /><br />“Tena wasifikiri kuwa kwa kupiga kelele vile serikali inaweza kuifikiria tena Dowans, hilo limepita na serikali haitainunua mitambo hiyo kwani hata sheria hairuhusu. Sheria ya umeme ya mwaka 2008, imeeleza waziwazi kuwa kama kuna watu waliohusika kudai ‘capacity charge’ wasipewe nafasi ya kuiuzia TANESCO umeme,” alisema Kimaro.<br /><br />Alidai kuwa, kinachomsumbua Rostam hadi kufikia kuliomba Bunge liunde kamati upya, ni kutaka mitambo ya Dowans inunuliwe.<br /><br />“Mimi ninataka kujua kinachomkera au kinachomfanya aweweseke ni nini? Awaeleze Watanzania waelewe, atumie muda huu kuueleza umma kama ana maslahi gani na Dowans au iliyokuwa Kampuni ya Richmond na si kulitakia Bunge kazi ambayo si yake,” aliongeza Kimaro.<br />Naye Lembeli, alisema Bunge ni kwa ajili ya Watanzania wote na maamuzi yaliyotoka ni ya wote.<br />Alisema Rostam hajaonewa na kamati kwani ilitoa ripoti na wabunge wote wa CCM wakaiunga mkono kwa pamoja, kwa hiyo ilifanya kazi yake.<br /><br />“Tatizo si kuonewa wala kamati teule ya Bunge, Rostam atafute kanuni za Bunge azisome na aelewe zinasemaje, kwanza asiionee kamati, sisi wabunge ndio tuliopitisha ripoti, kama tungeona ina makosa na kubaini kuna mtu ameonewa, tungeikataa.<br /><br />“Anapotumia muda mwingi kudai kuwa iundwe kamati upya, mara jopo la majaji kuchunguza upya, mbona alishajitokeza mara kadhaa kwenye vyombo vya habari akadai kuwa hausiki? Kwani hilo halitoshi? Mbona maelezo anayoyatoa kwenye magazeti kuwa hakuhusika hayaelezi kama alionewa? Na alionewa wapi?” anahoji Lembeli.<br /><br />Akizungumzia suala hilo, Selelii, ambaye alikuwa mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo teule, alisema ndoto za Rostam ni za mchana na hazitekelezeki katika Bunge hili na kwa kutumia kanuni hizi za Bunge zilizopo.<br /><br />“Hizo ni ndoto, tena za mchana, hakuna kitu kama hicho, Bunge lilishafanya kazi yake na kuimaliza, anachokitaka yeye hakiwezekani kwa Bunge la Tanzania, na kama ni kwa Bunge la hapa Tanzania basi si kwa kanuni hizi tulizonazo,” alisema.<br /><br />Alisisitiza kuwa, siku zote mtu anayetuhumiwa kwa kukosa, hawezi kukubali kosa hata kama atachapwa namna gani, kwa hiyo huo ni ujanja ambao unatumika kujinasua na tuhuma hizo.<br />Selelii alimtaka Rostam achukue ripoti ya kamati hiyo, aangalie vipengele vyote vinavyomtaja kuwa anahusika na Richmond na Dowans, halafu aende kwenye hoja bila kuzunguka.<br /><br />“Kama kweli Rostam ana uhakika na hayo malalamiko ambayo anayatoa kila mara na hata kupitia baadhi ya vyombo vya habari, arejee kwenye ripoti yetu ya kamati, asome maeneo yote yanayomgusa na kumhusisha na Richmond na Dowans, halafu ajenge hoja,” alisema Selelii.<br /><br />Hivi karibuni, Rostam alikaririwa na chombo kimoja cha habari akiliomba Bunge liunde jopo la majaji watatu kuchunguza upya sakata hilo ili kutoa hukumu ya haki.<br /><br />Siku chache baada ya Rostam kuomba Bunge liunde jopo hilo la majaji, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, alisisitiza kuwa haiingii akilini, kwa mbunge huyo kutaka uchunguzi wa suala hilo ufanywe na majaji, na juzi mbunge huyo wa Igunga alirejea tena ombi lake la kutaka iundwe tume huru.<br /><br />“Kwanza, labda nikwambie tu, maamuzi yaliyofikiwa na Bunge katika Richmond hayawezi kuchunguzwa upya na mhimili mwingine wowote wa dola.<br /><br />“Tunazungumzia kumaliza suala la Richmond si kuanza upya, kama ana pesa zake (Rostam) za kulipa majaji, ni huko huko, lakini hilo haliwezekani,” alisema Sitta.<br /><br />Alisema ushahidi mbalimbali ulionyesha uhusiano wa mawasiliano ya mbunge huyo na Richmond kisha Dowans.<br /><br />“Hivi mnataka ushahidi upi zaidi? Ushahidi wa mawasiliano ulionyesha jinsi mtu huyu alivyokuwa akiratibu Richmond kisha Dowans,” aliongeza Spika.<br /><br />Rostam, mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, amekuwa akitajwa kama mmoja wa vigogo walioshiriki katika kufanikisha Richmond kupewa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura katika mazingira tata.<br /><br />Mkataba na kampuni hiyo yenye taarifa tata kutoka Costa Rica na Marekani, ulisainiwa na TANESCO Juni 23, 2006.<br /><br />Lakini baada ya kusakamwa kwa muda mrefu, alipopata nafasi katika kikao cha Kamati ya Mzee Mwinyi na wabunge wa CCM, iliripotiwa kuwa Rostam aliongelea kuundwa kwa tume huru kuchunguza kashfa nzima ya Richmond kwa madai ile ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Mwakyembe, ilipotosha.<br /><br />“Ripoti ya Richmond imeidhalilisha serikali kwa maslahi ya kisiasa. Ili mambo yaishe ni vema uchunguzi huru ukafanyika. Tusipofanya hivyo tutaendelea kuwachanganya wananchi.<br /><br />“Msimamo wangu tangu kamati teule ya Bunge itoe taarifa yake bungeni, uko pale pale. Ripoti ilijaa upotoshaji na uongo. Nilitaka kuongea bungeni nikazuiwa,” alisema Rostam.<br /><br />Kamati hiyo teule ilisema katika taarifa yake kuwa, Rostam aliitwa ili aeleze uhusiano wake na Richmond kutokana na kampuni hiyo kutumia anuani ya barua pepe na fax ya Kampuni Caspian na sababu za kuitafutia Richmond kampuni ya ushauri wa mambo ya habari, lakini hakujitokeza.<br /><br />Rostam alijieleza katika mchango wake wa maandishi wakati wa kujadili ripoti ya Richmond kuwa, Kamati ya Mwakyembe ilimuita kumhoji Desemba 24, mwaka jana wakati ikijua kuwa siku hiyo asingeweza kupatikana kwa sababu ya sikukuu.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-74134096595961586532009-11-19T20:46:00.000+03:002009-11-19T20:46:00.524+03:00Ndege ya Rais wa Tanzania<a href="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwTnACGivwI/AAAAAAAAAFo/KUNk5QakYCI/s1600/ndege+ya+rais.jpg"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5405699440501767938" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 573px; CURSOR: hand; HEIGHT: 345px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="http://1.bp.blogspot.com/_D0trN7SXoqg/SwTnACGivwI/AAAAAAAAAFo/KUNk5QakYCI/s400/ndege+ya+rais.jpg" border="0" /></a><br /><div align="center"><span style="color:#6600cc;"><strong>Ndege ya Rais aina ya Gulfstream 550 </strong></span></div><br />Hizi ndio details za gulf stream 550,<br />Developing nation:<br />United States of America<br />Manufacturer/designer:<br />Gulfstream Aerospace Corporation.<br />Production line:<br />Savannah, GA USA.<br />Type aircraft:<br />long-range business jet .<br />First flight:<br />August 31, 2001.<br />First delivery:<br />2003.<br />Gulfstream G550<br />Cockpit crew:<br />2.<br />Passengers:<br />14 – 18.<br />Cabin length:<br />15,27 m.<br />Cabin diameter:<br />2,24 m.<br />Cabin height:<br />1,88 m.<br />Cabin volume:<br />47,3 m³.<br />Baggage compartment:<br />6,4 m³.<br />Wing span:<br />28,50 m.<br />Fuselage length:<br />29,39 m.<br />Height:<br />7,87 m.<br />Engines:<br />two Rolls Royce BR710 C4-11 each rated 68.4 kN.<br />Weight:<br />- basic operating weight with 4 crew: 21.909 Kg.<br />- max. zero<br />-fuel weight: 24.721 Kg.- fuel: 18.733 kg.<br />- max. payload: 2.812 Kg.<br />Max. take off weight:<br />41.277 Kg.<br />Max. landing weight:<br />34.156 Kg.<br />Cruise speed:<br />946 km/h.<br />Service ceiling:<br />12.497 m.<br />Max. ceiling:<br />15.545 m.<br />Max. range:<br />12.501 km.<br />Performance:<br />- take-off run 1.800 m at max. take-off weight.<br />- landing run 844 m at max. landing weight.<br /><br />Nadhani kuna umuhimu wa kufahamu haya.Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-55502635006033086152009-11-18T15:53:00.000+03:002009-11-18T15:56:19.391+03:00KUUELEWA MFUMO WA UTAWALA WA KIFISADINa. M. M. Mwanakijiji<br /><br />Maadui wa Tanzania siyo Rostam, Lowassa, Chenge, Mramba, Yona au mtu yeyote ambaye ameonakana na kutajwa kuwa ni fisadi au kuhusishwa na kashfa za kifisadi. Hawa wote na wengine wengi ambao nimewabatiza majina ya “makuwadi wa ufisadi” na “vikaragosi vya ufisadi” ni matokeo tu ya yule adui yetu namba moja ambaye bila ya kumshughulikia basi juhudi zote za kupigana na “ufisadi” zitakuwa ni kama juhudi za anayezama majini huku kwa hasira akiyapiga ngumi maji hayo ili “kuyakomoa”. Ni zoezi lisilo na tija.<br /><br />Anayepigana vita dhidi ya ufisadi (awe ndani ya CCM au nje yake) akifikiria kuwa anapigana dhidi ya watu “fulani” basi hajajua uzito wa vita hii iliyo mbele yetu; vita ambayo hatukuitafuta bali tumejikuta tunalazimika kuipigana kwani imeletwa kwetu bila kumchokoza mtu na haitaondoka isipokuwa kwa kuishinda tu.<br /><br />Tukijifunza katika vita ya Kagera tunaweza kuona kuwa lingekuwa kosa kubwa sana kwa wapiganaji wetu kuwaadhibu wanajeshi wa UPDF (Jeshi la Wananchi wa Uganda) tukifikiria kuwa wao ndio walikuwa adui zetu. Tunaelewa kwamba wanajeshi wale walikuwa wanatekeleza amri ya vita toka kwa amiri Jeshi Mkuu wao wa wakati ule Idi Amin Dada. Sasa kama tungepigana ili kushinda wapiganaji wa Uganda kwenye jukwaa la vita halafu basi tungechekwa na jumuiya ya kimataifa kwa kutokuelewa tulipigana dhidi ya nani hasa.<br /><br />Adui yetu wakati ule ulikuwa ni utawala wa Nduli Idi Amin na mfumo mzima wa utawala wake uliosababisha sisi twende vitani licha ya juhudi zote za kuepuka vita kuchukuliwa na kushindikana. Ndio sababu wakati wa tangazo la vita kwa Taifa letu Baba wa Taifa aliweka lengo lililokuwa wazi kabisa, kuyarudisha majeshi ya Amin toka ardhi yetu (kama kuwarudisha nyuma makuwadi wa ufisadi), kumkata makali Amin kabisa asiweze kuthubutu kutuvamia na kuwa tishio kwetu tena.(kama kuwakata makali mafisadi wasipate nafasi za kuchukua pesa zetu).<br /><br />Katika hilo lengo la pili vikosi vyetu vilipewa jukumu la kuhakikisha vinammaliza kabisa adui na kuhakikisha kuwa habakii tena madarakani. Hivyo, tunajifunza kutoka vita vya Uganda kuwa haikutosha kumrudisha adui nyuma au kuyatoa majeshi yake toka ardhi yetu; ilitupasa kuhakikisha kuwa adui hapati tena nafasi ya kuthubutu kutishia mpaka wetu na hivyo licha ya kuingia Uganda hadi Kampala, vikosi vyetu vilisonga mbele hadi Jinja na Entebbe na kusababisha Idi Amin kuachia ngazi na kukimbia taifa lake kwa aibu.<br /><br />Vikosi vyetu havikuondoka Uganda mara tu baada ya Amin kutoroka bali baadhi ya wapiganaji wetu walibakia Uganda kusaidia katika ujenzi wa taifa hilo na hasa ujenzi wa jeshi jipya lisilokuwa tishio kwa majirani zake kwa kutoa mafunzo na kulinda amani wakati jeshi la Uganda linapangwa upya.<br /><br />Vita ya ufisadi nayo ni vivyo hivyo. Wale tunaowaita mafisadi, makuwadi wa ufisadi, vikaragosi vya ufisadi ni watumishi wanaofaidika na mfumo wa utawala wa kifisadi. Ndugu zangu, adui nambari moja wa maendeleo na mafanikio ya Watanzania ni mfumo haramu uliotengenezwa na utawala wa kifisadi. Ni lazima kwa mpiganaji yeyote kuelewa mfumo huu unavyofanya kazi kwani wale wote tunaowaita mafisadi leo hii ni matokeo ya mfumo huu wa kiutawala; mfumo ambao ni mchanganyiko wa mifumo midogo midogo ya kisiasa, kiuchumi, na kisheria ambayo msingi wake ni ubinafsi, kutokuwajibika, kulindana, utawala wa hofu, kubebana na kuvumiliana kwa kadiri ya kwamba wanufaikaji ni kikundi cha watu wachache walio katika utawala na wale wanaohusiana nao kwa karibu.<br /><br /><br />Mfumo wa utawala wa kifisadi ni nini basi?<br />Ni muungano wa utendaji kazi wa mifumo ya kisiasa, uchumi, na kisheria ambao msingi wake ni kujitajirisha kwa haraka haraka pasipo kuogopa matokeo yake. Mfumo wa kifisadi unahusiana moja kwa moja na utajiri wa “haraka haraka” ambao unafanywa kwa kulainisha utendaji kazi wa vyombo mbalimbali vya dola vyote vikitengeneza kama mwamvuli mkubwa kwa watawala. Lengo kubwa la mfumo huo ni kuwalinda watawala.<br /><br />“Mfumo” ni nini hasa?<br />Mfumo yaani “system” kwa kiingereza unaweza kuelezewa kama muunganiko wa michakato, kanuni, shughuli mbalimbali vikifanya kazi kwa pamoja kufikia lengo moja. Neno “system” linatokana na neon la Kigiriki “systema” yaani “kuleta pamoja”. Ndani ya mfumo mmoja mkubwa unaoweza kuzaa mifumo mingine midogo midogo ikifanya kazi mahsusi lakini yote ikitekeleza lengo moja kubwa.<br /><br />Mfano mzuri hapa ni wa kutumia motokari (gari). Lengo kubwa la gari ni uwezo wake wa kuendeshwa. Hivyo, ukiona gari linakwenda basi unajua kuwa lengo lake limefanikiwa na wakati wowote ukiona gari linazimika zimika au kukwama kwama basi unajua kuna tatizo fulani. Mafundi wa magari wanapoletewa gari bovu wanauliza tatizo nini au dalili gani dereva aliziona. Katika kufanya hivyo fundi-gari anaanza kufikilia ni mfumo gani mdogo (sub-system) wenye tatizo.<br /><br />Ataangalia mafuta ya breki, mafuta ya injini, maji ya kupoozea, oili n.k na kama gari haliwaki kabisa likiwaswa basi ataangalia kama stata bado inafanya kazi, betri kama bado ina nguvu n.k Ni katika kuiangalia hii mifumo midogo midogo ndivyo anaweza kugundua tatizo na kulishughulikia na hatimaye kulirudisha gari barabarani.<br /><br />Mfano mwingine mzuri ni wa kuelewa mfumo wa mwanadamu. Mwanadamu ameumbwa akiwa na mifumo mikubwa mikubwa na mingine midogo midogo lakini yote ikifanya kazi kuhakikisha mtu huyo ni hai na anaishi kwa afya. Wengi tunaifahamu mifumo ile mikubwa ya mwili kama Mfumo wa Fahamu (nervous system), mfumo wa chakula (digestive system), mfumo wa Uzazi (Reproductive System), mfumo wa utoaji uchafu mwilini, mfumo wa pumzi, na mfumo wa damu. Ndani ya mifumo hii mikubwa ipo mifumo mingine midogo midogo na yote hii ikifanya kazi “kwa pamoja” inafikia lengo la kutufanya tuwe na afya na kuendelea kuishi.<br /><br />Kunapotokea tatizo kwenye mfumo wowote kati ya hiyo mtu atajikuta ni mgonjwa na maendeleo ya sayansi na teknolojia leo hii kunawezesha baadhi ya mifumo kusaidiwa kufanya kazi na mashine mbalimbali.<br /><br />Madaktari wote na wauguzi na wataalamu mbalimbali wa tiba wanajifunza juu ya mifumo hii na ile mingine na kwa kadiri ya taaluma zao wengine wanajikuta wanasomea zaidi utendaji kazi wa mfumo mmoja maalum na kuwa mabingwa wa eneo hilo. Vivyo hivyo wataalamu wa magari wapo ambao wamekubuhu katika mambo ya umeme wa magari na wengine katika injini n.k<br /><br />Katika haya yote, mifumo hii inaangaliwa kwa ukaribu wake na ni msingi wa kuelewa utendaji kazi wa gari, kiumbe au kitu chochote kinachohusisha mfumo zaidi ya mmoja. Ni kwa sababu hiyo basi ni muhimu kuelewa kuwa mfumo wa utawala wa kifisadi huundwa na utendaji kazi wa mifumo mikubwa mitatu ambayo ndiyo huwezesha mfumo huo kufanya kazi yake ya kukitengenezea kikundi cha watu wachache utajiri wa haraka haraka bila kuogopa matokeo yake. Kimsingi kabisa, mfumo wa utawala wa kifisadi umejengwa ili kunyonya na kukandamiza.<br /><br />Ni mifumo ipi inayounda mfumo huu?<br />Kama nilivyodokeza hapo juu mfumo wa utawala wa kifisadi huundwa na utendaji kazi wa mifumo ya kisiasa, kisheria, na kiuchumi. Mifumo hii mitatu ikifanya kazi kwa pamoja huuisha utawala wa kifisadi, uupa nguvu na kuufanya udumu. Tuangalie mifumo hii mitatu jinsi ilivyo katika Tanzania.<br /><br />Mfumo wa Kisiasa:<br />Mfumo wetu wa kisiasa umetengenezwa ili kulinda maslahi ya kikundi cha watu walio madarakani. Haujatengenezwa ili kuruhusu ushindani wa haki wa kisiasa, na hauruhusu changamoto ya kweli ya siasa za kidemokrasia. Utaona kuwa katika mfumo wetu wa kisiasa, katiba ya nchi inaelezea juu ya ujenzi wa taifa la kijamaa na ile ya chama tawala nayo ikisema hivyo hivyo. Hata hivyo hakuna mtu yeyote ndani ya serikali ya sasa au kwenye chama anayeweza kutetea ujamaa leo hii au kutuelezea ni “ujamaa” wa aina gani wanauunda.<br /><br />Maana yake ni kuwa, watawala waliopo sasa hawajali hasa katiba inasema nini kwani kwao katiba ni kama mapendekezo ya aina fulani tu na siyo mkataba unaowafunga watawala kwa watawaliwa. Leo hii siyo Kikwete, Makamba wala Kingunge wanaoweza kutuambia ni aina gani ya ujamaa wanaoutekeleza kwa mujibu wa Katiba.<br /><br />Ni mfumo ambao umewekeza nguvu kwenye chama cha kisiasa kiasi kwamba watu wachache kwenye chama hicho wanaweza kutuamulia ni nani anakuwa Rais wetu au Spika wetu wakiamua tu kumvua uanachama. Ni mfumo ambao unafanya geresha ya demokrasia kwa kufanya uchaguzi wa vyama vingi huku mfumo wa sheria walioutengeneza ukizuia kabisa uchaguzi huru na wa haki.<br /><br />Hivyo, mfumo wa kisiasa wa kwetu ni kiinimacho cha siasa za kidemokrasia kwani ndani yake kuna vizuizi vingi vya utendaji kazi wa demokrasia; kutokuwepo kwa tume huru ya uchaguzi, matokeo ya uchaguzi wa rais hayawi rasmi hadi tume isiyo huru itangaze, kukataza wagombea huru, ukosefu wa chombo cha kusimamia Bunge, n.k<br /><br />Mfumo wa Kisheria<br />Mfumo wetu wa kisheria katika utawala wa kifisadi umeundwa ili kuondoa hasira na siyo kushughulikia tatizo lenyewe hasa linalosumbua jamii. Kwa kiasi kikubwa utaona kuwa sheria mbalimbali zimeundwa zikiwa na majina mazuri na ya kupendeza lakini zikiangaliwa kwa karibu utaona kuwa zimeundwa ili kuwafanya watu wasikasirike sana.<br /><br />Sheria mbalimbali zilizotungwa kwenye utawala wa kifisadi zimetengenezwa ili kuzuia watu wasijichukulie sheria mikononi lakini wakati huo huo kutoa ulinzi wa aina yake kwa wahalifu wanasiasa.<br /><br />Mojawapo ya vitu ambavyo vimeondolewa kwenye sheria nyingi ambazo zingeweza kuwakamata wanasiasa na watendaji wazembe ni kile ambacho tunakiita kama “trigger clauses”. Kwamba endapo kitu x kitatokea basi mtu y atachukuliwa hatua zifuatazo. Kwa mfano, endapo mtendaji anatakiwa kutoa maelezo na Mkaguzi Mkuu ya matumizi ya shilingi milioni 300 na akashindwa nini kimtokee? Utaona sheria zetu haziko wazi zaidi ya kumpa CAG uwezo wa kuonesha au kutoa maelekezo kuwa huyo “y” achunguzwe au kuchukuliwa hatua “zinazopasa”.<br /><br />Utaona kuwa sheria zetu zina matundu ya makusudi kabisa yenye kuzuia utekelezaji wake wa mara moja na hivyo matundu hayo yamekuwa ni kinga kubwa ya makuwadi wa ufisadi kwani wanajua kabisa kuwa mtu akitaka kuzifuata sheria hizo atajikuta anashindwa kabla hajafika mbali.<br /><br />Hivyo, mfumo wetu wa kisheria umeundwa ili kuzuia hasira lakini kushindwa kuzuia vitendo vya ufisadi uliokubuhu. Mtu yeyote anayesoma sheria ya kupambana na kuzuia rushwa, sheria ya madini, sheria ya usalama wa taifa na sheria ya makosa ya kuhujumu uchumi utaona kuwa watawala wamezitengeneza ili zisifanikiwe. Na hivi karibuni watawala hao hao wamepunguza nguvu ya baadhi ya sheria hizo kwa sababu wanajua akiingia mtu kichaa kwenye ofisi ya DPP kuna watu wengi watatiwa pingu.<br /><br />Mara zote kwenye utawala wa kifisadi, watawala hutumia mianya mbalimbali kuvuruga utawala wa sheria ili kujikinga na mashtaka huko mbeleni. Ndio maana leo hii tuna mtu ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu kwa miaka 10 na ambaye yeye mwenyewe anashtumiwa kwa uvunjaji mkubwa wa sheria lakini hakuna mtu mwenye ubavu wa kunyosha kidole na badala yake anakingiwa kifua; ndio maana leo hii baadhi ya “watunga sheria” wetu ndio wale wale wanaotajwa kwenye baadhi ya uvunjaji mkubwa kabisa wa sheria katika jamhuri yetu.<br /><br />Mfumo wa kiuchumi<br />Katika utawala wa kifisadi, mfumo wa kiuchumi hufanana na mfumo wa kiuchumi katika utawala wa kidemokrasia. Ukiangalia kwa juu juu mfumo wa kiuchumi unaundwa na taasisi kama zile zilizopo kwenye nchi za kidemokrasia na ukisoma maandishi mbalimbali unaweza kabisa kuamini kuwa mfumo huo wa uchumi katika utawala wa kifisadi unalingana kiutendaji na mfumo wa kiuchumi katika utawala wa kidemokrasia. Hili si kweli.<br /><br />Unapokuwa na mfumo mbovu wa kisiasa na kisheria, mfumo wa kiuchumi nao hauwezi kuwa salama. Kwa maneno mengine, mfumo wa kiuchumi hauwezi kusalimika pale ambapo mfumo wa kisiasa na ule wa kisheria inapokuwa matatani. Mara zote ubovu wa mfumo wa kisheria na kisiasa huonekana katika ubovu wa mfumo wa kiuchumi.<br /><br />Katika Tanzania ya leo hii tunaweza kujiuliza ni mfumo wa aina gani wa kiuchumi tunaoufuata? Je ni ubepari au ujamaa? Je ni mchanganyiko wa aina hizo mbili na kwa namna gani? Mara nyingi utamsikia Kikwete na wanasiasa wengine wa CCM wakielezea juu ya “mfumo wa Soko” au mfumo wa “ushindani” je hii kiitikadi ina maana gani? Je, ni mashindano kati ya tajiri na maskini, aliyenacho na asiyenacho, mwanaCCM na asiye mwanaCCM?<br /><br />Na hata wakati mwingine unaposikia takwimu mbalimbali za kiuchumi toka Benki Kuu hatuna budi kujiuliza hivi ni kweli takwimu hizo ziko sahihi kwa kiasi gani? Kwenye nchi ambayo uzalishaji unafanyika kwa zaidi ya asilimia 90 kwa njia zisizorasmishwa tunaweza vipi kuelezea kwa uhakika hali ya kiuchumi? Kwenye nchi ambapo asilimia zaidi ya 20 (Kikwete hivi karibuni alidai asilimia 30) ya bajeti inaishia kwenye vitendo vya rushwa na ufisadi, unaweza vipi kuelezea kuwa mfumuko wa bei uko chini ya tarakimu mbili?<br /><br />Unawezaje kuelezea “kukua kwa uchumi” na ukawa sahihi kwenye taifa ambalo madini yake haijulikani kwa hakika ni kiasi gani kinatolewa nje na mahali ambapo makampuni yanaweza kusafirisha nje faida yao kwa asilimia 100 huku yakitangaza kupata hasara kila mwaka kwa mujibu wa sheria nyingine tuliyowatengenezea?<br /><br />Tunaweza vipi kupima kwa haki pato la mwananchi wakati sehemu ya pato hilo ni lile linalotokana na rushwa kidogo? Unaposema bei ya kitu (bidhaa au huduma) ni kiasi fulani lakini wakati huo huo mtu anatakiwa kubajeti ndani yake “kitu kidogo” juu ya bei hiyo, mchumi anapopiga hesabu zake anachukulia na hicho “kitu kidogo” ndani au hapana?<br /><br />Kimsingi utaona kuwa katika mfumo wa utawala wa kifisadi, mfumo wa uchumi ni wa kudanganya. Yaani, taarifa rasmi za kiuchumi haziakisi ukweli hasa wa shughuli za kiuchumi na uwezo wa uchumi huo (kwa uzuri au kwa ubaya). Matokeo yake wakati mwingine watu wanaamini kuwa uchumi wao unafanya kazi vizuri zaidi wakati hiyo “vizuri zaidi” ni kwa sababu ya vitendo vya kifisadi.<br /><br />Ndio maana kuna baadhi ya watu wanaamini kabisa kuwa endapo ufisadi utapigwa marufuku kabisa na kila mtu kulazimishwa kuishi kwa haki kunaweza kutokea maandamano makubwa sana. Kwani kwa mara ya kwanza, watu watatakiwa kuishi kwa uhalisi wa vipato na matumizi yao.<br /><br />Sasa basi, tunaweza kuona kuwa mafisadi waliopo sasa ni mazao ya mfumo uliopo sasa hivi. Hata tukiweza kuwaangusha na kuwatia pingu mafisadi wote bado tutakuwa na kizazi kipya cha mafisadi kwani mfumo uliowatengeneza bado upo.<br /><br />Itakuwa ni sawasawa na kiwanda cha kutengeneza magari; kama kuna mahali ambapo mashine moja haiingizi breki kwa usawa kwenye gari, basi magari yatakayotoka yatakuwa na matatizo na breki zake. Watu watapata ajali na mengine itabidi yaondolewe barabarani. Lakini kama suluhisho ni kuondoa magari mabovu ambayo tunajua yanatoka kwenye kiwanda fulani lakini wakati huo huo kiwanda bado kinatengeneza magari mabovu kwa sababu sehemu ya mashine yake (mfumo wake mmoja au zaidi) imeharibika basi tutakuwa tunacheza “pata potea”.<br /><br />Suluhisho siyo tu kuondoa magari mabovu barabarani bali vile vile kurekebisha mashine kiwandani ili zisitengeneze gari lenye matatizo ya breki.<br /><br />Leo hii ninachosikia ni watu kulalamikia “mafisadi” (magari mabovu), watu wanapiga kelele ni kwa kadiri gani mafisadi wameifisadi nchi n.k lakini sijamsikia hata mtu mmoja mwenye ujasiri wa kusema kuwa tatizo letu ni “kiwanda”.<br /><br />Ndio maana nimesema awali kuwa tatizo letu siyo Rostam, Lowassa, Chenge au Yona; hawa ni dalili tu ambazo tunaweza kuziondoa barabarani. Tutakuwa hatuna hekima kama tunaamini kuwa tukiwaondoa hawa toka madarakani basi ufisadi utakwisha. Tusipobadilisha mfumo wa kiutawala ufisadi tutaendelea kuzalisha mafisadi tu. Haijalishi ni chama gani kiko madarakani.<br /><br />Ndio sababu, tunapowasikiliza wanaotaka kugombea mwakani hatuna budi kujiuliza na kuwauliza wao, wanampango gani wa kuubadilisha mfumo wa kiutawala wa ufisadi badala ya kuwashughulikia mafisadi wa sasa tu? Watafanya nini kuurekebisha mfumo wetu wa kiutawala ili usitoe mafisadi na vifaranga vyao?<br /><br />Ni katika kuelewa hili ndipo tunaweza kuelewa kuwa adui yetu wa kwanza kabisa katika vita hii ni mfumo wa utawala wa kifisadi. Lakini ni nani huyu aliyejemedari aliyeuunda, kuupanga, na kuusimamia mfumo huu wa kifisadi kiasi kwamba tunavuna matunda yake machungu leo hii? Ni nani huyo ambaye anapaswa kuzuiliwa asiendelee kutufyatulia matofali ya mchanga mtupu kujengea taifa letu? Wengine, wanafikiria ni mtu mmoja au kikundi cha mafisasdi.<br /><br />Mimi napendekeza; ni mfumo wa utawala wa Chama cha Mapinduzi. Unabisha?<br /><br />Niandikie:<br /><br />mwanakijiji@mwanakijiji.comKyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-77731703471919109092009-11-17T22:03:00.000+03:002009-11-17T22:03:00.408+03:00Mo Ibrahim: Viongozi Afrika hawako makiniMMILIKI wa taasisi ya Mo Ibrahim amesema matatizo yote yanayoikumba nchi za bara la Afrika, ikiwemo vita, njaa na magonjwa, yanatokana na viongozi wake kutokuwa makini na kutofuata misingi ya utawala bora.<br /><br />"Viongozi wetu wengi si makini na pia hawafuati misingi ya utawala bora na kutokana na haya ndio maana bara hili bado lipo nyuma kiuchumi na linasumbuliwa na matatizo ya njaa, magonjwa na vita," alisema mmiliki huyo, Mo Ibrahim jijini Dar es Salaam juzi katika hafla maalum ya muziki ikiwa ni sehemu ya maadalizi ya mkutano uliofanyika jana kwenye ukumbi wa Mlimani City.<br /><br />Katika mkutano uliokutanisha viongozi mbalimbali kutoka nchi za bara la Afrika, pamoja na mambo mengine walijadili masuala mbalimbali yakiwemo ya mabadiliko ya hali ya hewa, kilimo na maendeleo ya nchi za Afrika.<br /><br />Mo Ibrahim, ambaye ni milionea alifafanua kwamba viongozi wa nchi za Afrika ni wepesi wa kuzungumza lakini si watendaji katika kufanikisha mipango ya maendeleo ya wananchi wanaowaongoza.<br /><br />Alisema kutokana na hali hiyo, Afrika inaonekana ni bara masikini na lenye matatizo mengi ikiwa ni pamoja na vita, njaa na magonjwa.<br /><br />"Kutokana na rasilimali tulizonazo katika nchi zetu hapa Afrika, hakuna sababu ya kuwa nyuma kiuchumi na wala kukumbwa na matatizo ya magonjwa, vita na njaa. Lakini haya ni kutokana na kutotekelezwa ipasavyo na kwa vitendo mipango ya maendeleo inayokuwa inawekwa na viongozi wetu," alisema<br /><br />Hata hivyo, Mo Ibrahim alisema bado kuna nafasi kwa viongozi wa Afrika kufanya jitihada zaidi kwa lengo la kufaniksha uchumi wa bara hili ili uachane na utegemezi kwa nchi za barani Ulaya, Amerika na Asia.<br /><br />"Ni wakati sasa kwa viongozi na Waafrika kujiamini katika mipango yao na kuachana na tabia ya kutegemea kusaidiwa katika kila kitu," alisema tajiri huyo.<br /><br />"Ni muhimu tukafikiria maisha ya baadaye ya watoto wetu yatakuwaje endapo hali itaendelea kama ilivyo sasa katika bara hili zuri na lililojaa mali."Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-3769445952068143358.post-5880419285465158862009-11-16T11:08:00.000+03:002009-11-16T11:33:16.235+03:00Selelii awazima Lowassa na Rostam<ul><li>Adai Kikwete alikabidhiwa mapema ripoti ya Richmond </li><li>Asema kama kumuokoa ni yeye aliyepaswa kufanya hivyo </li></ul>Na Saed Kubenea<br />MwanaHALISI<br /><br />JUHUDI za mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na mwenzake wa Igunga, Rostam Aziz kutaka kujivua na gome la Richmond zimezimwa, MwanaHALISI limeelezwa.<br /><br />Taarifa kutoka ndani ya kikao cha kamati ya wazee wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichofanyika Dodoma wiki iliyopita, zinamtaja mbunge wa Nzega Lucas Selelii kuwa ndiye aliyezima ndoto za Lowassa na Rostam kujisafisha.<br /><br />Inaelezwa kwamba Selii alizima ndoto za Rostam na Lowassa baada ya kuanika ushiriki mzima wa wanasiasa hao wawili katika mkataba huo. Mkutano kati ya kamati ya wazee na wabunge ulifanyika siku tatu mfululizo katika ukumbi wa zamani wa Bunge mjini Dodoma.<br /><br />Akiongea kwa kujiamini na kuchambua hoja moja baada ya nyingine, Selelii alisema Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond ambapo yeye alikuwa mmoja wa wajumbe wake inaoushahidi kwamba Richmond ni mali ya Rostam.<br /><br />Kwa upande wa Lowassa, Selelii alisema alibeba kampuni hiyo kwa maslahi ya binafsi ya rafiki yake huyo.<br /><br />Akiongea baada ya Rostam kukana kumiliki kampuni hiyo na kutaka kuundwa kwa Tume huru kuchunguza mkataba huo, Selelii alisema <strong>“Rostam amewadanganya kwa kusema hahusiki na Richmond.”</strong><br /><br /><strong>“Huyu Rostam ndiye aliyetafuta nyumba kwa ajili ya matumizi ya ofisi ya Richmond. Ni yeye aliyelipia pango la nyumba hiyo,” alisema Selelii huku akitolea macho Rostam. Alisema, “Kamati yetu ilihakikishiwa na mtoto wa Mucadam (Hussen Mucadam) ambaye ndiye mwenye nyumba kwamba nyumba iliyotumiwa na Richmond ilipangwa na Rostam.</strong><br /><strong></strong><br />”Huku wabunge na wajumbe wa kamati ya wazee wakiwa wamepigwa na butwaa, Selelii alisema <strong>“hata jopo la waadishi wa habari lililofanya kazi ya kusafisha Richmond lilitafutwa na Rostam.”</strong><br /><br /><strong>Alisema Rostam alifikia hatua ya kutumia waandishi hao wa habari mara baada ya vyombo vya habari kuanza kueleza utata wa mkataba. “Ni huyu Rostam aliyekodisha jopo la waandishi wa habari watatu mashuhuri nchini kwa ajili ya kupoza makali. Tumezungumza na waandishi wa habari hawa mmoja baada mwingine na wote wametuthibitishia hili,” alisema Selelii.</strong><br /><strong></strong><br /><strong>Alitaja hata majina ya waandishi hao kuwa ni Gideon Shoo, Jimmy Mdoe na Salva Rweyemamu</strong> ambaye sasa ni mkurugenzi wa mawasiliano ya rais. Tarehe 29 Juni 2006, serikali kupitia Shirika la Umeme la Taifa (Tanesco) ilisaini mkataba wa kufua umeme wa megawati 100 na kampuni ya Richmond Development Company (LLC) bila kwanza kuhakiki uhalali wa kampuni hiyo.<br /><br />“Kama hahusiki kwa nini aliwatafuta hawa waandishi wa habari? Kwa nini aliwapa kazi,” alihoji Selelii.Alisema mbali na waandishi wa habari na utafutaji wa nyumba, Kamati Teule iliweza kuthibitisha kwamba baada ya Richmond kuhuisha mkataba wake kwa Dowans, wafanyakazi watatu wa Caspian walionekana katika Dowans.“Kwa maana nyingine, Dowans, Richmond na Caspian ni baba mmoja mama mmoja.”<br /><br /><strong>Alisema Kamati Teule imepata ushahidi kwamba “fedha za Dowans zilihamishiwa katika akaunti ya Caspian; Rostam alikuwa akifuatilia mwenyewe fedha hizo hazina,” alisisitiza Selelii.</strong><br /><br />Mbunge mmoja wa Bunge la Muungano aliliambia MwanaHALISI kwamba wakati Selelii akieleza wajumbe taarifa hiyo, ukumbi mzima ulikuwa kimya.<br /><br /><strong>“Hata sindano kama ingeanguka, ingeweza kusikika. Nakuambia yule jamaa jinsi alivyokuwa akiongea kwa upole na taratibu, kila mtu alikuwa na shauku ya kumsikiliza,” alisema.</strong><br /><br /><strong>Anasema, “Rostam alikuwa amekaa kimya. Alikuwa kama vile amelowa mvua.”Baada ya kueleza ushiriki wa Rostam Selelii aliyeongea kwa kupanga hoja zake alirukia Makongoro Mahanga, mbunge wa Ukonga, ambaye awali alidai kuwa “ripoti ya Bunge ilikuwa feki.”</strong><br /><br />Makongoro amesema “ripoti yetu ni feki; Kamati Teule haikumshirikisha Rais Jakaya Kikwete. Haikumueleza; kama angeelezwa angemuokoa Lowassa,” alisema Selelii kwa taratibu. Alisema madai hayo ya Mahanga hayana ukweli, na kwamba yamelenga kuhamishia tatizo kwa wengine. Alihoji: Kama ripoti ilikuwa feki inawezekanaje rais aliyepewa taarifa hiyo kabla ya kuwasilishwa bungeni akaiamini?<br /><br />Kuhusu Kamati Teule kutomshirikisha rais Kikwete, Selelii alisema kabla ya kamati kuwasilisha ripoti yake bungeni ilikabidhi ripoti kwa rais. Selelii alikuwa akijibu hoja ya Andrew Chenge na Mahanga waliotumia muda mrefu kueleza kikao juu ya kutoshirikishwa rais Kikwete. Alisema, “Rais alikuwapo hapa Dodoma wakati mjadala wa Richmond unafukuta. Tayari alikuwa na ripoti yetu. Sasa kwa nini yeye hakumpa waziri mkuu wake,” alihoji Selelii na kuongeza, “haikuwa kazi ya kamati kumpa ripoti Lowassa.”<br /><br />Alisema, Rais ana vyombo vya ulinzi na usalama. Je, kama yeye mwenye vyombo hivi hakuona kasoro, nani mwingine mwenye mamlaka ya kudai kuwa ripoti yetu ilikuwa feki,” alihoji.<br /><br />Akiongea huku akionekana mwenye hasira, lakini kwa taratibu mno, Selelii alisema, “mnaleta umbeya hapa eti rais hakujua haya. Rais tulimpa ripoti hii kabla ya kuwasilisha bungeni.” Taarifa zinasema Selelii alikiambia kikao hicho kwamba Kamati Teule imefanya kazi yake kwa kufuata misingi ya sheria. “Duniani kote mtuhumiwa hawezi kupewa taarifa ya kilichomo katika ushahidi hadi pale suala hilo linapoingia mahakamani. Katika hili Lowassa hana wa kumlaumu,” Selelii alisisitiza.<br /><br /><strong>Baada ya kumaliza kuumbua Mahanga, Selelii aligeukia Sophia Simba ambaye alituhumu Kamati Teule kuwa imemuonea Lowassa na kumvua nguo mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela na mumewe Joh Malecela. Katika hilo, Selelii alisema, “Sophia Simba huyu ni mwenyekiti Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT). Pia ni waziri anayesimamia utawara bora,” chanzo cha habari ndani ya kamati kinanukuu Selelii. Anasema, “aliyoyasema hapa hayakustahili kutolewa katika kikao hiki. Haya ni maneno yanayopaswa kutolewa kwenye kitchen party. Nimemsikiliza kwa makini, mheshimiwa Simba amezungumza mambo binafsi yanayohusu mtu binafsi,” alisema. </strong><br /><br />Mbili, Selii alisema, “Sophia Simba amesema hapa kuwa Lowassa ni mwanamme namba moja. Ni mwanamme wa shoka. Akimaanisha kwamba wanaume wote akiwamo rais, waziri mkuu, wabunge na madiwani siyo kitu. Mimi sikubaliani naye. Labda kama mwanamme wa shoka katika masuala mengine,” alisema kwa kujiamini.<br /><br />MwanaHALISI limefahamishwa kuwa mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge, Dk. Harrison Mwakyembe alikabidhi ripoti ya kamati yake kwa Spika wa Bunge, Samwel Sitta 31 Desemba 2007.<br /><br />Mara baada ya Sitta kupokea ripoti ya Mwakyembe aliondoka nchini kwenda Uingereza kuhudhuria mkutano wa Bunge la Jumuiya ya Madola.Taarifa zinasema mara baada ya Sitta kurejea nchini alikabidhi ripoti hiyo kwa rais Kikwete. Hiyo ilikuwa 29 Januari 2008; kabla ya Kikwete kuelekea Addis Ababa, Ethiopia kuhudhuria mkutano wa viongozi wakuu wa Afrika (AU).<br /><br />Rais Kikwete alisafiri kuelekea Ethiopia 29 Januari 2007. Alirejea nchini 5 Februari 2008. Lowassa alikabidhiwa ripoti na Sitta 6 Februari 2009.“Kwa mujibu wa kanuni za Bunge, iwapo nitakupa ripoti hii, sharti nifanye hivyo pia kwa kiongozi wa upinzani,” Sitta alinukuliwa akimueleza Lowassa.<br /><br />Baada ya Sitta kumkabidhi Lowassa ripoti hiyo, alimkabidhi ripoti hiyo “Kiongozi wa Kambi ya upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohammed,” taarifa zinaeleza.<br /><br /><strong>Kwa upande wake, Sitta amekana kuwa Rostam aliwahi kuwasuluhisha yeye na Lowassa. “Ni uwongo mtupu. Mimi sijawahi kusuluhishwa na Lowassa. Kwanza, hatukuwa na ugomvi, sasa kwa nini tusulihishwe,” alihoji Sitta. Alisema madai ya Rostam kwamba Sitta alitaka nyumba yenye hadhi Dar es Salaam na Urambo hayana msingi, kwa kuwa suala la makazi ya spika hupangwa na katibu mkuu kiongozi.<br /><br /></strong>Kyela Community Initiativeshttp://www.blogger.com/profile/11935115572769261160noreply@blogger.com0